Wito wa serikali kuzitaka Taasisi za fedha kushusha viwango vya riba upewe mkazo

Mwadilifu Mdhulumiwa

JF-Expert Member
Jul 22, 2021
418
630
Salam ndugu wana JF!

Moja kwa moja kwenye maada, ndugu zangu kwa muda mrefu kumekuwapo na wito na maagizo mengi ya serikali kuzitaka taasisi za fedha kushusha riba wanazotoza katika mikopo wanayotoa kwa wanananchi.

Kila linapojitokeza tukio linalomkutanisha ama Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu au Waziri wa fedha katika hotuba wanazotoa ni lazima tu moja ya mambo huwa ni kuzungumzia kuzitaka taasisi hizo za fedha kushusha riba zao za mikopo ili kuleta nafuu kwa wanaoomba mikopo hiyo.

Hata hivyo utekelezaji wake umekuwa ni wa kusuasua sana kwani mpaka sasa bado viwango vya riba za mikopo kwenye taasisi zote za fedha viko juu sana!

Hivyo wananchi tunajiuliza je nini sababu ya taasisi hizi kupuuzia au kukaidi wito unaotolewa kwao na serikali? Serikali ndiyo inayosajili na kutoa vibali na leseni za biashara hizo, Je inashindwa wapi kuweka viwango vya riba elekezi kwa mabenki yote?

Wananchi tunaitaka serikali ikazie na kufanya ufuatiliaji wa wito na maagizo inayoyatoa kwenye taasisi za fedha ikiwa ni pamoja na kuzitaka benki kupunguza masharti na vikwazo wanavyoweka katika utoaji wa mikopo hiyo. Mathalani inafahamika vijana wengi hawana hata viwanja vya kujenga nyumba , ajabu kijana akienda benki kuomba mkopo mdogo tu wa milioni 2.5, anaambiwa mpaka uwe na hati ya nyumba.

Tunaiomba serikali iwe serious na suala hili, kwani vijana wengi wamejiajiri kupitia shughuli binafsi, Hivyo ni wajibu wa serikali kutanua na kuboresha mazingira ya uwezeshaji kiuchumi.
 
Unapigwa danganya toto nawe unakubali. Kama wangekuwa na nie wasingekuwa wanato matamko bali wangetunga sheria.
 
Salam ndugu wana JF!

Moja kwa moja kwenye maada, ndugu zangu kwa muda mrefu kumekuwapo na wito na maagizo mengi ya serikali kuzitaka taasisi za fedha kushusha riba wanazotoza katika mikopo wanayotoa kwa wanananchi.

Kila linapojitokeza tukio linalomkutanisha ama Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu au Waziri wa fedha katika hotuba wanazotoa ni lazima tu moja ya mambo huwa ni kuzungumzia kuzitaka taasisi hizo za fedha kushusha riba zao za mikopo ili kuleta nafuu kwa wanaoomba mikopo hiyo.

Hata hivyo utekelezaji wake umekuwa ni wa kusuasua sana kwani mpaka sasa bado viwango vya riba za mikopo kwenye taasisi zote za fedha viko juu sana!

Hivyo wananchi tunajiuliza je nini sababu ya taasisi hizi kupuuzia au kukaidi wito unaotolewa kwao na serikali? Serikali ndiyo inayosajili na kutoa vibali na leseni za biashara hizo, Je inashindwa wapi kuweka viwango vya riba elekezi kwa mabenki yote?

Wananchi tunaitaka serikali ikazie na kufanya ufuatiliaji wa wito na maagizo inayoyatoa kwenye taasisi za fedha ikiwa ni pamoja na kuzitaka benki kupunguza masharti na vikwazo wanavyoweka katika utoaji wa mikopo hiyo. Mathalani inafahamika vijana wengi hawana hata viwanja vya kujenga nyumba , ajabu kijana akienda benki kuomba mkopo mdogo tu wa milioni 2.5, anaambiwa mpaka uwe na hati ya nyumba.

Tunaiomba serikali iwe serious na suala hili, kwani vijana wengi wamejiajiri kupitia shughuli binafsi, Hivyo ni wajibu wa serikali kutanua na kuboresha mazingira ya uwezeshaji kiuchumi.
Kama unamtumia mzazi wako hela kidogo akanunue Panadol, serikali inaipiga tozo,wakishusha riba it means na commission yao si itapungua ??!
 
Salam ndugu wana JF!

Moja kwa moja kwenye maada, ndugu zangu kwa muda mrefu kumekuwapo na wito na maagizo mengi ya serikali kuzitaka taasisi za fedha kushusha riba wanazotoza katika mikopo wanayotoa kwa wanananchi.

Kila linapojitokeza tukio linalomkutanisha ama Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu au Waziri wa fedha katika hotuba wanazotoa ni lazima tu moja ya mambo huwa ni kuzungumzia kuzitaka taasisi hizo za fedha kushusha riba zao za mikopo ili kuleta nafuu kwa wanaoomba mikopo hiyo.

Hata hivyo utekelezaji wake umekuwa ni wa kusuasua sana kwani mpaka sasa bado viwango vya riba za mikopo kwenye taasisi zote za fedha viko juu sana!

Hivyo wananchi tunajiuliza je nini sababu ya taasisi hizi kupuuzia au kukaidi wito unaotolewa kwao na serikali? Serikali ndiyo inayosajili na kutoa vibali na leseni za biashara hizo, Je inashindwa wapi kuweka viwango vya riba elekezi kwa mabenki yote?

Wananchi tunaitaka serikali ikazie na kufanya ufuatiliaji wa wito na maagizo inayoyatoa kwenye taasisi za fedha ikiwa ni pamoja na kuzitaka benki kupunguza masharti na vikwazo wanavyoweka katika utoaji wa mikopo hiyo. Mathalani inafahamika vijana wengi hawana hata viwanja vya kujenga nyumba , ajabu kijana akienda benki kuomba mkopo mdogo tu wa milioni 2.5, anaambiwa mpaka uwe na hati ya nyumba.

Tunaiomba serikali iwe serious na suala hili, kwani vijana wengi wamejiajiri kupitia shughuli binafsi, Hivyo ni wajibu wa serikali kutanua na kuboresha mazingira ya uwezeshaji kiuchumi.
Huu wito uendane na vitendo kutoka kwa watunga sera. Ili kuchochea ukuaji wa uchumi na shughuli za sekta binafsi, lazima mabank yafanye kazi zaidi na wajasiriamali wengine wote. Kwasasa mazingira sio rafiki sana kwetu.
 
Mabenki Hayaweki wazi riba zao,
Wanajinadi kuwa riba ni kuanzia 13% Hadi 16% na bima ya mkopo 1%

Ukifatilia Kwa undani riba ni 17%
 
Back
Top Bottom