Nimeishi sana arusha na huku ndiko makao makuu yao na wana Projects nyingi sana wenyewe wanaziita ADP's cha ajabu kila ADP ofisini wote ni wachaga! Nilishtuka kidogo lakini nikapotezea nikajipa moyo labda 'mcheza kwao utunzwa' (wachaga>>arusha) baadae nikahamia tanga nako wana ADP nyingi sana wilaya tofauti tofauti nako pia hali ni ileile kila ofisi ya ADP unayoenda wachaga wamejaa!!! Ikaniuma kiduchu nikajipa moyo labda kwasababu tuko nao karibu (tanga na arusha).. sasa last week nimekuja Morogoro nikaenda pale ofisi yao kuu ya mkoa (MOROGORO CLUSTER OFISI) nikakuta ofisi wachaga 90%!!! Kesho yake nikaenda kwenye moja ya projects zao inaitwa MLALI ADP iko ndani ndani kabisa vijijini huko nako project manager mchaga, project accountant mchaga, zagazaga nyingine nao 80% wachaga!! Nikafadhaika sana ikabidi nimuulize swali mmoja ni Staff wa hapo mlali adp (sio mchaga) akanijibu kuwa hata yeye aelewi ila hali ni hiyo hiyo karibia tanzania nzima, yeye binafsi kabla ya kuja mlali alikuwa ofisi ya kigoma nako hali ni hiyo hiyo, wachaga wachaga wachaga!!!! Nikachoka..
------------------------
UPDATE
Sina shida yeyote na World Vision kuajiri wakrist kwasababu wao ni shirika la kikrust na hiyo ni policy yao na katika kusajiliwa imesajiliwa hivyo! Siko hapa kuongelea DINI.. Wapo wanaosema naendekeza ukabila kwa kuzungumzia wachaga, lakini mimi naamini kuwa kama kuna mahali tunakosea ni vizuri kusahihishana, na wanachofanya hawa wenzetu wa World Vision si sahihi hata kidogo...
Binafsi sinawahi kuomba kazi World Vision wala sijawahi kufikiria hilo lakini nimefanya nao kazi mara nyingi sana nikiwa kama consultant (kama ambavyo nafanya kazi na mashirika mengine mengi). Kwa mfano; mwaka 2006 nilishiriki kufanya evaluation ya mradi wa Mlali ADP na kuandika proposal ya kuomba extension ya miaka mitano ya mradi (mradi ulikuwa unatakiwa kuphase out mwaka huo) na 'wazungu' wakawapa extension! Mwaka 2008 nilihusika tena kuandaa proposal ya kuomba extension ya pili ya miaka mitatu na 'wazungu' walikubali.. ieleweke kuwa huu ndio mradi pekee toka kuanzishwa kwa World Vision Tanzania ambao ulifanikiwa kupata extension mara mbili.. mpaka leo hii watu wanashangaa tulifanya 'mazingaombwe' gani mpaka wale 'wazungu' wakakubali.. hivyo naomba ieleweke naifahamu vilivyo World vision na najua ninachokiongea..
Nirudi kwenye mada, kuna watu hapa wanadai kuwa shirika limejaa wachaga kwasababu wao ati wamesoma sana, huo ni UONGO wa hali ya juu.. nitaeleza.. katika shirika la world vision majority wa staff wake ni jamaa wanaitwa CRS (mwaka 2012 walibadilishwa jina na kuitwa DA, na kuanzia Oct 1, 2013 wameanza kuitwa SPF) hawa jamaa (CRS/DA) kabla ya octoba mwaka jana karibia wote walikuwa ni form VI leavers!!! Walikuwepo mmoja mmoja wa kuokoteza ndio walikuwa form six, na wengine wana certificate!! Waratibu wa miradi na baadhi ya PF ( project facilitator) ndio walikuwa na shahada! Lakini DA's/CRS karibia wote hawakuwa hata na diploma (hapa tunaongelea zaidi ya wafanyakazi 1500 tanzania nzima)! Ni mwaka jana tu hapa octoba ndio wamebadilisha hiyo tittle na kuiita SPF (sponsorship and project facilitator) na wakaweka sharti muombaji awe na angalau diploma! Lakini miaka yote hawa jamaa walikuwa ni form VI leavers tena wale waliokosa nafasi za kwenda advanced level!! Sasa ninyi wenzetu mnaopiga kelele kuwa wachaga ni wasomi ndio maana wamejaa World Vision, mnataka kutuambia kuwa hakuna WALUGURU waliomaliza form VI mpaka mchukue form VI wa arusha muwapeleke Morogoro, inamaana hakuna WAHA Waliomaliza form 4 mpaka mpeleke wachaga kigoma, hakuna wazigua wenye form 4 pale korogwe na lushoto na korogwe????
Cha kushangaza zaidi kuna ADP moja pale Morogoro cluster office, ambapo wameajiri Office attendant (mfagiaji) mchaga kutoka arusha huyu dada anaitwa Matilda! Inamaana waluguru na wapogoro hawajui kufagia!!! Unaweza kusema hii ni coincidence?????