Who is Salim Ahmed Salim?

Vichwa vingine vinafaa kufanya kazi chini ya Amri! mambo ya Hewala mkubwa!
 
FMES na Nyani Ngabu hawakosei kabisa!
Waafrika ndo tulivyo!

Ila mkuu, kwa nini tuwapigie kura watu wasiotaka kutoka madarakani?
Vipi kuhusu watu kama Maalim Seif, tangu 1995 anagombea yeye tu?
Siku akishinda ataweza kutoka madarakani kwa hiari kweli?

Dah kwa kweli hili hata mie huwa linanishangaza sana ingawaje wana demokrasia na maendeleo wamekuwa wakijaribu kuonyesha mfano bora wa demokrasia lakini vyama vingine vya upinzani wamekuwa wakienda tofauti kabisa na demokrasia wanayoihubiri majukwaani..hivi jamani kwa mfano ktk CUF ama TLP..ina maana hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kugombea urais ukiacha bwana profesa haruna/maalim seif na muheshimiwa lyatonga?

Sijui, lakini kwa tafakari yangu naona hapa kuna tatizo kubwa, tena saana tu.

Otherwise pengine ndio mfumo uliopo kwenye katiba husika, kwamba mtu agombee mpaka ashinde, mtizamo wangu tu.
 
Prof Lipumba,
Unasemaje kuhusu Salim na Vasco?

"I personally know Kikwete as a nice guy but I don't consider him to be presidential material. I don't think he is serious,"

(would rather have seen Dr. Salim Ahmed Salim as a President?)

"Failing to elect Salim Ahmed Salim (for presidency) has damaged the union. You can never get a Zanzibari as qualified as Dr. Salim," Kikwete is the so-called youth candidate even though he is one year older than me.

He was a year ahead of me at the university. But as an individual he is not a threat to me. To me, Salim was a bigger threat," (Lipumba said this in 2005)
 
Hii ya Kalamu hata mimi imenikata maini kabisa pamoja na mapenzi yangu kwa Salim. Yaani huyu bwana hutakuja kumsikia akinyanyua mdomo kabisa kuhusu uozo wote unaendelea. Sasa wakati mwingine tunashindwa kujua convictions zake ni zipi na kama hatujui convictions zake anatukwaza sana sisi wapenzi wake kumtetea mbele ya vichwa kama akina FMES!

Hata hivyo nafikiri huyu mzee wetu walishamjeruhi sana na sidhani kama anaweza kuuzika tena na kukabili mashambulizi ya wanasiasa wa leo TZ.

Anaweza kuhimili, si unaona McCain baada ya 2000 amerudi tena, sema swali la kujiuliza wananchi tuko tayari kumchagua na kumpitisha?

Kwenye hili la kuzungumzia ufisadi anajua mwenyewe kwa nini yuko kimya kuna watu kadhaa ambao I have always admired them naona wamekaa kimya tangu hili sakata la ufisadi limeanza.

On the other hand wakizungumza tutasema wanataka cheap political attention na tutaanza kuuliza walikuwa wapi siku za nyuma and blah blah...
 
Anaweza kuhimili, si unaona McCain baada ya 2000 amerudi tena, sema swali la kujiuliza wananchi tuko tayari kumchagua na kumpitisha?

Kwenye hili la kuzungumzia ufisadi anajua mwenyewe kwa nini yuko kimya kuna watu kadhaa ambao I have always admired them naona wamekaa kimya tangu hili sakata la ufisadi limeanza.
On the other hand wakizungumza tutasema wanataka cheap political attention na tutaanza kuuliza walikuwa wapi siku za nyuma and blah blah...

Wait a moment, tusikatike maini, sio lazima imani juu ya uwezo wa mtu ijengwe juu ya kasema nini
waswahili wanasema; mja hunena, muungwana hutenda.

Aidha, tokea siku nyingi concerns za Salim sio Ufisadi tu, kinamuuma zaidi ufukara wa waafrika. Namnukuu:
"…Democracy must deliver on bread and butter issues; otherwise democratic transitions will be reversed and the continent will slide back into situations where the politics of poverty give rise to the poverty of politics.

