Masterproud
JF-Expert Member
- Sep 14, 2012
- 441
- 118
Tukirudi kwenye maudhuri ya habari, Marehemu Mwaikusa alikuwa nafanya shughuli zake na mashirika mengi na watu binafsi katika uhai wake. Ni jambo la kawaida kitokeapo kifo uchunguzi kufanyika katika maeneo ambayo alikuwa anafanyia kazi na kuhusiana nao kikazi. Lakini tahadhari inatakiwa kuwepo kwani katika habari hii imeegemea zaidi shirika hilo la Benedictine Fadhers Peramiho wakati marehemu amefanya kazi katika mashirika mbalimali na watu mbalimbali lakini hawajatiliwa mashaka ya kuonyesha uzito kama jambo hilo linavyokuzwa hapa bila kuonyesha ushahidi wenye kuleta uzito. Kudhania tu huku na madhara ya kulichafua shirika ni kasoro kubwa ya vyombo vya habari kuandika habari kwa kina kupamba magazeti bila kufanya uchunguzi wa kina na kujiridhisha na ukweli wa wanachokianika gazetini, ndiyo kasoro inayoonekana wahariri wakuu wa vyombo vyetu vya habari na wanahabari wenyewe kutokuwa makini, labda wanakosa habari za kujaza kurasa za magazeti, hivyo kuchomekea mada zisizo na uchunguzi ulikamilika katika kesi nzito kama hii kunakoweza kusababisha uchafuzi wa hali ya hewa.
Hapo kuna kitu kinatakiwa kufichwa! na kinachotafutwa ni nafasi dhaifu! Aidha ni wapiga ramli wako kazini!Mh Abate lambert, na mauaji ya Prof, sijui!!
Ni lazima watu wasiamini tuhuma za kanisa ama watu wake wasiakini kuhusika na mauaji hayo kwa vile wao niwatakatifu sana. Labda tungeamini kama ingewahusisha watu wasiokwenye imani hiyo. NI MAONI TU
Hisia zangu ni kwamba huu ni uzushi wenye lengo la kuchafua kanisa. Kuna wadini Raia Mwema? Ni gazeti ambalo nalinunua kila wiki; lakini kwa makala za aina hii, itanibidi nitafakari kama niendelee kupoteza mia tano yangu kila wiki.
Abate Lambert Doerr OSB? Kama naota vile!
Hata Mhashamu Kadinali amewahi kuhusishwa na deal za DAWA ZA KULEVYA! Huu ni muendelezo tu
Mbona leo unatoka sana povu kwenye kutetea Umafia? Hao wameweka uchunguzi wao na wewe weka wako kupinga usitoe povu jingi mdomoni.Mengi hata mazuri yenye kufanywa kwa nia njema yanaweza kutafsirika kwa mtazamo wa kimafya kwa sababu iwe ni kweli au fitina.
Kinachonishangaza kiwete kumsingizia kushinda mbio
bado nina majonzi ya msiba wa baba askofu Aloysius balina, sitachangia uzi huu leo.
Jibu hoja sio jazba tu. Sasa ndio muone Uislamu unaposingiziwa kitu wanajisikia vipi waislamu wenyewe, uchungu ulioupata wewe na wengine wanaupata the same. Liwe funzo kuepuka kukashifiana humu JF. Ni hayo tu.Upumbavu mtupu! Na wewe uliyeleta hii maada you must be retarded and devoid of any sense of critical thinking. Shenzi type! Ningekuwa karibu na mwandishi wa huu upuuzi au mleta maada, wazushi wote wawili ningewapiga vibao vya nguvu! Pambaaf!
Picha:Kushoto watawa wa Peramiho wakiwa kanisani kusali sala ya Ofisio (liturujia ya vipindi) na kulia ni Kanisa Kuu la Abatia Peramiho ambalo zamani yalikuwa makao makuu ya Jimbo la Peramiho iliyokuwa Abatia Nulius (Kuongozwa na mkuu wa shirika la watawa) imezaa Jimbo Kuu la Songea, Jimbo la Njombe na Jimbo la Mbinga, ambayo ni majimbo yanayoongozwa na Maakofu wazalendo.
Shirika la Wabenedition Tanzania ambalo ni tawi toka shirika la Mt. Otilia kutoka Ujerumani kuingizwa kwenye tetesi ya kashfa ya mauaji ya Mwanasheria Mwaikusa, ni jambo la kushtua na si la kawaida, pengine ni mbinu ya kuyumbisha ukweli wa kilichojilia, huku wakihusishwa Br. Aidan OSB na Br. Edmond OSB kwa kile kinachoelezwa sahihi za hao wanashirika la Benediction Fathers Peramiho kukutwa kwenye document ya Mwaka 2003 inayoonyesha wanahisa katika machimbo yamgodi wa Lukarasi.
Jambo linalonishangaza ni kuhusushwa Abate Lambert Dor OSB ambaye ni mkuu wa shirika hilo huko Peramiho, wakati wahusika ni hawa wawili pengine walifanya mikataba binafsi na si shirika.
Ninavyoelewa kuna upungufu mkubwa kuhusu habari hiyo kwa maana kwamba wenye mamlaka katika shirika lao kufanya mikataba si kila mwanashirika, ila ni Procurator wa shirika mwenye dhamana na mambo ya uchumi wa shirika, na udadisi wangu bado sina hakika kama hawa ni wako katika kitengo cha procurator ya Peramiho Abbey, huenda ni miradi binafsi inayofanywa na hao mabradha wawili na hivyo kulitia aibu na miskusuko shirika. Pengine uchunguzi ufanyike kwa kiwango cha kisheria, maana kama habari ilivyoletwa inatoa mswali ambayo kuna upungufu mkubwa wa kulihusisha shirika hilo ambalo makazi yake yako St. Otillien, nchini Ujerumani.
