WORLD VISION ni shirika la wachaga??

WORLD VISION ni shirika la wachaga??

Status
Not open for further replies.
Utamu wa tra unaujua au unausikia mkuu,hasa uwe kamishna,kila rushwa inayopigwa ya maana una sehem yako,mkakati wa kitilya kubaki pale ulikua mzito,bahati mbaya tu kwake aliyekua kampa uhakika alifariki.

Kufanya kaz gvt kuna utamu wake hasa ukiwa bosi,jiulize kwa nini watoto wa vigogo wasiendeleze miradi ya wazee wao lakin wanataka kaz serikalini,sehem nyeti!wanajua raha yake.

Sure mkuu, si TRA tu bali hata katika taasisi nyingine za serikali hawa watu wanakuwa kunguni kabisa waking'ang'ania tu. Cha kusikitisha ni hao watoto wao wamefeli shule za nje wakirudi tu vimemo vinawapa kazi katika taasisi hizi za serikali. No wonder ndiyo maana they are non-performing institutions!!!! Brain zinaajiriwa Private!!!! Si tunaona jinsi gani vijana wadogo with brains wana shine huko private?? Wanafanya mambo makubwa sana!!!! Sub-standards nyingi za vibosile huko serikalini!!! Ni wachache wao with brain ila kwa culture hazisikilizwi!!!! Kwanza junior hawezi shauri boss, tehe tehe!!!
 
Mi umeniacha kuzungumza kuwa ni form vi waliokosa nafasi za advance!
 
sikatai kuwa kuna weza kuwa na kaupendeleo. lakini niweke wazi maeneo mengi tz yanatofautiana itikadi. moja ya itikadi ya wenzetu huko moshi ni kusomesha watoto.

kuna familia nyingi unakuta kipaumbele ni mme kuowa na mke kudai talaka na watoto kulelewa bila muelekeo. sisemi kuwa hawawezi toka wasomi lakini mazingira sio user friend. mbona wahaya ndio wanaongoza kufundisha vyuoni hujasema?

Wewe nawe ni mchaga without doubt. Elewa mada jomba. Unamaanisha nyie wachaga ndio smart ktk malezi kuliko kabila zote tz. Hilo la vyuo si kweli ni mchanganyiko huwezi fananisha mantiki yake na hii mada. Pyuuuu!.
 
Ungechunguza endapo wana sifa za kazi wanazofanya na utaratibu wa kupata ajira,kamq vigezo na masharti vimezingatiwa na.watu wanasifa zonazotakiwa.

Hilo ndilo suala la msingi. Uzuri amesema yeye mwenyewe hajawahi kuomba kazi huko. Watu wengine kazi ya kulalamika lakini hawaingii kupigania fulsa zinapopatikana. Wachagga ni daring people au unaweza kusema ni risk takers ndio maana wapo kila mahali. Lakini wenzetu wale kutokana na uhaba wa aridhi kule kwao waliwekeza sana upande wa elimu kama aridhi mbadala kwa watoto wao ndio maana wametawanyika kila mahali. Mkoa wa kilimanjaro ndio unaongoza kwa kuwa na shule nyingi za sekondari kama sikosei. Aidha walilitumia vema zao la kahawa kusomesha watoto wao wakati likiwa na bei hivyo wale waliosoma nao wanawasomesha wadogo zao au watoto wao. Wachagga hawatofautiani sana na wahaya kwa kujali elimu. Ndio maana utawakuta sana wahaya na wachagga kwenye ofisi za kitaaluma sana kama benki, TRA, vyuo vikuu kama wahadhiri, bandari, mashirika ya nje kama hilo World Vision nk. Hebu tujiulize, ulitegemea uwakute wamasai, au wazaramo na wakwere wengi hapo??!!
 
Nadhani mtoa mada ni BOLD kama anavyojiita mwenyewe. Kwa kazi anayoifanya nilitegemea awe na weledi wa hali ya juu ya kuweza kuchambua mbichi na mbivu. Consultant anaeweza kupata tender world vision na asie na uelewa kama mheshimiwa BOLD ni hatari kwa taifa la nchi.