While linkages between good governance and sustainable economic development might not necessarily be perfect guarantees for sustaining democracy and a culture of political tolerance, they were nevertheless "important thresholds in creating acceptable African norms and behaviour" hii aliisema Oktoba 1999
 
Dah kwa kweli hili hata mie huwa linanishangaza sana..ingawaje wana demokrasia na maendeleo wamekuwa wakijaribu kuonyesha mfano bora wa demokrasia lakini vyama vingine vya upinzani wamekuwa wakienda tofauti kabisa na demokrasia wanayoihubiri majukwaani..hivi jamani kwa mfano ktk CUF ama TLP..ina maana hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kugombea urais ukiacha bwana profesa haruna/maalim seif na muheshimiwa lyatonga?? Sijui.. lakini kwa tafakari yangu naona hapa kuna tatizo kubwa..tena saana tu..otherwise pengine ndio mfumo uliopo kwenye katiba husika..kwamba mtu agombee mpaka ashinde..mtizamo wangu tu...

Nilimsikia mwenyewe Lyatonga akisema nji ii kama hajatosheka basi, hagombei tena bali atamuunga mkono mgombea atakayesimamishwa na umoja. Haya aliyasema Mji kasoro bahari hadharani tr. 5 May 2007 saa 11 na dk. 7 jioni.
 
Dah kwa kweli hili hata mie huwa linanishangaza sana..ingawaje wana demokrasia na maendeleo wamekuwa wakijaribu kuonyesha mfano bora wa demokrasia lakini vyama vingine vya upinzani wamekuwa wakienda tofauti kabisa na demokrasia wanayoihubiri majukwaani..hivi jamani kwa mfano ktk CUF ama TLP..ina maana hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kugombea urais ukiacha bwana profesa haruna/maalim seif na muheshimiwa lyatonga?? Sijui.. lakini kwa tafakari yangu naona hapa kuna tatizo kubwa..tena saana tu..otherwise pengine ndio mfumo uliopo kwenye katiba husika..kwamba mtu agombee mpaka ashinde..mtizamo wangu tu...

kwani hao wana democrasia na maendeleo ndio kwanza walirusha ndoano yao ya kwanza 2005?? tusiwape sifa ya democrasia wakati nao wanamapungufu yaleyale, kwa mfano viti maalum wote kutoka mikoa flani je hiyo ndo democrasia? ni mtazamo tu
 
The President who never became.

Thats sound like a cute title of the Book. Mkumbo unasemaje?

Iandikwe hivi bwana, S.A.S THE DELAYED PRESIDENT
akingali hai u never know
Siku akitwaliwa hajawa ndio biography za never became ziandikwe.
 
Swali kubwa ni je Salim ana future ndani ya CCM kama anataka kuliongoza Taifa letu?

Kasifa kamoja kachafu katika CCM ni kuwakataa watu wenye uwezo, this is the biggest weakness ya CCM ambayo bahati mbaya wana CCM wengi wasio viongozi hawaijui.

Yaani kuwa na uwezo katika CCM tayari ni kikwazo kikubwa sana, wao wanataka uwe mswahili swahili hili hivi, usiwe serious; the likes of JK, Mudhihiri, Makamba, Nchimbi, etc ndio wanatakiwa kwenye CCM na ni watu aina hii watakaopambana na akina Zitto kwenye chaguzi za miaka 10 ijayo.

Sasa mzee wetu Salim na watu kama akina Mwandosya, Magufuli, Mwakyembe, etc kwa kweli itabidi wasahau kabisa kupata nomination ya presidency au hata uwaziri mkuu kupitia CCM.

Sasa hawa jamaa wa aina ya Salim wangekuwa majasiri wangejisogeza CHADEMA haraka sana. Lakini sidhani kama huo ujasiri wanao, wakati utatuambia.
 
CCM wakituletea huyu 2010 mbona nitawapenda!!, kama hawataweza kumwambia Vasco da Gama aachie usukani, basi angalau wamsimamishe Visiwani Zanzibar. just a wish Tena kama hawataki, heri utaratibu wa mgombea binafsi ungeharakishwa, hapo watanzania tunakamata huyu tunaunganisha na Dr.Slaa, bonge la timu ya ushindi halafu uone kama TZ haitabadilika,au sio jamani?


