Will the real Paul Makonda please stand up?

Will the real Paul Makonda please stand up?

Hivi unaamini kuna kesi itafunguliwa? C'mon ngosha!

Ndio yaleyale ya International Court of Justice(ICJ) tuliyoambiwa baada ya Uchaguzi Mkuu 2015.

Ninakuambia hakuna kesi bali ni porojo tu za kisiasa kama kawaida yetu.

Mwenye uwezo wa kufungua kesi ni mwenye vyeti ambaye anadaiwa kwa mujibu wa mchungaji Gwajima kuwa dada yake alichukua vyeti vyake. Hawa wanasiasa wengine wanapiga porojo tu.

Muda ni jibu sahihi. Tutakumbushana hapa Jamiiforums.
Kwahiyo kwa kuwa mwenye vyeti hajafungua kesi basi maana yake Bashite hawezi kuwa na kosa? Daudi Bashite ni nani kwani?
 

Attachments

  • Screenshot_2017-03-17-11-42-17.png
    Screenshot_2017-03-17-11-42-17.png
    89.6 KB · Views: 23
Kwahiyo kwa kuwa mwenye vyeti hajafungua kesi basi maana yake Bashite hawezi kuwa na kosa? Daudi Bashite ni nani kwani?

Unauliza swali na kujiuliza swali tena, wewe huyo huyo!

Upuuzi hupuuzwa na mtu mwenye kujitambua na kujiamini.

Wasiojitambua pia ni wale wasiojua vyeti vinatolewa na nani na vinaoneshwa kwa nani!
 
Hivi unaamini kuna kesi itafunguliwa? C'mon ngosha!

Ndio yaleyale ya International Court of Justice(ICJ) tuliyoambiwa baada ya Uchaguzi Mkuu 2015.

Ninakuambia hakuna kesi bali ni porojo tu za kisiasa kama kawaida yetu.

Mwenye uwezo wa kufungua kesi ni mwenye vyeti ambaye anadaiwa kwa mujibu wa mchungaji Gwajima kuwa dada yake alichukua vyeti vyake. Hawa wanasiasa wengine wanapiga porojo tu.

Muda ni jibu sahihi. Tutakumbushana hapa Jamiiforums.
Kakumbushane na bwana wako
 
In the interest of full disclosure, mimi sijui chochote kile cha ziada kuhusu hili sakata la vyeti vya mkuu wa mkoa wa Dar zaidi ya hiki ninachokisoma kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vinginevyo vya habari.

Lakini nikiwa mtu mwenye akili zangu timamu [well, naamini wapo wataobisha kuwa nina akili timamu, it's all good] nina maswali mepesi sana lakini ambayo naona kama vile hayana majibu kamili ya kueleweka.

Nimeshahoji juu ya uwezekano wa Makonda kufunguliwa mashitaka kwa manufaa ya umma. Hilo nimesikia kuna mtu au watu wanaolifanyia kazi.

Gwajima na Makonda wao naona wamegoma kabisa kutuonyesha vyeti walivyo navyo. Oh well...fine.

Sasa nije kwa huyo Paul Makonda halisi. Yaani Paul Makonda mwenyewe aliyeibiwa au aliyeuza [allegedly] huo utambulisho wake kwa Daudi Bashite.

Yeye huyo mtu yuko wapi?

Sasa hivi anatumia jina gani?

Anafanya shughuli gani?

Hivi huyo mtu hana ndugu, jamaa, na marafiki ambao wanaweza kutupa walau usuli [background] kidogo wa huyo mtu?

Naamini huyo Paul Makonda halisi haishi kwenye ombwe. Naamini anaishi miongoni mwa jamii.

Sasa kweli hao watu anaoishi nao na kukutana nao hakuna hata mmoja wao aliyejitokeza mpaka hivi sasa kusema lolote?

I'm getting so sick of this bullshit.

So will the real Paul Makonda please stand up...?

I repeat, will the real Paul Makonda please stand up...?
Kama aliuza cheti unategemea atajitokeza? Si ndo atapiga hela vizur

Pili lazima ujue kuwa jina makonda ni jina lililobadilishwa mahakamani baada ya jamaa kuapa. Palikua na surname la Paul kabla ya makonda
 
Tatizo wabongo kama wewe hujiulizi huyo mwingine original anatumia jina gani huko kwao aliko, maana na yeye mlituambia ni mwajiriwa pia.
Tatizo la wabongo wa design yako hawajui mnaweza kubadili surname kwa kuapa mkabak na first na second name;mnategemea partner in crime aje kumlipua mwenzie
 
Haoni tatizo lolote anaendelea na kazi yuko tayari kuwa sio kiongozi mzuri kwa mujibu wako. Unasemaje?
Kwa sababu hajaelimika.

