William Malecela: Dissaster waiting to happen

William Malecela: Dissaster waiting to happen

Nafikiri watu wengi pamoja na hata mleta mada wamechanganya mambo. Sidhani kama suala hasa hapa ni Jumuiya ya Afrika Mashariki. Suala hapa ni kama kweli tunapekeka watu makini kutuwakilisha huko. Inawezekana aliyosema William ni ya kweli kabisa lakini mbona wanasiasa wetu wakati wa kampeni huwa wanafanya hivyo hivyo kwa kutuondhoreshea list ya matatizo yetu na jinsi watakavyoyatafutia ufumbuzi lakini wakishachangualiwa hawafanya chochote?

Wakati babake alivyopigwa chini na Lusinde watu hapa walishangilia weee, kumbe Lusinde mwenyewe mliokuwa mnamshangilia ndiye huyo. Leo mnapewa maneno matamu na William tayari kwishaney. Ukitaka kuwapiga bao Watanzania ongea tuu kile wanachotaka kusikia. Hata kama ukiwa kichaa watakuchagua tuu uwawakilishe. Muone hata Lusinde kadhibitisha yeye ni kichaa wa kuzaliwa lakini still walimchagua kuwa mbunge wao.

Hatuna tabia ya kwenda deep na ku-examine hawa watu kama kweli wana credentials zinazotakiwa kutuwakilisha hasa kwenye ngazi za kimataifa where the national interests are at stake. Kwa kweli inabidi ifike mahali tujiulize: Are we picking the right people to represent and defend our interests in the East African Community na kwingine kote duniani? Je, process nzima inayotumika kuwapata hawa wawakilishi ni fair na open kwa watu wote? Au watu wanapitishwa kwa kujuana tuu? Imefika wakati tuache kudanganywa na maneno ya watu wanaodai kuwa wanataka kutuwakilisha wakati wanataka tuu uongozi kwa faida zao binafsi.

Kama kweli kuna mtu aliyesikiliza interview ya William kuanzia mwanzo mpaka mwisho na ku-conclude kwamba anafaa kabisa kutuwakilisha EAC then we have got a long way to go. Seriously, utakuwa huna tofauti na yeye kusema kuwa tuna gap ya miaka 250 kufikia demokrasia ya Marekani. Kama ndivyo unavyotaka then muunge mkono lakini usilalamike kuhusu demokrasia mbaya Tanzania kwa muda wa miaka 250 kama bado utakuwa hai.

EMT, mimi sina cha kuongeza!!!!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
- Mkuu mleta Mada heshima mbele sana, bado nina uchovu sana maana jana tumemaliza kuhesabu kura usiku sana na kampeni kwa ujumla ilikuwa ni an-experience, kwa hiyo nitarudi tena later!

William.
 
william Malecela wengi tunakufahamu tu kupitia jamiiforums lakini watanzania wengi hawajakusikia ungeanza na kujitangaza mapema kama ulikuwa na nia ya dhati ya kuingia kwenye siasa.

Kutumia short cut kwenye siasa unaweza kuwa unajitenegenezea ajali mbaya ya kisiasa.

Kumbuka SIYOI SUMARI alipokufa tu baba yake ndipo akataka siasa na wewe mzee wetu John Malecela alipoanguka tu jimboni kwake umechomoza kwenye siasa.

Hata kama nia yako ni njema umekosea mahesabu ili uweze kukubalika na watanzania wengi ndio maana wengine wanafikiri unatumia jina la baba kama ngao ya kufika juu kwa sababu umeruka baadhi ya ngazi muhimu kwenda juu
Kwakuwa Wiliamu Malecela ni mtanzania na amezaliwa Tanzania, anahaki ya kushiriki siasa za Tanzania bila kuwekewa mipaka. Acheni kujifanya ninyi ndio wenye haki kuliko watu wengine, eboo!!!
 
Nakubaliana na hoja ya kujiunga na federation kuwa slow, ila kuna vitu ameongea eti watanzania wengi waliopo nje wanaikosoa serikali kwasababu ni CDM huu ni uongo uliopitiliza, naimani kuwa hata ukiwa ccm unaweza kuikosoa serikali inapokosea.
 
- Mkuu mleta Mada heshima mbele sana, bado nina uchovu sana maana jana tumemaliza kuhesabu kura usiku sana na kampeni kwa ujumla ilikuwa ni an-experience, kwa hiyo nitarudi tena later!

William.

Mnafuta baadhi ya michango yetu, hasa yenye ukweli dhahiri, Baharia utafeli haraka sana kwenye siasa, utafelishwa na stail ya anna killango kukinusuru ccm jambo ambalo limeonekana kwako pia. sikutarajia uisifie serikali ya ccm mpaka inavyogawa madini yetu!!! kwa jinsi hii kenya wataendelea kutambulika kuwa ndiyo wenye tanzanite nyie mko bize kukinusuru chama kilichooza mwili mzima. Mawaziri ambao ni zao la ccm wanagawa ardhi kwa wageni, wewe unasifu hilo!!!! huko ndiko kutekeleza matakwa ya watanzaniaaaaaa? badilika kutoka sauli uwe paulo i.e ccm to cdm. hakuna porojo katika hili.
 
