Who really killed Prof. Mwaikusa?

Kweli Tanzania hatutaendelea, watawa wanafanya njama za kuua kwa ajili ya pesa eti unawaita wahuni.

Ama kweli Tanzania italiwa kwelikweli, maana maliasili zinaondoka bado tunawatetea wahalifu.

Hiyo skandali ni kweli kabisa na shirika ndio lililokuwa linamiliki mgodi, hapa hakuna kumunya munya. Kwenye hili hakuna siri. Juu ya mauaji ya Prof sijui.

Subirini CHADEMA washinde migodi yote itamilikiwa na Shirika wakisaidiwa na Ujerumani. Hapa ndio mwisho wa Tanzania.

Are you sure what you talking about? Hayati Mwaikusa alifanya mashauri mengi kwenye makampuni mengi ya kitaifa na kimataifa, binafsi na ya kiserikali, jumuiya mbalimbali nk, iweje wadonoe kapunje haka na kutogusa sehemu ambazo zinaweza kuashiria uwezekano huu?

Unamfahamu Rt Rev. Abbot Lambert Dorr OSB wa Abatia Peramihi, wilaya ya Songea vijijini katika Mkoa Ruvuma ambaye alikuwa anaongoza Abatia hiyo ya wamisionari wabenediktini ambayo makao yake makuu yako St. Otilien nchini Ujerumani na makao makuu ya confoederation yakiwa Rome wanakoendesha Chuo cha St Anselm ambao kinatoa mafunzo ya shahada za Liturgia ya kanisa, Mkuu wa hapo St Anselmo akiwa ni Victor Damez aliyekuwa Mkuu wa St Otilian?

Huo uchafu wa mgodi ni nini ukilinganisha na makubwa yalifanywa miaka nenda rudi kujenga mashule, hospitali, zahanati, vituo vya afya, na mengineyo, ni mgodi gani waliouendesha kupata pesa za kujenga hayo kama si misaada ya waumini na serikali ya Ujerumani na Uswiss kufadhili hayo yote?

Unafahamu umri wa hawa wazungu wa Ujerumani? Kama nilivyokuambia sasa hivi ni wazee ambao hata kukumbuka maua kuyamwagilia uani pao hawana, halafu wahangaikie migoni ya uswahilini? Zaidi kibaya eti kupanga na kumwuka Maikusa? Kama hatua zikichukuliwa na wahusika kulishinikiza gazeti lithibitishe publication nakuhakikishia itaumbuka.

Mhariri mkuu wa gazeti hilo anatakiwa kutafakari vya kutosha kuhusu upotoshaji huo, wasionewe wanyonge kwa vile hawana uwezo wa kujenga hoja za kujitetea.
 
Wewe vilevile you're guilty sababu una-propagate na ku-sensationalize upuuzi kama huu. Kama hii habari ungeiacha kule Raia Mwema, sidhani kama kuna mtu angehangaika nayo, maana ni ujinga mtupu.

Habari hiyo imeshanukuliwa na vyombo vingi.

Kunyamazia upuuzi huu maana yake kushabikia vyombo hivyo vya habari viendelee kufanya upuzi ule ule, lazima kieleweke na wafanye tathmini ya kutosha kabla ya publication. Tukinyamaza kesho watafanya mabaya zaidi ya hili. Unachotaka mwanao anapoharibi kitu ni kunyamazia tu badala ya kufanya jitihada kuonya asirudie makosa hayo.
 
Nikilinganisha hizi habari, Raiamwema siwaelewi kabisa

Rwanda yatajwa kifo cha Prof. Mwaikusa | Gazeti la MwanaHalisi

Mwanahalisi walikuwa wanafanya uchunguzi na uchambuzi wa kina ambao hata kuwashtaki ilishindikana ndio maana serikali ikatumia uamuzi wa mezani kupitisha rungu lake kutokana na kuabishwa yanayojilifichika. Raia mwena huwa mimi si msomaji wake, kwani uchambuzi wao hauko makini, wanachukua habari za vijiweni na kuziweka ukurasa wa mbele na kuzipa uzito wa juu.
 