Kuongelea ukabila kwa Tanzania ni uchochezi usiokuwa na maana.Tumesoma na hao wachagga hadi vyuo vikuu...nashindwa kuelewa kama PWC, KPMG, n.k nao wana ukabila maana vigezo vyao ni GPA na hao wachagga ndio asilimia kubwa wananyakuliwa tukiwa bado vyuoni.Inanilazimu kuamini kuwa kuna jitihadi za ziada zinatumika kupata nafasi mahali fulani kuliko kutumia kigezo cha ukabila.
 
Hilo ndilo suala la msingi. Uzuri amesema yeye mwenyewe hajawahi kuomba kazi huko. Watu wengine kazi ya kulalamika lakini hawaingii kupigania fulsa zinapopatikana

Mkuu, kwanza nina mashaka kama umesoma bandiko langu lote! Kwa kukusaidia tu kuelewa ni kwamba siwezi kuomba kazi WVT kwasababu sina sababu ya kufanya hivyo, I have my own consultancy firm! Hivyo siwezi kuacha kazi katika kampuni yangu mwenyewe nikaombe kazi ya DA hapo WVT yenyemshahara wa 360,000/=!!! huo utakuwa ni WENDAWAZIMU.! Fursa niliyonayo binafsi naiona ni kubwa kuliko hiyo iliyopo WVT! Ninachojaribu kuhoji hapa kwann WVT inaajiri hasa hasa watanzania wa kabila fulani pekee..
 
Wachagga ni daring people au unaweza kusema ni risk takers


Inawezekana wachaga ni daring people lakini ni ukweli usiopingika kuwa ndani ya WVT wanapendelewa!! Nimeeleza kuwa kwa miaka mingi tu WVT wamekuwa wakiajili katika kitengo cha DA watu waliomaliza form VI .!! Wote tunafahamu jinsi form VI walivyojaa huku mitaani, lakini still DA wa WVT walikuwa wamejaa wachaga!! Huu u'daring' wao uko wapi? Binafsi sioni 'u-daring'wowote kwa wao kujaa WVT!!!
 
wacha kuleta maswala ya ukabila hapa kinachotakiwa ni hawaharibu kazi cha msingi ss sote watanzania bana
 
wacha kuleta maswala ya ukabila hapa kinachotakiwa ni hawaharibu kazi cha msingi ss sote watanzania bana

Tehe tehe tehe!! Ati hawaharibu kazi!!! Subiri nitaleta hapa bandiko kuelezea hali ya kiuchumi na kiutendaji ilivyo kwa sasa WVT!! Utashangaa mpaka utazirai... ni viroja
 
hili ni shirika la kikristo lililoanzishwa na Mchungaji kwa ajili yakusaidia jamii. Policy yao iko wazi kuhusu ajira lazima uwe committed Christian ( sio mkristo mlevi, muhuni, mwizi na sifa zake zinajulikana) kwani uuliza pia reference toka kwa . mchungaji wako au kiongozi wako wako wa kanisa. maswali ya kibiblia ni ili kupima ukristo wako kwa sehemu.
kwa sehemu niliwahi kuwafahamu staff wa WVision hapa Dar. mabos walikuwa 1. mhaya 2. mnyakyusa 3. mhaya4. sukuma na mmeru. hao wachaga unaosema sijui umetoa wapi umbeya huu.
ushauri wangu kwa mtu kama wewe..... tafuta urafiki na waliofanikiwa katika sector tofauti za maisha utajifuna kitu na sio kutafuta visa na maneno mbofu mbofu.
 
Ebu endeleza utafiti wako kwy mashirika na tahasisi za umma huko ndy unaweza pata attention,maana world vision ile ni just NGO tu.
 
tatizo la ukabila limekuwa kubwa katika kila idara na sekta muhimu hapa nchini, taratibu tunaharibu nchi yetu
 
Mimi nimeanza kuijua World vision muda mrefu na walikuwa na miradi mingi sana mkoa wa Kagera na most of people na wengine nikiwa nawajua walikuwa ni Wahaya na Wanyambo na sikuwahi kuona Mchagga hata mmoja, kadri illivyoendelea nimeshuudia watu wengi wakiwemo marafiki zangu wakiwa wameajiliwa na hiyo World Vision na wote ninaowajua na wana nafasi kubwa si Wachagga. ni Mchanganyiko wa makabila ila Wakristo. Kwa hiyo ili uweze kuajiliwa lazima uwe Mkristo na hiyo siyo hoja maana waanzilishi wameweka sharti ilo. Kwa hiyo hoja ya kusema World Vision ni ya Wachagga kwa kweli inanipa ugumu kuamini. Mimi mwenyewe hapa siyo Mchagga kusema kwamba nawatetea bali naongelea kile ninachojua kuhusu World Vison

