What is your favorite food?

What is your favorite food?

grilled-chicken.jpg

hii tamu sana ila hiyo misukari juu hua inazingua sana..
 
Huyu Mkereketwa_Huyu anasema eti miaka ya 1970 ilikuwa inaliwa na watu maskini tena kwa usiri halafu ni chakula cha ng'ombe na sungura....unaamini hicho?

Mkuu Excellent, naomba unielewe kidogo. Nazungumzia marafiki zangu ambao nilikuwa nao miaka hiyo kwani mitaa ya kwetu kule Msasani ilikuwa ukila hii kitu watoto wenzako walikuwa hawakuelewi na wanaanza kukuonea huruma kwa kuwa kwenu mafukara, hivyo kutokana na kasumba hii mimi sijawahi kukipenda hiki chakula na hata nilipokuwa A level siku hiki chakula kikipikwa tulikuwa tunaambiwa kuwa hakuna hela za kutosha hivyo Mwalimu Nyerere kasema miezi 18 wananchi wote tufunge mikanda. Hiko ndicho kisingizio tulichokuwa tunapewa shuleni kwa kula makande kwani si chakula kinachopendwa na wengi japo kuna kabila linalikua hii pilau tena kwa maringo kabisa. Yaani ilikuwa ni sawa tu na kula chunga na ugali wa unga ulio oza toka Marekani kipindi kile. Yote haya tulikuwa tunakula A level kwa kisingizo cha miezi 18 wananchi wote tufunge mikanda. Man, I hate CCM na sera zake....tuliteseka jamani na bado tunazidi tu kuteseka tu chini ya utawala wa hawa manyau-nyau.
 
Hawa ni mateka wa kivita? Au ni makruta wa alshabaab?
attachment.php
Inasikitisha na ni kweli picha ina lugha nyingi. Naona hapa kuna wanaogombania pumba na wanaojisevia kupiga magoli nyuma ya wenzao. Naona kuwa wengine wana usongo kabisa wa kula na wengine wanajisukimizia midushelele yao nyuma ya wenzao tena kwa hisia kali.
 
Chakula kingine ambacho nakichukia ni dagaa wa Kigoma/Mwanza, yaani sielewi tu uzuri wake. Mtu badala ya kula na ku enjoy chakula unashinda kuvunja mawe mdomoni na kuharibu meno yako. Ndiyo maana wale dagaa wanaitwa misumari, ila ilibidi waitwe koleo ama nyundo.
 
Babu weeh!
Hujakutana na mpishi anaejua kuziswafi zikaswafika! Huoni wala kusikia mchanga hata tone. By the way dagaa wa kigoma na wa zanziba na wa nyasa hawanaga mchanga. Only wa mwanza. Dagaa is my fauvorite na nikipika utabloo
cc Donn mangi

wewe bwana uko kama kakangu mmoja. Eti hali smoked fish kama kambale na dagaa pia, kisa tu anawa-associate na umaskini. Hata akute kambale mkubwa, kaungwa na nazi na haijakatika tui, imechanganywa na bamia, viazi na nyanya chungu. Hagusi! Yuko kama mchawi yaani aagh!
Chakula kingine ambacho nakichukia ni dagaa wa Kigoma/Mwanza, yaani sielewi tu uzuri wake. Mtu badala ya kula na ku enjoy chakula unashinda kuvunja mawe mdomoni na kuharibu meno yako. Ndiyo maana wale dagaa wanaitwa misumari, ila ilibidi waitwe koleo ama nyundo.
 
Last edited by a moderator:
Wengine hawakaangi wanatia kitunguu swaumu tu na nazi. Mie napenda kukaanga nyanya na kitunguu kwanza, then naweka swaumu. Halafu kisamvu kinafuatiwa na tuibla kutosha ama karanga (peanut butter unakoroga na maji inakuwa kama tui).
Ukichemsha sana itashika chini, i mean kuungulia.
hapo sawa kabisa,mmh hivi kisamvu inakaangwaje?kama mboga zingine?
 
Babu weeh!
Hujakutana na mpishi anaejua kuziswafi zikaswafika! Huoni wala kusikia mchanga hata tone. By the way dagaa wa kigoma na wa zanziba na wa nyasa hawanaga mchanga. Only wa mwanza. Dagaa is my fauvorite na nikipika utabloo
cc Donn mangi

wewe bwana uko kama kakangu mmoja. Eti hali smoked fish kama kambale na dagaa pia, kisa tu anawa-associate na umaskini. Hata akute kambale mkubwa, kaungwa na nazi na haijakatika tui, imechanganywa na bamia, viazi na nyanya chungu. Hagusi! Yuko kama mchawi yaani aagh!

I lived in Kigoma for a while mpaka nikajua Kiha kidogo, dagaa wao kuna wenye mchanga na siwapendi hata kidogo. Unakula samaki hana hata nyama ni miba tu na mchanga what the hell si bora kula panzi au panya?
 
Mmh, inawezekana kuna wanaokuwa na mchanga. Ila sijakutana nao. Ngoja niombe ruhusa kwa Pa2 siku nikipika dagaa nikualike. Dagaa is delicious asikuambie mtu!
I lived in Kigoma for a while mpaka nikajua Kiha kidogo, dagaa wao kuna wenye mchanga na siwapendi hata kidogo. Unakula samaki hana hata nyama ni miba tu na mchanga what the hell si bora kula panzi au panya?
 
Back
Top Bottom