Habari hiyo ni kama ifuatavyo hapo chini nukuru kutoka gazeti la Raia Mwema.
Hivi kubakwa watoto sio Ukatili? Mbona the same kanisa lishahusishwa na kiongozi wa dunia papaa aliomba radhi?Candid Scope,
..waliofanya mauaji hayo ni WAHUNI.
..watawa wa ukweli hawawezi kujihusisha na ukatili.
Pole sana, kwa kumuenzi Balina kemea kanisa kuacha maovu na vitendo vya ukatili, hilo litakuwa mchango tosha ukikaa kimya hawataacha huu Umafia worldwide.bado nina majonzi ya msiba wa baba askofu Aloysius balina, sitachangia uzi huu leo.
Yaani siamini kama JF mmetawaliwa na udini namna hii, hii habari ingehusishwa na dini ya kiislam leo hapa wasingepata mtetezi hata mmoja na ikiwa imetokea kwenye credible source kama Raia Mwema ambayo wakileta habari za ufisadi wa serikali na CCM tunasherekea bila hata kuwapa serikali muda wa kujitetea.
Hii inatofauti gani na habari za serikali kumuhua Daudi Balali? Mbona sikuona utetezi wa aina hii? Nimekuwa dissapointed na wana board itabidi habari za hapa niziangalie kwa busara zaidi, tumetawaliwa na udini kuliko objectivity
Sisemi watawa wameua lakini wanaweza kuua maana sio mara ya kwanza na wameua sana, ukiristo kama zilivyo dini nyingine zinaenezwa kwa upanga. So sio habari ya ajabu
Leo ndo nimetoka kifungoni, ngoja nikae kimya kidogo
Picha:Kushoto watawa wa Peramiho wakiwa kanisani kusali sala ya Ofisio (liturujia ya vipindi) na kulia ni Kanisa Kuu la Abatia Peramiho ambalo zamani yalikuwa makao makuu ya Jimbo la Peramiho iliyokuwa Abatia Nulius (Kuongozwa na mkuu wa shirika la watawa) imezaa Jimbo Kuu la Songea, Jimbo la Njombe na Jimbo la Mbinga, ambayo ni majimbo yanayoongozwa na Maakofu wazalendo.
Shirika la Wabenedition Tanzania ambalo ni tawi toka shirika la Mt. Otilia kutoka Ujerumani kuingizwa kwenye tetesi ya kashfa ya mauaji ya Mwanasheria Mwaikusa, ni jambo la kushtua na si la kawaida, pengine ni mbinu ya kuyumbisha ukweli wa kilichojilia, huku wakihusishwa Br. Aidan OSB na Br. Edmond OSB kwa kile kinachoelezwa sahihi za hao wanashirika la Benediction Fathers Peramiho kukutwa kwenye document ya Mwaka 2003 inayoonyesha wanahisa katika machimbo yamgodi wa Lukarasi.
Jambo linalonishangaza ni kuhusushwa Abate Lambert Dor OSB ambaye ni mkuu wa shirika hilo huko Peramiho, wakati wahusika ni hawa wawili pengine walifanya mikataba binafsi na si shirika.
Ninavyoelewa kuna upungufu mkubwa kuhusu habari hiyo kwa maana kwamba wenye mamlaka katika shirika lao kufanya mikataba si kila mwanashirika, ila ni Procurator wa shirika mwenye dhamana na mambo ya uchumi wa shirika, na udadisi wangu bado sina hakika kama hawa ni wako katika kitengo cha procurator ya Peramiho Abbey, huenda ni miradi binafsi inayofanywa na hao mabradha wawili na hivyo kulitia aibu na miskusuko shirika. Pengine uchunguzi ufanyike kwa kiwango cha kisheria, maana kama habari ilivyoletwa inatoa mswali ambayo kuna upungufu mkubwa wa kulihusisha shirika hilo ambalo makazi yake yako St. Otillien, nchini Ujerumani.
Habari hiyo ni kama ifuatavyo hapo chini nukuru kutoka gazeti la Raia Mwema.
Binafsi sijaona hoja yenye kulihusisha shirika la wamisionari wabenediktini hawa katika mauaji hayo, kwani kama kuonekana sahihi za baadhi yao kwenye mikataba au shughuli mbalimbali ni wengi sana na ni mashirika mengi na watu binafsi walifanya kazi kama hizo na Hayati Mwaikusa. Je hao wote wahisiwe kuhusika na kifo hicho eti kwa vile walisiana kikazi katika uhai wake basi ndio walitoa uhai wake?
Nisingependa mhariri wa gazeti achukue habari za vijiweni na kuifanya habari kuu kwenye gazeti lake isiyo kuwa na utafiti wala vielelezo vya kuridhisha umma kwa shirika kama hili limehusika kukodi wauaji.
Jambo moja hili si shirika la Tanzania, ni la kimataifa, maana yake hali inaweza kuchukuliwa kimataifa kwa vile wakuu wa shirika hilo si raia wa Tanzania, bali ni wa nchi ya kigeni. Ndio maana kuna umihimu Gazeti lithibitishe tuhuma hizo au la likanushe kwa uzito ule ule, vinginevyo lifungiwe kwa uzushi.
Labda Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Mhashamu Norbert Mtega atatoa kauli. Vinginevyo Mkuu wa shirika lao Abbot Jeremy toka St Otilien Ujeruman atoe ufafanuzi wa kuhisika shirika lake katika mauaji haya.