Mwazange
JF-Expert Member
- Nov 16, 2007
- 1,056
- 83
Nimeisoma hii thread kuanzia mwanzo hadi hapa ninandikapo. Kuna mambo tofauitofauti niliyoyaona yamejitokeza hivyo na mimi nitaomba kuchangia kidogo.
1. Swali la msingi lililoulizwa tokea mwanzo na muanzilishi wa thread naona bado halijajibiwa. 'Je ni kweli bwana William anataka kugombea umbnge wa EAC?' Ningeomba muhusika ajibu, ili tuweze kuanza kuuliza maswali yanayohusiana na huo wadhifa rasmi. Maana hii sijui kafanya kazi gani lini na wapi, mimi kama mtanzania haikunizuia kuamka leo asubuhi na wala haitonizuia kwenda kulala leo usiku (Means it is not my business). Kama tutaanza kuchunguzana namna hii, nina imani hakuna kiongozi yoyote aliye msafi hapa duniani. Labda tuwarudishe Yesu na Muhammad ndio waje watuongozee siasa na maendeleo yetu.
2. Mjadala muhimu sana unaondelea wa kuhusu EAC; Ni muhimu sana kuangalia faida na hasara za hizi jumuia tunazojiingiza. Kuna yeyote aliyefanya tathmini ya nini tunachopata kwa sisi kuwemo kwenye hii taasisi? Maana naona this time around imekaa kibiashara/kimaslahi sana kuliko ilivyokuwa wakati uliopita(mtizamo wangu tu). Nini kimepatikana na nini kimepotea so far tokea kujiunga kwetu, na nini matarajio yetu kwa kuendelea kuwepo?
1. Swali la msingi lililoulizwa tokea mwanzo na muanzilishi wa thread naona bado halijajibiwa. 'Je ni kweli bwana William anataka kugombea umbnge wa EAC?' Ningeomba muhusika ajibu, ili tuweze kuanza kuuliza maswali yanayohusiana na huo wadhifa rasmi. Maana hii sijui kafanya kazi gani lini na wapi, mimi kama mtanzania haikunizuia kuamka leo asubuhi na wala haitonizuia kwenda kulala leo usiku (Means it is not my business). Kama tutaanza kuchunguzana namna hii, nina imani hakuna kiongozi yoyote aliye msafi hapa duniani. Labda tuwarudishe Yesu na Muhammad ndio waje watuongozee siasa na maendeleo yetu.
2. Mjadala muhimu sana unaondelea wa kuhusu EAC; Ni muhimu sana kuangalia faida na hasara za hizi jumuia tunazojiingiza. Kuna yeyote aliyefanya tathmini ya nini tunachopata kwa sisi kuwemo kwenye hii taasisi? Maana naona this time around imekaa kibiashara/kimaslahi sana kuliko ilivyokuwa wakati uliopita(mtizamo wangu tu). Nini kimepatikana na nini kimepotea so far tokea kujiunga kwetu, na nini matarajio yetu kwa kuendelea kuwepo?