Habari hiyo imeshanukuliwa na vyombo vingi.

Kunyamazia upuuzi huu maana yake kushabikia vyombo hivyo vya habari viendelee kufanya upuzi ule ule, lazima kieleweke na wafanye tathmini ya kutosha kabla ya publication. Tukinyamaza kesho watafanya mabaya zaidi ya hili. Unachotaka mwanao anapoharibi kitu ni kunyamazia tu badala ya kufanya jitihada kuonya asirudie makosa hayo.

Kwa hiyo inaonekana nia yako ya kubandika maada hii is just so that kwamba wewe mwenyewe, pekee yako na kwa juhudi zako binafsi, uweze ku-refute every single issue mentioned in the story, au siyo? Waingereza wana msemo "Dont bite more than you can chew". Sasa una kazi kubwa sana, maana kuna watu wa kila aina humu ndani wenye backgrounds and convictions za kila namna. Jee, unaweza kuwaridhisha wote kwa maandishi yako pekee yake?
 
monks.jpg

Mkuu wa Shirika la Peramiho Benedictine Fathers (OSB) Abate Lambert kwenye picha hiyo aliyeko mbele mstari wa nyuma mpenda watu, mleta maendeleo na usitawi wa wananchi wengi ukanda wa Ruvuma na Kusini nyanda za juu kwa wengi wanashangazwa na habari hiyo toka Raia Mwema yenye taswira ya kuchafua badala ya ukweli halisi.

Bahati nzuri siku za nyuma nilipokuwa mwanahabari nilifanikiwa kuwepo kikazi maeneo hayo mwenyeji wangu akiwa Ahmed Jongo. Baadhi ya watajwa nawafahamu si kitu cha kawaida kufanya jambo kama hilo ukitilia maanani ninavyomfahamu Abate Lambert Dor na anavyoheshimika katika Jimbo la Songea na majimbo yandokando na naendeleo kwa wananchi. Hospitali ya St. Joseph Peramiho ndio kimbilio kubwa ukanda huo. Shule ya sekondari Peramiho imetoa wasomi wengi wa kike nchini. Kuna mengi naona wasioijua Peramiho ndio wanaoweza kuzusha mambo yasiyo na kichwa wala miguu, flagment.

UKIINGIA KWENYE BIASHARA UNAKUWA UMETOKA KWENYE UTAKATIFU. sishangai sana kama wakihusishwa.biashara maana yake faida.faida ni kwa njia yeyote ikiwemo kukwepa kodi, magendo, kuua yeyote anaye kukwamisha kupata faida n.k
 
Hivi ndivyo inavyouma mtu akikukwaza kuhusu imani yako!nadhan ni fundisho humu jf kuhusu kuheshimiana,naona watu kama wamemeza omo vile.
Hizi dini mbili za wakoloni sometimes zinamfanya mtu asiweze hata kufikiri nje ya box.
 
Najiukiza mazingira ya kifo cha mwaikusa na barlow hayatofautiani sana,ila polisi wapo busy sana na issue ya barlow than that late man,mwaikusa kwanini?
 
Kwa hiyo inaonekana nia yako ya kubandika maada hii is just so that kwamba wewe mwenyewe, pekee yako na kwa juhudi zako binafsi, uweze ku-refute every single issue mentioned in the story, au siyo? Waingereza wana msemo "Dont bite more than you can chew". Sasa una kazi kubwa sana, maana kuna watu wa kila aina humu ndani wenye backgrounds and convictions za kila namna. Jee, unaweza kuwaridhisha wote kwa maandishi yako pekee yake?


Kwenye maovu tunatabia ya kuonya na kukemea yasijirudie, kwa wale ambao hawana hulka ya kubadilika kwa ushupavu wao ni tatizo lao na yakayowapata hatumo kwa vile sisi tumejitahidi tulishoweza kuwasahihisha lakini hawasahihishiki. Wale ambao kwa unyofu wa moyo wakiona wameteleza, nafasi hii wataihusujia kwani ni kioo cha kujitazama wasifanya makosa yale yale kila leo.

