World Cup 2010 SA: Match updates (From June 11)

World Cup 2010 SA: Match updates (From June 11)

Yaani Karai la Ekoto leo limetoboka kabisa.................
 
nilisemaga hapa huyu jamaa wanampa ukumbi sana. keshatunyonga sasa. heheheheh kesho alfajiri naenda kuuza TV.
 
Safi sana sana. Walau timu za Africa sasa zote zinaisha na nitabaki bila timu. Hongera sana Denmark.

Yaani mtu hapa na hapa anakosa. Hii mijinga haina shabaha si kawaida.

Ila Ghana kwa kweli wamevunja rekodi, khaaaa...
 
Aibu kweli jamani. Yaani pamoja na kupata nafasi nyingi za wazi Cameroon itakuwa timu ya kwanza kuaga haya mashindani!!
 
Mwakilishi mwingine wa Afrika yupo uwanjani, je tutegemee nini?

Watakuwa timu ya kwanza ya Afrika kuaga leo??
The Answer is YES naona kuna haja ya FIFA kupunguza nafasi za ushiriki kwa AFRICA kwenye WC bora iwe inakwenda timu moja au Mbili!! mambo gani haya kupeana presha usiku huu mpaka wine inagoma kuingia kwenye koho! aaagr
 
kwa wale wenye matatizo ya headache, bp na mengineyo nawashauri mkapumzike maana hapa naona mambo hayaendi vizuri
 
Ivory coast naye atacheza kwenye mdomo wa Brazil, sijui kama kuna kupona hapo...
 
Kuanzia leo sirudiii kushabikia timu za africa zote ni kichwa na mwendawazimu zinatupa presha za bure huo ndo msimamo wangu....
 
huyu idrisou urefu wa bure.......anakosa free headers....
 
Cameroon wametoka KIUME leo. Hongera kwa walau mechi nzuri sana.
 
hahaaaa! mkuu, na hatuwezi kuwa Asia, Europe au Amerika, tujipende tulivyo, kwanza hii fani tumevamia tu, sie waaafria fani yetu ni kucheza na ng'ombe, mbuzi kukimbiza kuku huku umevaa gunia na kuvutana na kamba

hahahha umenivunja mbavu.....
 
kitu kinachonifanya nifurahie hii 2010 WC ni kimoja tu, lile timu ambalo nalichukia kuliko yote duniani nalo pia linaboronga (ENGLAND). msijali washirika kesho tunamfanyia BRAZIL kiulaini kabisa.
 
Back
Top Bottom