Huna tofauti na yule mnyama anaezaa na kula watoto nimesahau jina lake
 
Na huyu mtu anatuambia na anataka kutwambia kwamba ni consultant. Kama kweli u-consultant uko hivyo nadhani kuna kasoro mahali. Maana kama kweli alitaka kufanya analysis ya kweli angeangalia sehemu nyingi za kazi na kutwambia Waruguru wako wangapi kila taasisi kulinganisha na Wachagga, Wahaya, Wanyakyusa na Wanyasa, kisa aende vyuo vikuu aangalie rate ya wanafunzi je wengi wanatoka katika makabila gani, na je kweli Waruguru, Wasambaa, wanashindana na makabila niliyotaja. Tuje hata walimu wa vyuo hivyo je ni Wasambaa, Wazigua, Wabondei na Wadigo, Wangulu, Wakagulu, Wasagala, Wapogolo, Wandamba wangapi katika vyuo hivyo. Watu wenyewe wa mikoa hiyo anayotaja wamekalia kupiga ngoma na kumtoa mwali shule saa ngapi ili wafanye kazi World vision? Penye ukweli lazima usemwe haya makabila ya Tanga na Morogoro si wote wana uwezo wa kufanya kazi world vision maana shule hawaendi.

Nadhani mtoa mada ni BOLD kama anavyojiita mwenyewe. Kwa kazi anayoifanya nilitegemea awe na weledi wa hali ya juu ya kuweza kuchambua mbichi na mbivu. Consultant anaeweza kupata tender world vision na asie na uelewa kama mheshimiwa BOLD ni hatari kwa taifa la nchi.

Kuongelea ukabila kwa Tanzania ni uchochezi usiokuwa na maana.Tumesoma na hao wachagga hadi vyuo vikuu...nashindwa kuelewa kama PWC, KPMG, n.k nao wana ukabila maana vigezo vyao ni GPA na hao wachagga ndio asilimia kubwa wananyakuliwa tukiwa bado vyuoni.Inanilazimu kuamini kuwa kuna jitihadi za ziada zinatumika kupata nafasi mahali fulani kuliko kutumia kigezo cha ukabila.
 
hili ni shirika la kikristo lililoanzishwa na Mchungaji kwa ajili yakusaidia jamii. Policy yao iko wazi kuhusu ajira lazima uwe committed Christian ( sio mkristo mlevi, muhuni, mwizi na sifa zake zinajulikana) kwani uuliza pia reference toka kwa . mchungaji wako au kiongozi wako wako wa kanisa. maswali ya kibiblia ni ili kupima ukristo wako kwa sehemu.
kwa sehemu niliwahi kuwafahamu staff wa WVision hapa Dar. mabos walikuwa 1. mhaya 2. mnyakyusa 3. mhaya4. sukuma na mmeru. hao wachaga unaosema sijui umetoa wapi umbeya huu.
ushauri wangu kwa mtu kama wewe..... tafuta urafiki na waliofanikiwa katika sector tofauti za maisha utajifuna kitu na sio kutafuta visa na maneno mbofu mbofu.

Hiyo unayoongelea ni ofisi moja pekee (only one ADP) Tanzania nzima ziko kama 67 hii!!
Halafu haya ni maoni yangu, kama unatofautiana na maoni yangu hiyo haina shida lakini hakuna haja ya kejeli na matusi!! TUHESHIMIANE HATA KAMA TUNATOFAUTIANA..
 
we consaltant ulishaomba kazi woldvision ukaulizwa kabila lako kwenye interview? kama una uhakika na ulichoandika ulichukua hatua yeyote ya kuwashauri maana umesema ulishafanya nao kazi tena ikakubalika? inaonyesha ulikuwa mwajiriwa huko ukafukuzwa kwa makosa yako mwenyewe au kiwango chako cha elimu unachotoa hapa ni hasira zako tu wala sio uchaga. kasome bwana uje uombe tena kazi acha hasira Mungu hapendi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom