Inasikitisha sana kama polisi badala ya kuwalinda rai wanawauwa kwa sababu ya kuandamana kwa gharama zao. Hii si haki na Polisi hao wanatakiwa kushitakiwa kwa Ocampo!
Poleni sana watu wa Arusha.
Hik! Hik! "Waliandamana CUF mkawabeza. WAHUNI WALE WAVAA BUIBUI NA VIBALAGHASHIA. waliuawa watu wengi kule pemba mkazidi kubeza. Leo mnasema CUF ni CCM-B. Mlisahau historia ya mapambano na DIRA ya siasa na uzalendo wa kitaifa. Aliwahi kuvunjwa mkono Profesa wa UCHUMI mkabeza eti Profesa uchwara. SASA ONJENI SHUBIRI HIYO NA MJUE SERIKALI IPO. NGOMA IKILIA SANA MWISHOWE HUPASUKA. Sifurahii ila nakumbushia!! viva Dr. Slaa dr wa ukweli" Hik!
Mlevi mwingine huyooooo... Tabu ya kunywa gongo 24/7 bila kula... kichwani HK
Issue hapa ni kesi gani? Wanaweza kushitakiwa kwa uhaini ama hata mauaji ya polisi kama watakua wanataka shari, ila kama ni kuepusha shari kesi itakua kuandamana bila kibali na wataachiwa kwa dhamana.
poleni viongozi wetu tuko pamoja tunajua hizi ni njama tu za ccm, na ccm kama hawajui wanazidi kupandikiza chuki kwa watanzania na huu ndio mwanzo wao wa kupotea kisiasa itabaki historia tu kama ilivyo kuwa kanu na vyama vingine vikongwe
siku hizi JF ina junior members wengi lakini wanazungumza kama seniors!!
wewe umeiskiliza saa ngapi? umeisikia mwenyewe? jee lugha inapanda? Unaelewa ung'enge?
Nonda habari hizi ni za kweli bofya bbcswahili km wenzako wanavyoelekeza.
jb sahihi ni waandishi wetu wa Arusha watakapotuletea habari za Mochwari, km ni uongo bbcswahili si waaminifu watachochea uongo kwani kupoteza ndugu kwa ajili ya kututetea inauma
Poleni wananchi wa Arusha
mahakamani kwa kosa gani? Sasa hao ndo wanataka kusababisha wananchi wafanye fujo ambayo aijawai tokea hapo arusha washindwe kuwapeleka mafisadi papa waje kuwapeleka wakombozi wa taifa hili? Tunawaombea mtakuwa salama na haki itapatikana
Naomba sana wanaCCM na hasa swahiba Kibs wasisahau kwamba when you fight with your son who is at the adolescent age, you are bound to be humiliated....
Arusha is the Geneva of africa... they would have chosen the better battle field not arusha
tourism industry is already damaged... while allowing the matching would have just ended with followers feeling fools of themselves
EAF's hub is arusha, i cant imagine how Kenyans are smiling right now
While you think you are slapping your wife, just remember your neighbours are enjoying your degradation
How wrong did the government go on this? no one knows
Kama vile mbegu iendapo ardhini kwa kuupoteza uhai wake ndivyo huchipua uhai ule ule katika mbegu nyingi. Watu hawa waliouawa Arusha na huyu rpc a.k.a malyamungu kwa kutetea haki yao ya kikatiba, hawakuenda bure. Damu yao imekuwa chachu iliyoziwasha nia na ari mpya ya sisi wananchi kudai haki zetu za msingi na fursa ya kuthaminiwa ubinadamu wetu katika taifa letu wenyewe. Hatutalala wala sasa hatutapumzika na tutatumia fursa yoyote itakayopatikana hata tumehakikisha huyu kaburu mweusi ndani ya nchi yetu anatokomezwa. Ni heri sisi sote tufe maana huo utayayari tumekwisha kuuva sasa, ili watoto wetu na kizazi kijacho kiwe salama.
Wana mageuzi wa kweli naomba sasa maneno yetu yawe mafupi bali matendo yetu ndiyo yazungumze zaidi.
.
EEH MUNGU ZILAZE ROHO ZA WAHANGA HAWA MAHALA PEMA PEPONI. NA WALE WOTE WALIOHUSIKA NA VIFO HIVI WATIWE ALAMA ILI WAWE WAZI KWA MALIPIZO, WASIACHWE WASHUKE KUZIMUNI KWA AMANI MAANA HAWAKUITAKA HIYO AMANI!
.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.