Weka aya/ mstari kutoka kitabu cha dini yako unaoona umeandikwa kwa ustadi, weledi na hekima ya hali ya juu

Sasa umeambiwa uwaangamize waamaleki...Waamaleki wako wapi?
Kwani nimesema naangamiza watu ? kuna wakati mtu unapata feelings za ukatili ukiweka na hiyo aya unakuwa mzuka unapanda zaidi ya mvuta ganja akiwa anavuta.

Napenda kuuliza Waamaleki hawakuwa watu ? mpaka itoke amri kama hiyo pengine ni ya kikatili zaidi kuwahi kutokea kwani inajumulisha vichanga ,watoto ,wanawake mpaka wanyama
 
QURAN 78 An-nabai
31.Hakika wachamungu wanastahiki kufuzu
32.Mabustani na mizabibu
33.Na wake waliolingana nao
34.Na bilauri zilizojaa
35.Hawatasikia humo upuuzi wala uongo
 
Mbona unaruka maswali aya ya pili haujajibu swali ?

Kwa ajili gani huo mstari upo si watu wapate mafunzo kama hauna umuhimu si usingewepo ?

Tukianza kuzungumzia Alshabab ni mada pana nitaharibu mantiki ya uzi .Uzi umetaka vifungu vya vitabu vya dini mimi nimeweka kifungu katika bible lakini nashangaa unanivamia na kunihoji kama nimetoa kifungu katika Kitabu cha wahuni huku ukiwaacha wengine, sasa wewe mleta mada unampangia mtu kifungu cha kupost ?


Anyway ngoja nifocous na maudhui ya uzi nipost kifungu kingine.View attachment 2657979

Na hiki kifungu napenda vilevile kukisoma.View attachment 2657980
Thanks
 
Zaburi ya 20 yote..


Yoshua1:5

Hapatakuwa mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha
 
Back
Top Bottom