Nakubaliana na hoja ya kujiunga na federation kuwa slow, ila kuna vitu ameongea eti watanzania wengi waliopo nje wanaikosoa serikali kwasababu ni CDM huu ni uongo uliopitiliza, naimani kuwa hata ukiwa ccm unaweza kuikosoa serikali inapokosea.

Ameshaanza kutekeleza maagizo ya nec ccm, kuishambulia cdm kwa failier za ccm, hajui anajimaliza ki-sioi sioi.
 
baharia itabidi ubadili style uwaonyeshe watu kuwa you are not thinking kama wao

Nakumbuka January alipoingia kwenye scene alisema kuwa ana ajanda 12345 na kusema ukweli japo yuko ndani lakini alisema wazi kuwa kuna mambo lazima yabadilike na hakuniogopesha hata kidogo

Unless ulifanya ile interview ukiwa umechoka asubuhi lakini i expected more
 
Wewe ndiye mjinga!
Angalia nchi kama Danmark, Norway. Hazipo kwenye european union na uchumi wake ni makini. Ficha ujinga wako usije ukaropoka na kujaji bila kuelewa duniani kuna nini. Nadhani wewe ndiye upo nyuma sana ki dunia. Huwezi ukazamisha uchumi wa Tz East Afrika na ukategemea tutaibuka. Ni muhimu tujijenge kwanza sisi ndiyo tufikirie kujiunga. Kwa taarifa yao asilimia 99.9999 ya vijana hawataki East africa federation kwani sasa ajila ni shida na hapo bado. Ardhi sasa hivi inamendewa na wageni, na vijana wa tanzania bado wengi ni maskini na wengi ndiyo tumetoka shule sasa huo ushindani tutauweza??

Statistics zako ni za uongo. Nani alikuambia Denmark na Norway si wanachama wa EU? Kwani kutotumia euro ndio kunawafanya wasiwe EU members?

Utafiti upi uliofanyika na ukathibitisha hiyo percentage yako?
 
ilipofika dakika ya 20 ya hiyo interview nikasema huyu sio william niinayemjua mimi

no way!
 
Mhh! Kiöngozi, mtoa mada sijui niseme una chuki binafsi na ze baharia w.melecela au unauelewa mdogo wa mambo ya e.a, au umekurupuka au ulitaka tu kujaza server. Sitegemei kama kuna kijana anayependa tanzania ifanye haraka kujiunga east afr. Vijana hawana ajira, ardhi taabu, elimu badala ya kuongezeka ubora, inapungua. Ukiwekwa na mkenya kwenye interview anakushinda. Kaa tulia, alfu njoo tena

nakushauri usikilize tena hiyo interview
 
SHAROBARO ! hivi hakuna picha nyingine nzuri zaidi ya hii? mbona inamuondoa personality kabisa, mie namuona kama sharobalo !
 
Nina imani ya kwamba wengi wetu ni vijana tunaofikilia maendeleo ya nchi yetu, ni vema sana.EAC kwa watanzania bado tuna wimbi la uwoga labda kuhofia wenzetu hasa vijana wa nchi jilani ya kenya kuchukua fursa zetukama ajila,ardhi na fursa za kibiashara.kwanini vijana wa kitanzania tunaogopa?je hatuna elimu ya kutosha? hatuna biashara ya kushindana na wenzetu?fursa gani zinatushinda?Tanzania ni nchi ya wasomi na wataalamu wakila aina,inatia shaka kuona tunakuwa na wasiwasi na hili shilikisho.

maoni yangu mimi kama kijana tuangalie fursa zilizopo hapa sasa na kwa wenzetu je mimi kama kijana wa kitanzania nipeleke bidhaa gani nchini kenya?na niingize tanzania bidhaa gani ambayo tanzania haipo ila ipo kenya na watanzania wanahitaji?
pia katika elimu zetu wengi wetu tuna profesional au utalamu katika fani moja tu kwa mfano ikiwa wewe umesoma IT basi ndo hiyo hiyo unaangaika nayo kutafuta kazi,na aliesomea utawala basi ndo hiyo hiyo tu jamani tutashindana vipi hapa?angalia hao wenzetu tunao waogopa wana fani mbali mbali wamesomea unamkuta mtu ana labda tu diploma ya IT huyo huyo ana diploma ya ugavi,anakuja kuwa tena na shahada ya utawala mtu mmoja,.
mwingine anakuwa na shahada mbili ya fani tofauti.sasa tujiulize vijana wenzangu nani anafani mbili tu tofauti?hapa kwetu mtu akisoma sheria basi yeye ni mahakamani tu hili shilikisho kwa mtindo huu litatushinda.
my advice,vijana tuangalie fursa wanazotumia wenzetu kwa umakini zaidi,,,,,kila la kheri W.MALECELA
 