Nyie watu mimi mbona mnanisikitisha? bado mnaitaka ccm? Salim ni mtu safi, ila ccm ni wachafu na hawataki kuwaanika wachafu ili waoshwe so hatujui nani ni mchafu zaidi na nani ni msafi sana. watamchafua huyu bwana!!! haijalishi rais ni msafi kiasi gani hawa mabwana hawaaminiki tena.

Mimi nimeamua kupotezea kura yangu upinzani mpaka siku itakapo-make a difference! kwani watu walisemaje kuhusu Jakaya? lakini serikali yake iko wapi? ameshavunja baraza mara ngapi na mara ngapi mmeshawishika kuona analivunja tena? kama watendaji ni wabovu yeye hawazi. Stress peke yake inaweza ikamfanya mtu ashindwe kutoa maamuzi.

Mmeyaona kwa JK!! Salim ni mtu mwenye busara na aliyaona hayo kitambo na ndio maana alipoambiwa agombee alikataa, nani anakataa kuwa mkuu wa nchi kwa nchi inayoongozeka? ni nchi kama yetu ndio watu wanakataa, kwani at the end of the day yyeye ndio ataonekana hana wala hakutumia busara. Paulo usije kucheza na sisi una mikono michafu!

Au mmesahau?
 
Mkuu Gamba,

Heshima mbele, tatizo sio CV za viongozi wetu, isipokuwa tatizo ni CV za sisi wananchi wapiga kura, Salim ana CV nzito lakini tatizo ni kwamba urais hauamuliwi na CV peke yake, kwa bahati mbaya pamoja na CV yake kuwa nzito, alishindwa kwenye uchaguzi wa mgombea wa rais wa CCM,

Sasa kama Muungwana tu alimshinda kule CCM, je atawezaje kupambana na kina Freeman, na Lipumba? Na je akikutana na Dr. Slaa sio ndio itakuwa mauti kabisa kwetu CCM! Pole pole ndugu, urais ni pamoja na kushinda uchaguzi,

Salim ni kweli ana CV nzito, na pia ametuweka kwenye ramani ya Dunia politically, lakini tatizo hakuwa na political base nyumbani, kuanzia visiwani mpaka Bara, sasa uongozi wa kubebwa kama wake ulimalizwa na siasa za vyama vingi!

Otherwise, ni kweli CV yake ni nzito sana!



Kwa mtazamo wangu, kushindwa kwake hakuhusiani na kushindwa kuwa-empress wananchi kwani wananchi hawapitishi mgombea wa chama. Wachafu wale walio atakuwa kikwazo kwenye biashara zao so wakamweka kando.

Kama huijui ccm unaweza kufikiri ni watu wazuri la hasha wale mabwana wametawaliwa na mizengwe bila kusahau propaganda zinazolenga kulinda maslahi binafsi.
 
Bosi Kitila, kama SAS analipa hivyo na CCM si mahala pake kwa nini ahamie CHADEMA na sio Chama cha Demokrasia Makini kwa Prof. Shayo?

Hivi kile kijiji chake cha Sayansi na Teknolojia kimeishia wapi? Maana jamaa ilifaa azaliwe Cuba maana ni mjamaa mno!
 
SAS aliangushwa na chama chake cha CCM, na sidhani kama alijua uozo kamili wa CCM alipoamua kugombea 2005. Alipokuwa anazunguka mikoani na kuona dirty techniques za wanamtandao na kashfa walizoibua dhidi yake macho yake yalifunguka. Na ukifuatilia kwa karibu alifanya maamuzi ya kuwa backbencher na hajihusishi na siasa za ndani.

Mimi naamini hawezi kubadili CCM, na anavyoendelea kubaki ndani ya chama, he is associated with the fisadiz apende asipende. He has to take the leap, na kuwa independent candidate, atapata kura za wananchi. The question is, is he ready to fight for the country?

Nafahamu kwamba SAS took it very personally kutokana na racial tone ya kampeni na alikataa tamaa akaahidi hatagombania nafasi yoyote Bongo. He is happy with his internatonal limelight. Swali, je yuko tayari kurudi?
 
CCM ni kama mtoto mtukutu aliyezoea uchafu akimuona mama yake au yaya anakuja kumwosha basi anaanza kupiga kelele na kulia. Kwake yeye watoto wenzie wachafu ndio marafiki zake wakubwa.

