Hakika hatujapotea ikiwa tulichoanya ni kuunda nguvu ya nchi tano kuwa na msimamo mmoja ktk maswala ya kimataifa iwe hata kuunda msimamo mmoja ktk biashara na mali zetu ktk soko huria, lakini I doubt kama tunaweza kuwa na uwezo huo maana viongozi wetu wenyewe wana fungamana wanapoona kuna maslahi yao.. Na kama tunafanya jumuiya hii ikiwa ni hatua ya Pan Africanism waliyotaka kina Nkurumah na Nyerere - safi kabisa! lakini sii kufikiria kuboresha Uchumi wa nchi yetu hili tumeliwa sisi -hatuwezi kufaidika na hilo..- Bob Siamini kwamba tumepotea na EAC, ninaamini kwamba tupo sawa ila marekebisho tu yanatakiwa na ni lazima tupelekea Strong MPs huko, wanaoweza kusimamia interest ya Taifa letu, badala ya siasa zaidi. Nina tatizo na Sarafu Moja na Free Movemment ya wananchi wa Members States kwenye hayo mawili ninasema we need to be very carefull ama sivyo tutaumia sana na pia la Ajira kwa maoni yangu halijakaa sawa linahitaji marekebisha, lakini yote yanajadilika!
FMeS!
Mfumo wetu wa kodi ndani ni mbovu sana inahitaji marekebisho makubwa, Policies zetu ktk uwekezaji wa viwanda mbovu au wananchi wenyewe wanapenda biashara za kuzungusha fedha haraka (money laundry) ambayo imehalalishwa Bongo na ndio maana hatuna viwanda, less than 2% wana account bank, wanalipa kodi au wana TIN number tofauti na Kenya ambao mfumo wao umejengwa kibiashara zaidi na wapo tayari kuingia jumuiya hii kwa faida yao..Kwao it's all blessing lakini sisi hatuna zaidi ya Ujirani mwema.