Mkuu ndizi ni zaidi ya tunda. Personally nikila ndizi mbivu au mbichi sioni kama vile nakula tunda. Suala kama ndizi ni tunda tuu au ni zaidi ya tunda limeshafika mpaka mahakamani.
Tafuta na uisome kesi moja mashuhuri sana ya United Brands vs European Commission. United Brands walikuwa ni major suppliers wa ndizi kwenye Umoja wa Ulaya. Walikuwa wana-import ndizi mbichi na mbivu.
Kwenye kesi hiyo, mahakama ilikuwa inaamua, pamoja na mambo mengine, soko la ndizi (relevant product market) in the context of competition law.
United Brands walidai kuwa soko la ndizi limejikita tuu kwenye matunda. European Commission wakadai kuwa ndizi ni zaidi ya tunda na kwamba the relevant product market siyo matunda bali ni ndizi.
Mahakama iliamua kuwa soko la ndizi ni tofauti na soka la matunda. Mahakama ilisema zao la ndizi lina special attributes kama mwonekano, taste, ulaini na kutokuwa na mbegu.
Mahakama iliongeza kuwa zao la ndizi ni muhimu sana kwa watu kama watoto, wazee na wagonjwa. Zaidi ndizi hazizalishiwi kwa msimu kama matunda ambayo yanapanda na kushuka bei kulingana na msimu wao.
Hii kesi inaonyesha tofauti kubwa iliyopo kati ya ndizi na matunda. I am sure hata wataalamu wa afya na lishe (achilia mbali Wahaya na Wachaga) watakuambia kuwa ndizi ni zaidi ya tunda. Usitake kuniambia hii ni miti ya matunda.