Kiongozi aliyeelimika hawezi kuacha mzozo uendelee wakati anaweza kuumaliza kirahisi tu.

Obama kazushiwa si mzawa wa US, akatoa cheti cha kuzaliwa, akamaliza mzozo.

Huyo ndugu yenu anashindwa kujibu maswali kwa sababu hilo jina kaunga unga, si lake. Anaogopa akianza kujibu ataibua mengi zaidi.
 
Tatizo la wabongo wa design yako hawajui mnaweza kubadili surname kwa kuapa mkabak na first na second name;mnategemea partner in crime aje kumlipua mwenzie

Tatizo la wabongo kama wewe maneno na majungu tu yanasumbua, onesha kama una fotocopy ya vyeti vya form four, kwa mwajiri wa yule Paul Makonda original, ama na cheti nacho cha necta walibadili jina. Kama huna copy angalau ya hicho cheti ningekushauri uaache majungu na roho ya kwanini. Alibadili jina huyo Makonda original mpaka akabadili jina la baba yake , at the very least kamtafute baba wa huyo Makonda original tuone kitamburisho cha mpiga kura kiko je?
 
Kwa sababu hajaelimika.

Kiongozi aliyeelimika hawezi kuacha mzozo uendelee wakati anaweza kuumaliza kirahisi tu.

Obama kazushiwa si mzawa wa US, akatoa cheti cha kuzaliwa, akamaliza mzozo.

Huyo ndugu yenu anashindwa kujibu maswali kwa sababu hilo jina kaunga unga, si lake. Anaogopa akianza kujibu ataibua mengi zaidi.
Hakuna mzozo wowote kila kitu kinaendelea kama kawaida pamoja na kazi yake. Kujibu tuhuma sio lazima kiutamaduni wala kisheria ni utashi wa mtu. Kwahiyo huwezi kulazimisha utashi kuwa takwa lako.
 
kama 'hadithi' za vyeti vya makonda ni kweli, mmiliki halali wa cheti atakuwa hayupo nchini. sababu zitakuwa ni 1)kukwepa kesi ya kuuza cheti, 1)kufuta ushahidi kwa mnunuzi. kesi hii haitafika mahakamani. japo wanaweza kuwepo wanaomfahamu mtuhumiwa walipokuwa o level, ushahidi wowote itakuwa ni kuivua nguo serikali, hivo hakuna shahidi atakaeitwa.
 
kama 'hadithi' za vyeti vya makonda ni kweli, mmiliki halali wa cheti atakuwa hayupo nchini. sababu zitakuwa ni 1)kukwepa kesi ya kuuza cheti, 1)kufuta ushahidi kwa mnunuzi. kesi hii haitafika mahakamani. japo wanaweza kuwepo wanaomfahamu mtuhumiwa walipokuwa o level, ushahidi wowote itakuwa ni kuivua nguo serikali, hivo hakuna shahidi atakaeitwa.

Wamtafute baba wa Paul Makonda original ama naye alibadili jina baada ya mwanane kuuza cheti? ha ha ha ha wabongo majungu tu yanasumbua.
 
Paul Muyenge akabadili to paul Makonda kwa kuapia mahakamani.So huwezi kumkuta paul Makonda.
 
Hakuna mzozo wowote kila kitu kinaendelea kama kawaida pamoja na kazi yake. Kujibu tuhuma sio lazima kiutamaduni wala kisheria ni utashi wa mtu. Kwahiyo huwezi kulazimisha utashi kuwa takwa lako.
Hakuna mzozo wowote wakati wewe mwenyewe unazungumzia hii habari na kila sehemu ukienda ni habari kubwa?

Wewe kama una mahaba naye Bashite sema tu.

Ila usiseme hakuna mzozo wowote.
 
Wabongo aina ya nyumbu ni viumbe mbumbumbu sana, hasara tupu. Bora ng'ombe atakupatia maziwa.
 
Back
Top Bottom