What is your favorite food?

What is your favorite food?

[Ni msosi gani ushawahi kula?msosi labda wa kabila lingine au taifa lingine?au msosi gani hutaweza kula?]

ME msukuma napenda sana ugari na mrenda + mtindi bla hvo kwa kweli ni napata shida kula ugali bila mtindi. tofauti na hiko cha kwetu napenda ugali wa mhogo na samaki mantura analiwa sana n'ghambo ya ziwa nyasa huko matema nk
 
Ni kweli uyasemayo, ila kula hiki chakula ni kuwanyima wanyama haki yao. Nakumbuka tulipokuwa shuleni miaka hiyo ya 70 mtu akila makande tunamkimbia kuwa amekula kinyesi (mavi ya kuharisha), na hata wenzetu wakila walikuwa hawasemi kuogopa kukimbiwa na marafiki zao.
Kwahiyo unamaanisha miaka ya 70 kushuka chini kande hailiwi?
 
[Ni msosi gani ushawahi kula?msosi labda wa kabila lingine au taifa lingine?au msosi gani hutaweza kula?]

ME msukuma napenda sana ugari na mrenda + mtindi bla hvo kwa kweli ni napata shida kula ugali bila mtindi. tofauti na hiko cha kwetu napenda ugali wa mhogo na samaki mantura analiwa sana n'ghambo ya ziwa nyasa huko matema nk
Mkuu ugali nadhani ni kila kabila sasa hivi,labda ambao hawawezi ni wale watoto wazazi wao mawaziri na wanakula hoteli...ila sema ukweli bhana raha ya msosi uwe na appetite,mfano mi naweza kula ugali na mboga yoyote
 
ugali

db_zambian-food-nshima-nsima-ugali-sadza05nyama1.jpg



Baba ujue nakudai kwa kunitamanisha,hapa nilipo nina miezi sita sijaiona hiyo menu......
 
Baba ujue nakudai kwa kunitamanisha,hapa nilipo nina miezi sita sijaiona hiyo menu......
Inaonekana huna access na bongo,acha hizo unga unauzwa bhana hata mi mwenyewe najipikia we unatafuta kwenye mahoteli ya huko nje?
 
Pilau miguu ya kuku hiyo kali ha ha unakula mpaka unajiramba ramba
 
Mimate imenijaa mdomoni... vyote nakula hapo
 
Kwahiyo unamaanisha miaka ya 70 kushuka chini kande hailiwi?

Inaliwa kwa wale wanaokula hiko chakula tena kwa siri siri, licha ya kukimbiwa na marafiki pia hiki chakula kilikuwa ni kwa ajili ya watu wasiojuwa kupika na mafukara.
 
[Mkuu ugali nadhani ni kila kabila sasa hivi,labda ambao hawawezi ni wale watoto wazazi wao mawaziri na wanakula hoteli...ila sema ukweli bhana raha ya msosi uwe na appetite,mfano mi naweza kula ugali na mboga yoyote]

HILO nalo neno? mana bila apetite hata upendacho waweza shindwa kula.
 
Dah mkuu ila kisamvu kura process mpaka utwangwe au kusagwa,ila sijui kikwenu mnapika mazima mazima?
Kisamvu ukipika kwa kukatakata hakiivi hata utie magadi lol. Kama uvivu weka kwenye blender low power. Kinatoka mwake. Usisahau kuweka karanga (mie natumia peanut butter tu kabisa)
 
Kisamvu ukipika kwa kukatakata hakiivi hata utie magadi lol. Kama uvivu weka kwenye blender low power. Kinatoka mwake. Usisahau kuweka karanga (mie natumia peanut butter tu kabisa)
sasa kwenye blender ndo unatoka uji kabisa??
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom