maramojatu
JF-Expert Member
- Mar 16, 2012
- 1,175
- 1,542
Habari ya jioni wanaJF,
Mimi kama mkazi wa DSM nimeona niweke hii thread hapa ili tuwe tunaishauri serikali jinsi ya kuboresha usafi wa mazingira tunayoishi. Ushauri serikali ifanye haya.
1. Kuongeza kodi maradufu kwenye nepi za watoto wanaoziita baby diapers... Hizi zimekuwa uchafu maeneo mengi. Kuna wakati mtu mmoja alijaza mfuko wa sulfate na kuniwekea kwenye eneo langu. Watu washauriwe kutumia nepi ambazo zilotimika miaka ya 1970.
2. Chupa za plastiki nyeusi zinazoweka vinywaji kama Azam kola sijui nini... Hizi waokota makopo hawaziokoti sijui haziwezi kuwa recycled au vipi. Kwa hiyo watumiaji na watengenezaji wa vinywaji hawa wanatakiwa waongezewe kodi au walazimishwe kuandaa utaratibu wa kuzikusanya na kuziteketeza kwa utaratibu unaofaa.
3. Serikali kurudisha utaratibu wa usafi wa mazingira siku ya jumamosi.
4. Mifuko laini la plastiki imerusi mitaani kwa utaratibu usiojulikana. Serikali ifuatilie hili na kuchukua hatua stahili.
Tafadhali ongezea maoni yako kwenye hili.
Usiku mwema
Mimi kama mkazi wa DSM nimeona niweke hii thread hapa ili tuwe tunaishauri serikali jinsi ya kuboresha usafi wa mazingira tunayoishi. Ushauri serikali ifanye haya.
1. Kuongeza kodi maradufu kwenye nepi za watoto wanaoziita baby diapers... Hizi zimekuwa uchafu maeneo mengi. Kuna wakati mtu mmoja alijaza mfuko wa sulfate na kuniwekea kwenye eneo langu. Watu washauriwe kutumia nepi ambazo zilotimika miaka ya 1970.
2. Chupa za plastiki nyeusi zinazoweka vinywaji kama Azam kola sijui nini... Hizi waokota makopo hawaziokoti sijui haziwezi kuwa recycled au vipi. Kwa hiyo watumiaji na watengenezaji wa vinywaji hawa wanatakiwa waongezewe kodi au walazimishwe kuandaa utaratibu wa kuzikusanya na kuziteketeza kwa utaratibu unaofaa.
3. Serikali kurudisha utaratibu wa usafi wa mazingira siku ya jumamosi.
4. Mifuko laini la plastiki imerusi mitaani kwa utaratibu usiojulikana. Serikali ifuatilie hili na kuchukua hatua stahili.
Tafadhali ongezea maoni yako kwenye hili.
Usiku mwema