asakuta same[/B], hapo nilipobold naomba nieleweke kwamba siungi mkono hg kuingia chumbani kwa baba na mama, let alone kutandika kitanda! Hoja yangu ilikuwa kwamba napata mashaka hiyo ndoa anayoizungumzia mtoa mada imejengwa katika misingi gani, maana ikiwa mnatafuta msuluhishi kwa vitu kama kupika, kufua na kutandika kitanda itakuwaje kwa mambo mengine makubwa zaidi? Tena tatizo sio kwamba hizo kazi hazifanyiki bali tatizo ni kuwa zinafanywa na hg! Ndio maana nikasema kama unaoa ili ufuliwe, upikiwe na kutandikiwa kitanda basi hapo kuna tatizo kubwa sana.
Ni vema pia mume ujue kutandika kitanda maana sio kila siku mkeo atakuwepo nyumbani.
Nakupongeza kwa kuamua kutohoji maana kutaepusha mengi,
ila nikushauri ikikutokea mkeo hatandiki kitanda usimuulize bali mkiamka asubuhi mwambie ashike shuka upande ule na wewe shika upande mwingine mtandike kitanda. Ukifanya hivyo mara mbili tu naamini atajifunza na kutandika kitanda yeye mwenyewe, la kama kuna tatizo kubwa zaidi linalomsababisha amwachie hg hiyo kazi.
Binafsi napenda kumhudumia mume kadri niwezavyo but sometimes najiuliza nawezaje: mke ameajiriwa DSM, ana changamoto ya long work hours na foleni barabarani - akitoka kazini saa 11 basi huenda akafika home saa 1 usiku au late zaidi. Swali anapika saa ngapi?
Kikubwa anachoweza kufanya ni kuset standards na kuzisimamia kuhakikisha chakula mnachokula ni bora kwa afya zenu; akiwahi basi ni heri zaidi - maana atapika mwenyewe.
Suppose tuna washing machine na tumble drier, kuna ubaya gani tukiweka nguo kwenye laundry basket (sio nguo za ndani na hiyo basket inakaa laundry room) then hg afue? Hii ni katika kurahisisha kazi kwa mama.
Naelewa wapo wanaume hupenda kuona wake zao ndio wanawafanyia hivyo vyote lakini ni vema wakiwa understanding kulingana na mazingira na hali halisi. Ikiwa mama ni house wife, sioni sababu ya kushindwa kufanya hizi kazi za nyumbani.