Website ya IKULU na miradi ya COMPUTER ya Serikali

Wakiweka website mnawachunguza sana, nondoz zao zote wanazoziweka mnazisoma kwa makini sana. Tangu Mwanakijiji awawashie moto Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, sidhani kama kuna wizara au idara ya serikali itakuwa inaanika nondo zake kwenye website yake, maana ni kama vile unajitakia kesi. Mtindo mpya wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ni kuweka percent za mikopo tu bila kuweka figures maana wameona ulaji wao unaweza kuyeyuka ivi ivi sababu ya uchunguzi wa akina Mwanakijiji!

Labda suala jingine la kujadili ni kuwa kwa nini tovuti nyingi za sirikali ziko kwa lugha ya kigeni? Je hii ni makusudi kuwanyima wasiojua lugha hii fursa ya kujua undani wa sirikali yao ama kuna agenda nyingine ya siri?
Naomba ufafanuzi tafadhali wana JF.
 
Jamaa wa University walishaomba kuingia huko lakini waungwana wakawatolea nje,pengine Mr.Mungi VPO amekomaa sana na hilo kwa ajili ya Dr.Shein.
Tatizo lingine ni hawa wakuu wa kurugenzi humo kwa wakubwa,longolongo tele ile ya Bunge sasa hivi ni mkono University ingawaje bado hawakupewa ushirikiano mkubwa
Wanabadilika ila kwa spidi ndogo sana,kuna watu wanaitwa MIS serikalini,wao ndio wanaonekana kuwa wataalamu kumbe ndio warasimu nambari wani,kinachoudhi ni vijana wadogo! Lakini ni user friendly kwa wahindi ,inasikitisha sana.
 
Tovuti ya JWTZ Yazinduliwa...

Kwa mara ya kwanza, jeshi la wananchi la Tanzania(JWTZ)
limezindua tovuti yake yenye lengo la kuongeza Ushirikiano
kati yao na wananchi.

Tovuti hiyo ni www.tpdf.go.tz iliyoznduliwa rasmi leo jijini
Dar es Salaam na Mnadhimu mkuu wa jeshi hilo,Luteni jenerali
abdulahaman Shimbo pichani, kwenye bwalo la maofisa wa jeshi hilo Upanga, Dar es salaam.

Luteni jenerali abdulahaman Shimbo alisema lengo la tovuti hiyo ni ukuaji wa sayansi na teknolojia hali inayofanya dunia kuwa kijiji kutokana na ukweli kwamba sekta ya mawasilianano kupanuka,

'' JWTZ lliona si vyema kuendelea kufunga funga mambo yetu na kuwa wapweke na tunaamini tovuti yetu ni endelevu, tunawaomba wananchi kutembelea tovuti hii na kutoa maoni yao kuhusu utendaji wetu na kutushauri. tupo tyari kuyapokea na kuyafanyia kazi yote mtajayotushauri kwa lengo la kuboresha jeshi jeshi,'' alisema Luteni Jenerali Simbo.unaweza kupata habari nyingi juu ya jeshi letu la JWTZ
kwa kutembelea WWW.TPDF.GO.TZ
 
Hakuna walichonifurahisha hawa wajeshi kama kuweka 'default page' katika lugha yetu ya taifa-kiswahili...ujumbe umeelekezwa kwa watanzania.

Ningefurahi zaidi kama sites zingine wangetumia lugha yetu; kwa mfano benki kuu na za biashara; na mashirika mengine.
 
Hakuna walichonifurahisha hawa wajeshi kama kuweka 'default page' katika lugha yetu ya taifa-kiswahili...ujumbe umeelekezwa kwa watanzania.

Ningefurahi zaidi kama sites zingine wangetumia lugha yetu; kwa mfano benki kuu na za biashara; na mashirika mengine.

Invisible,
Nilishwahi kuandika makala katika magazeti yetu ya Tanzania, kwamba, kwa nini tovuti nyingi za sirikali ziko kwa lugha isiyo ya taifa wakati walengwa wakuu wa taarifa husika ni Watanzania? Hakuna aliyejibu.
Haina maana kuweka taarifa ambazo walengwa wa kwanza ni wananchi wa Tanzania katika lugha ya kigeni. Huu ni ulimbukeni. Afadhalli hata ingekuwa kwa lugha mbili basi, Kiswahili na lugha ya kikoloni, lakini wao wamekomalia lugha ngeni tu. Kwa tovuti ya wizara ya utalii hili ni sawa, lakini kwa tovuti za wizara huu ni upotofu mkubwa.
Hili nalo tulijadili hapa JF tuangalie hatima yake, binafsi linanikera sana.
 
1884 – 1918.
Wjerumani Walianzisha jeshi waliwatumia Wanubi toka Sudani.



Hivi ni kwa nini Wajerumani walichukua askari Wanubi ktk jeshi? kwani sisi wazee wetu walikataa kumtumikia Mjeremani?
 
Cha kushanga wamezinduaje website ambayo haijakamilika? au wanadhani website maanake ni index page pekee [homepage]? Wanajeshi hawa lazima wauje website ni sawa na kitabu. huwezi ukazindua kitabu kava tu au chenye utangulizi pekee. sioni walikuwa na haraka za nini kuzindua kitu ambacho hakijakamilika.

Kama ilikuwa lazima wazindue kwa mda huo basi wasingeweka hizo link ambazo hazijakamilika. unajua inaboa sana unaona kuona kichwa cha habari halafu habari yenyewe haipo, kisingizio eti bado inaandaliwa. This is unprofessional

Watanzania lazima tujifunze kuacha utamaduni wa kukurupuka kufanya mambo. hii inaonesha ni jinsi gani tulivyo wasio makini.
 