Hii ndio maana ya retreat, bila hivyo tusingekuwa na nafasi ya kujirudi.
 
Taarifa inasema aliuwa na majambazi akiwa ndani ya gari mbele ya get la nyumbani kwake, wakati anajiandaa kuingia ndani, 'majambazi' hao walikimbia mara baada ya tukio hilo bila ya kuchukua kitu chochote. Hiyo ni taarifa Polisi kwa mujibu wa mlinzi. Sasa hapa sijui ni documents zipi walizopora na je wanasheria huzurula na documents halisi au vivuli?
Taarifa nyingine, nje ya jeshi la Polisi na mlinzi iliihusisha serikali ya Kagame na mauaji yale, na nyingine ikaihusisha serikali ya Tanzania, kuwa ilitelekeza hayo kwa lengo la kufukia ukweli juu ya suala la balali.
Na sasa hv tena kuna wachunguzi wanakuja na taarifa zao kuhusu uhusika wa shirika la kitawa.
Inawezekana kabisa ikawa hivyo, lakini msingi wa vielelezo vinavyojengwa ni dhaifu sana kubeba tuhuma.
 
UKIINGIA KWENYE BIASHARA UNAKUWA UMETOKA KWENYE UTAKATIFU. sishangai sana kama wakihusishwa.biashara maana yake faida.faida ni kwa njia yeyote ikiwemo kukwepa kodi, magendo, kuua yeyote anaye kukwamisha kupata faida n.k

Jambo la msingi yahati Mwaikusa alifanya mengi tu kwa makampuni na watu binafsi, lakini kwa nini waelemezwe mzigo huu hawa wamisionari bila uthibitisho wa ushahidi wao kukodi wauaji toka Peramiho Mission wamvizie nyumbani kwake Dar?
 
Nijuacho ni kuwa prof aliuawa na watu wanaozaniwa ni toka burundi na rwanda nse prof alikuwa anasimamia baadhi ya kesi
Hii ya leo ndo nashangaa ila kama wanahusika hao watawa mbona wangetumia mbinu zingine kutekeleza hayo bse prof aloshindiliwa risasi za kutosha na mpaka leo kimya

Na ya Daudi Balali je!?
 
Taarifa inasema aliuwa na majambazi akiwa ndani ya gari mbele ya get la nyumbani kwake, wakati anajiandaa kuingia ndani, 'majambazi' hao walikimbia mara baada ya tukio hilo bila ya kuchukua kitu chochote. Hiyo ni taarifa Polisi kwa mujibu wa mlinzi. Sasa hapa sijui ni documents zipi walizopora na je wanasheria huzurula na documents halisi au vivuli?
Taarifa nyingine, nje ya jeshi la Polisi na mlinzi iliihusisha serikali ya Kagame na mauaji yale, na nyingine ikaihusisha serikali ya Tanzania, kuwa ilitelekeza hayo kwa lengo la kufukia ukweli juu ya suala la balali.
Na sasa hv tena kuna wachunguzi wanakuja na taarifa zao kuhusu uhusika wa shirika la kitawa.
Inawezekana kabisa ikawa hivyo, lakini msingi wa vielelezo vinavyojengwa ni dhaifu sana kubeba tuhuma.

Binafsi sijaona hoja yenye kulihusisha shirika la wamisionari wabenediktini hawa katika mauaji hayo, kwani kama kuonekana sahihi za baadhi yao kwenye mikataba au shughuli mbalimbali ni wengi sana na ni mashirika mengi na watu binafsi walifanya kazi kama hizo na Hayati Mwaikusa. Je hao wote wahisiwe kuhusika na kifo hicho eti kwa vile walisiana kikazi katika uhai wake basi ndio walitoa uhai wake?

Nisingependa mhariri wa gazeti achukue habari za vijiweni na kuifanya habari kuu kwenye gazeti lake isiyo kuwa na utafiti wala vielelezo vya kuridhisha umma kwa shirika kama hili limehusika kukodi wauaji.