316444_2385989848381_1209820481_32959751_2885080_n.jpg

Nimesikiliza interview yake aliyoifanya ambayo imepostiwa michuzi blog. Inaonekana huyu yuko out of touch na maendeleo ya dunia

Hoja zake kubwa ni hizi:

4. William anasema kuwa angefurahi sana kama National Service ikarudishwa ili kurejesha uzaelndo kwa vijana lakini ukweli kasahau:

a) Kwa nini iliondolewa in the first place

b) Uzalendo hauwezi kupatikana kwa kulazimishana

c) Atapata wapi budget ya kuirudisha hiyo National service


d) Uzalendo haupatikani kama serikali haitazami wananchi wake

6. Amesema kuwa Tanzania middle class wamekuwa wengi....well ukweli ni kuwa tanzania ina population ya almost 44 million na the so called middle class ni less than 8% sasa na ni wale wale ambao ni watoto wa kishua na extension zao. Namshauri williama atoke aende rufiji, Mkuranga Kisarawe na tendahimba kama atakuta middle class hata mmoja.

9. William anasema kuwa achievements zake kubwa ilikuwa ni kuandaa sherehe ya kumpokea Asha Migiro alipoteuliwa kuwa Dpeuty SG wa Ban Ki Moon, mimi binafsi sioni kama hiyo ni issue na sioni kama ni achievement ya maana.

William kama mawazo yako ni hayo then I give up!
hawa watu wa dizaini hizi hawawezi kutusaidia chochote zaidi ya kutafuta recognation kutoka kwa watu tuliojichokea.

Chukulia mfano mzuri wa Bwana Sioi na ubunge wa Arumeru, anakwenda kuomba ubunge sehemu asiyoishi na wala hajajiandikisha kupiga kura pale, kisa eti ndio natokea hapo. Unadhani angeliupata watu wa Arumeru Mashariki wangemuona hapo!?

Sio mambo ya ushabiki bali Joshua Nassari katoa wazo zuri kuwa 'masikini wanachagua masikini mwenzao". Nakuwa na mashaka nikiangalia list ya wanaowania huu uwakilishi/ubunge wa EAC kama kuna yeyote mwenye upeo na nia ya kinachotakiwa kule.
Ndio maana Wakenya wanatudharau!

 
Mimi nakushauri ujiandae kurudi mtera jimbo liko wazi yuko mtu anapashapasha kiti pale lakini ameharibu sana hadi kwa majirani kwa matusi yanayoumbua utu wa watanzania.hivi ulikuwa wapi kumashauri babako akuachie jimbo badala yake wananchi wamemuachagua kilaza huyu ambaye memory yake inatemamatusi bila mpangilio. Infact mtera ni kama mwanamkiwa kwa sasa na jk analicheki jimbo kiaina hasemi chochote. Hamna kitu pale zaidi ya porojo za mipasho.
Kuhusu east africa it is too early. Kule we need critical thinkers. Hivi sasa hapa east africa tz inatizamwa kama mwali mdoli ambaye anapaswa kuchumbiwa kwa mahari ya ng'ombe 100 kutokana na raslimali ilizo nazo. Sasa sijui mnaingia huko mkiwa mnajua warundi, wanyarwanda , wakenya na waganda wamekaa mkao wa kula. One mistake two goals kama lionnel messi. Haina maana kuwa critical ni kuwa radical. Ila kuwa na uwezo kutambua upana na marefu ya hoja hasa zenye muelekeo wa kujinufaisha na nchi yetu hali sisi wenyewe hatutapata kitu. Huo ndio ukweli uliopo africa mashariki pinga usipinge. Sasa huyu bishoo ataweza? Si bora hata dr adamson sigalla
 
yule mwingine the so called "Dr" Shayo ndio BURE kabisa
 
alinichekesha sana na mdano wa bilbilia alioutoa

huyu kweli mwanasiasa
 
Huyu kijana ni bogus.

Hawa ndio wanafanya tuanze kuichukia CCM.

CCM hawa watoto wa kina Malecela mngewaweka mbali kabisa na siasa za CCM wacha wakajiunge na vyama vya upinzani msingethubutu kuwakubalia hata uanachama, baba yake alifanyia nini cha maana Watanzania? zaidi ya kujilimbikizia Ng'ombe kila pembe ya Dodoma?
 
Kati ya vijana waliopita katika hatua hii ni Elibariki Kingu, Fancy Nkuhi, Mrisho Gambo na William Malechela tuwaweke kwenye mizania tuone ni yupi anastahili kuaminiwa na Watanzania ili awawakilishe katika chombo hicho muhimu
 
Back
Top Bottom