Link zote kuanzia Muundo wa Jeshi hadi mwisho wangeziondoa hadi hapo zitakapokuwa tayari. kwa kweli hii kazi chafu kabisa sijawahi kiona. Huyu web designer sijui alikuwa anawaza nini kufanya kazi kama hii.
 
Naona ndio mambo ya e-government JK aliyotuambia mara tu baada ya kukwaa madaraka!!!!!!!!!
 
na juzi tuu walimpeleka mtu course London kusomea uendeshaji wa hiyo website,nimeamini aliyesema zimetengwa 500 kwa ajiri ya huu utumbo....sijui lini wataanza kufanya kazi na kuacha kugeuza kila kitu ni ulaji.
 
Huu sasa ni udaku kama siyo Umbeya.

Mnataka website ya ikulu ya nini?.

Kuna lipi hasa mnataka kulifahamu ambalo mtashindwa kulipata bila ya kuwepo kwa website hiyo?. Natoa hoja
 
Huu sasa ni udaku kama siyo Umbeya.

Mnataka website ya ikulu ya nini?.

Kuna lipi hasa mnataka kulifahamu ambalo mtashindwa kulipata bila ya kuwepo kwa website hiyo?. Natoa hoja

..kama hujui unachoongea bora kufunga hilo bakuri lako.
 
Huu sasa ni udaku kama siyo Umbeya.

Mnataka website ya ikulu ya nini?.

Kuna lipi hasa mnataka kulifahamu ambalo mtashindwa kulipata bila ya kuwepo kwa website hiyo?. Natoa hoja

Mtambo wa kuropoka nadhani ukikaa kima itakuwa busara zaidi. Kwa upeo wako watu hawatakiwi kuona site ya ikulu? okay mimi natafuta information kutoka state house nitumie source gani? Huoni kuwa ni busara kutumia hiyo site ya Ikulu kuliko Kikwete.com?

Ficha upumbavu wako onyesha hakima zako (Ivisible, 2006)
 
Nishasahau how many days zishapita lakini all i know kuwa wale waandishi wa Kimataifa watakao ongozana na Bush watataka kujua what weve been up ndipo salava ataanza kumungunyua maneno

Imagine researches wa Condi kule State wanavyopata taabu kutaka kujua some basic info lakini wapi

Membe hilo halitaki

 
Mheshimiwa naweza kukuambia kuwa mimi nimeweka kama vile hobby kujua what ikulu have been up to especially katika masuala haya ya kuconnect na wanajamiii

Hii siyo webiete ya IKULU na wala msimpe Salva any credit kwa hili kwani wao walichokifanya wamekuja FJ wameona jinsi tunavyowabebea bango kisha probably wakampigia simu bwana yule mwenye KIKWETESHEIN.COM sasa wakaamua kuchukua hiki kipande cha JAKAYA KIKWETE


Nimetazama hizi domain names naweza kukupa info ifuatayo:




Sasa lets move to hiyo the so called website ya IKULU


hapo hakuna kitu kwani ukienda kwenye hii webisite http://www.kikweteshein.com/tanzania/ utaona pembeni kuna chini kuli kuna hiyo THE STATE HOUSE sasa ukibonyeza hiyo itafunguka nini?



http://statehouse.go.tz/president/

sasa hawa huyu salva na wenzake waache kutuchezea akili zetu

kuna habari kuwa webiste ya maoni iligharimu dola laki tatu sasa sijui kama kuna ukweli kwenye hilo lakini msishangae wakijidai hii link hapo juu wameinunua kwa dola milioni moja
Game,
Nami najiunga katika ku-monitor maendeleo ya hizi websites, International media inazihitaji. Na wasithubutu kutuongopea kuhusiana na malipo au gharama za kuendeleza websites, tunayajua!!

SteveD.
 
Mheshimiwa naweza kukuambia kuwa mimi nimeweka kama vile hobby kujua what ikulu have been up to especially katika masuala haya ya kuconnect na wanajamiii

Hii siyo webiete ya IKULU na wala msimpe Salva any credit kwa hili kwani wao walichokifanya wamekuja FJ wameona jinsi tunavyowabebea bango kisha probably wakampigia simu bwana yule mwenye KIKWETESHEIN.COM sasa wakaamua kuchukua hiki kipande cha JAKAYA KIKWETE


Nimetazama hizi domain names naweza kukupa info ifuatayo:




Sasa lets move to hiyo the so called website ya IKULU


hapo hakuna kitu kwani ukienda kwenye hii webisite http://www.kikweteshein.com/tanzania/ utaona pembeni kuna chini kuli kuna hiyo THE STATE HOUSE sasa ukibonyeza hiyo itafunguka nini?



http://statehouse.go.tz/president/
GAME,
Kwa maoni yangu Whois info za website kama hizi za serikali hazitakiwi kuwa private. Kila mmoja akicheck inabidi aone ni nani registrant na kujua gharama za servers update na mengineyo. Mambo ya kutumia domain privacy katika website zinazohudumia wananchi kwa kweli sioni mantiki yake.

SteveD.
 
Nimecheki website ya IKULU kama wameweka taarifa za kuahirishwa kwa ziara ya rais wa Uturuki lakini wapi!!

haya endeleeni kumtetea SALVA
 
Back
Top Bottom