Jambo moja hili si shirika la Tanzania, ni la kimataifa, maana yake hali inaweza kuchukuliwa kimataifa kwa vile wakuu wa shirika hilo si raia wa Tanzania, bali ni wa nchi ya kigeni. Ndio maana kuna umihimu Gazeti lithibitishe tuhuma hizo au la likanushe kwa uzito ule ule, vinginevyo lifungiwe kwa uzushi.

Labda Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Mhashamu Norbert Mtega atatoa kauli. Vinginevyo Mkuu wa shirika lao Abbot Jeremy toka St Otilien Ujeruman atoe ufafanuzi wa kuhisika shirika lake katika mauaji haya.
 
Wakati mwingine tunapaswa kuwa makini sana na taarifa za magazeti, hivi watawa/mabruda wanaweza kweli kuhusika na mambo ya UJAMBAZI wa kumuua Prof. Mwaikusa (R.I.P)?

Je ya RWANDA yalihishia WAPI??
 
Kwa nini wasikamatwe???Wauaji ni wahalifu na kama kweli serikali inajua hivyo kwa nini mpaka leo wako nje??? Je vyanzo vya mwandishi ni vipi? Kwa nini wauaji wa Prof kila mara wanabadilika?

Usalama wa taifa ndio chanzo cha habari za mitaani kwani wangefanya kazi yao ipasavyo tetesi, hisia, shuku, visingekuwepo. Tutahisiana mwisho wa siku ni sheria kifuani, miguuni, mkononi halafu tutasoma namba.
 
Inafahamika kuwa prof Mwaikusa aliuwawa na serikali ya kagame nd hili linahusishwa sana na yeye kujiingiza na siasa za mauaji ya kimbarik nchini Rwanda...Raia mwema
chini ya uenyekiti wa Jeneral Ulimwengu
wana interest na ukaribu na rwanda na hapa wanajaribu kupotosha

Wewe ni Great Thinker,Ukweli upo TISS huyu mzee JU anatumia falsafa ya miluzi mingi humpoteza mbwa!
 
Nikilinganisha hizi habari, Raiamwema siwaelewi kabisa

Rwanda yatajwa kifo cha Prof. Mwaikusa | Gazeti la MwanaHalisi

Mkuu hata timing yake ni highly questionable - kuna kitu wanataka ku-pre empty hapa! Kuna wakati fulani mwandishi mmoja alikuwa amepania kupotosha habari kuhusu mapinduzi ya Zanzibar - anawasema vibaya wakina Okello na wengine, yaani anaonyesha wazi wazi chuki zake binafsi na kujaribu ku-water down efforts za watu walijitolea muhanga!

Mwenyekiti wa gazeti la RaiaMwema Bwana Ulimwengu ni mtu mahili sana, amewahi kufanya kazi Serikalini na anajuwa mambo mengi sana including ukweli kuhusu kilicho jili wakati wa wapinduzi ya Zanzibar; mimi nilikuwa najiuliza maswali mengi: kwa nini alikuwa anaruhusu wandishi wa habari kupotosha ukweli kimaksudi!!
 
Yaani siamini kama JF mmetawaliwa na udini namna hii, hii habari ingehusishwa na dini ya kiislam leo hapa wasingepata mtetezi hata mmoja na ikiwa imetokea kwenye credible source kama Raia Mwema ambayo wakileta habari za ufisadi wa serikali na CCM tunasherekea bila hata kuwapa serikali muda wa kujitetea.

Hii inatofauti gani na habari za serikali kumuhua Daudi Balali? Mbona sikuona utetezi wa aina hii? Nimekuwa dissapointed na wana board itabidi habari za hapa niziangalie kwa busara zaidi, tumetawaliwa na udini kuliko objectivity

Sisemi watawa wameua lakini wanaweza kuua maana sio mara ya kwanza na wameua sana, ukiristo kama zilivyo dini nyingine zinaenezwa kwa upanga. So sio habari ya ajabu
 
Tunasahau kuwa sisi ni binadamu, hakuna mkamilifu wala malaika, na ahukumiwe kama ni kweli, tena wawaexpose kabisa kwa kufanya uhalifu chini ya kivuli chà kanisa
 
Back
Top Bottom