No wonder sisi tutaendelea kuburuzwa na wakenya kiuchumi kila siku kwa sababu ya kuwa na viongozi kama akina makamba
 
Huyu kwani amezaliwa wapi labda niulize amezaliwa Tanzania ? ,Amezaliwa Zanzibar ,amezaliwa Tanganyika Amezaliwa Unguja au amezaliwa Pemba.

Nikiwapanga na0na Picha ya Salim naona picha ya Dr.Omar naona picha ya Mzee wa Mikasi (Dr.Shein)sasa suali je hawa kwa muonavyo nyinyi wanaweza kuwa Maraisi wa Tanzania ?
Kama kipimo ni mtu kwao Salim kwao Pemba Mkoani ,Shein nafikiri Mtambwe na Marehemu Dr.Omar labda wawi pia sina uhakika.

Je watu hawa tokea wapate uongozi wa juu ukianza na Ubunge wamewafanyia kitu gani watu wa kwao waliwahi kutetea sehemu wanayo toka, naona kama ni watu wapendao madaraka tu na kila wakienda juu husahau na kuwasahau waliowawacha njiani makwao ni sawa na wabunge ambao hawaonekani kwao mpaka wakati wauchaguzi jambo ambalo wananchi wameanza kuwakacha wabunge wa aina hii ambao ni mzigo usio na faida wakishaufikisha pale penye matumaini kwamba atatusaidia akipata ubunge na ahadi kabakaba.

Naamini kabisa kuna wabunge hawajawahi kusema hata neno moja zaidi ya kupiga makofi na kushangilia hata hawajui ni kitu gani wanashangilia just wamo tu ,lengo na nia pamoja na madhumuni waliokwendea bungeni na matatizo yote waliyowaahidi wapiga kura wao yanakuwa kapuni na hata hawayabebi kuelekea nayo DODOMA kwani ni mzigo wasio weza kuusemea mbele za wabunge wenzao.

Na hawa akina Salim ni watu ambao hawana uzalendo zaidi ya kujituma kwa ajili ya wengine ni kivuli cha Mvumo. Kaeni chonjo nao.

Tunataka viongozi ambao wanasimama bungeni na kupigia makelele uwoza ndani ya serikali bila ya kuogopa ,yaani hawa ndio viongozi wa kupigania kuwepo madarakani ,hivi ni nani shujaa kama Seif Sharif pale aliposimama mbele ya Mwalim Julius Nyerere na kupinga Zanzibar kununua mafuta kutoka Tanganyika kwa bei ya fedha za kigeni na kumwambia Nyerere kuwa ikiwa tutahitajika kununua kwa fedha za kigeni basi tutatafuta pale yanapouzwa kwa bei poa.

Hawa ni watu ambao hawana muhali katika kulinda maslahi ya Taifa na mwisho wake mwenyewe mwalimu Nyerere aliamini kama huyu kiumbe sio mchezo akamwalika kula pilao Butiama na mpaka leo Wabutiama wanamheshimu Seif Sharif wakijua ni mtu anaejali raia na kufika kumpa uchifu wa kikuria.

Hakuna kitu cha kufanya zaidi ya kuiondoa CCM madarakani ili kuwezesha kujenga ukuraza mpya wa maisha bora kwa kila Mtanzania ,lakini kwa hizi kasi mpya WaTanzania wataachwa njiani na Kikwete wakibaki kusema CCM ndio baba ,baba gani anawacha watoto wanakufa njaa na wazazi wanawake kujifia mahospitalini wakilala kwenye sement na kitanda kimoja watu watatu hivi hizi ndio kasi za CCM na Kikwete au ni kasi za CCM na kiwete ,maana hawezi kufanya lolote miaka inakatika yeye anasafiri kila siku akirudi anabadili mawaziri na kuingiza marizavu ,yaani kama hawa marizavu wangekuwa wazuri kwa nini wasichezeshwe kwenye kipindi cha mwanzo, kwa ufupi timu nzima ya CCM ni mbovu na imeoza na haitapwata ushindi kwa maisha bora kwa kila Mtanzania na badala yake itakuwa huzuni na vilio na maisha duni kwa kila Mtanzania kadiri ya siku zinavyosonga mbele na ndio kama tuonavyo mabilioni ya fedha yamechotwa na hakuna kinachorudishwa zaidi ya kudanganywa na watu wanaojiita viongozi wa umma.Kubwa lijalo !!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom