We mwanamke inakuwaje unatandikiwa kitanda?

We mwanamke inakuwaje unatandikiwa kitanda?

nadhani hujasoma post zote toka mwanzo. Kuna mahali nimesema mke ni mlinzi wa mume wake na mume ni mlinzi wa mke wake. Kwa maana kwamba wote ni wadhaifu kwahiyo kila mmoja ana wajibu wa kumsaidia mwenzake kutokuwa exposed kwenye risk.
Tafdhali usikae pembeni kwakuwa mawazo yako ni muhimu sana katika mjadala huu. Wala usigune ndugu yangu sometimes we learn in hard ways.
huwa sipendi kabisa ku-buy story cjui risk, cjui madudu gani!! Ulishaamua kuoa/kuolewa! Period!!! No risk no rubbish, mambo mengine ni kujiendekeza na kujirahisi!! Nipo bosi wangu, ni mimi tu kukuletea habari za kuwakaribisha mahausgal kwa room, lol!
 
kwakuwa chumbani kwetu beki tatu haruhusiwi kuingia, mke wangu akiwa katika hali ambayo hawezi kufanya usafi wa chumba nafanya mimi mwenyewe. Na ukweli wa mambo ni kwamba ni kawaida ya mke wangu kufanya usafi wa chumba chetu na hata siku moja hajawahi kulalamikia hilo.
sasa hivi ana kichanga, hope unamsaidia, ujue mgongo hautamuuma sasa hivi, ila huko baadae yaweza kuwa issue!
 
Hahahaha sasa poti wale wazee na vijana wanaowagegeda mabeki tatu huwaoni ama hujawahi hata kuwasikia? Najua wewe hapo hotelini kwako kuko shwari, je na kwa hoteli ya jirani yako ambako beki tatu si sawa na mtoto wa nyumbani hupafikirii?


Hiyo ndiyo njia yako ya kumwaga apology Poti??

Kwa kweli suala la mtu kutembea na house girl ni uovu kama uovu mwingine......mithili ya ujambazi na ufisadi...

Na hao wanaofanya vitu kama hivyo haki yao ni Keko au Segerea (siyo pale kwa Poti lakini..lol)!!

Kwamba wapo ni sawa ila tunatakiwa kuwapiga vita kama tunavyopambana na mafisadi!

Babu DC!!
 
Kuna tofauti kubwa kati ya kuheshimu na kuabudu...,,..,,,.

Mimi simuabudu mwanaume, namuabudu MUNGU pekee aliyenipa uhai ,na akili timamu za kutambua baya na zuri.
Kila wakati wa kuolewa anapata mafundisho toka kwao. nafikiri mm ndivyo nilivyofundishwa kuwa niheshimu Ndoa na nisimuabudu Mwanaume, na nifanye majukumu yangu kama Mke na Housegirl afanye yake.
 
Kwakuwa chumbani kwetu beki tatu haruhusiwi kuingia, mke wangu akiwa katika hali ambayo hawezi kufanya usafi wa chumba nafanya mimi mwenyewe. Na ukweli wa mambo ni kwamba ni kawaida ya mke wangu kufanya usafi wa chumba chetu na hata siku moja hajawahi kulalamikia hilo.


Hongera sana Poti,

Ila sasa wale ambao tunashindwa kufanya huo usafi (for whatever reasons) tunatumia wasaidizi....

Kuna tofauti hapo Poti???

Babu DC!!
 
huwa sipendi kabisa ku-buy story cjui risk, cjui madudu gani!! Ulishaamua kuoa/kuolewa! Period!!! No risk no rubbish, mambo mengine ni kujiendekeza na kujirahisi!! Nipo bosi wangu, ni mimi tu kukuletea habari za kuwakaribisha mahausgal kwa room, lol!

Kweli eenh? kuna kamsemo fulani kwamba wanao-take risk ndio wanaofanikiwa huenda ndio siri yako ya mafanikio. Ila mimi binafsi siwezi kuruhusu mke wangu awe exposed kwenye mazingira yenye risk ya kumfanya auze mechi.

Ahsante kwa kunikumbusha hicho kisa cha Ayubu mtumishi wa Mungu.
 
MIMI PIA HUANIKA NJE, ILA NAFUNIKIA JUU KANGA YANGU NYEPESIIII AU MTANDIO!! na hata wakiingia kufanya usafi hawazioni, zipo bathroom kwangu, na usafi wa bathroom nafanya mwenyewe hiyo nilishindwa kumuachia hausgal! ila mausafi mengineeeeee ya chumbani lazma wafanye!


Kwa nini unazificha kiasi hicho??

Mie kwanza nakereka kuona chupi ambayo mtu kaivaa ila siyo chupi iliyoanikwa kwenye kamba...

Babu DC!!
 
sasa hivi ana kichanga, hope unamsaidia, ujue mgongo hautamuuma sasa hivi, ila huko baadae yaweza kuwa issue!

Sasa hivi ni kula, kunyonyesha mtoto na kulala tu. Tena ninamkanda mwenyewe maji ya moto!! Na usafi wa chumba nimeshika mwenyewe usukani.
 
Kweli eenh? kuna kamsemo fulani kwamba wanao-take risk ndio wanaofanikiwa huenda ndio siri yako ya mafanikio. Ila mimi binafsi siwezi kuruhusu mke wangu awe exposed kwenye mazingira yenye risk ya kumfanya auze mechi.

Ahsante kwa kunikumbusha hicho kisa cha Ayubu mtumishi wa Mungu.

Hahahahahahahahahahahah,

Ni wewe kweli Poti?? Ndiyo maana umesema mnalindana??

Mnatumia silaha gani kaka Mwita Maranya...??? May be na mimi nikanunulie li AK 47 limoja niliweke ndani kwa ajili ya ulinzi wa bibi...lol


Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
kwa nini unazificha kiasi hicho??

Mie kwanza nakereka kuona chupi ambayo mtu kaivaa ila siyo chupi iliyoanikwa kwenye kamba...

Babu dc!!
nimerudi na wakwe zangu, wapo kwangu kwa sasa, so naona si heshima wakiona za mtoto wao na mkwe wao! Ila wakisepa tu, ni mwendo wa kuziachia kama bendera ta taifa!
 
Mimi simuabudu mwanaume, namuabudu MUNGU pekee aliyenipa uhai ,na akili timamu za kutambua baya na zuri.
Kila wakati wa kuolewa anapata mafundisho toka kwao. nafikiri mm ndivyo nilivyofundishwa kuwa niheshimu Ndoa na nisimuabudu Mwanaume, na nifanye majukumu yangu kama Mke na Housegirl afanye yake.


Hongera sana Lisa,

Hivi umewahi kujiuliza ili kupata sababu kwa nini house girl haruhusiwi kukufanyia usafi chumbani??

Au umelichukua tu kamaa maandiko matakatifu?

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Hivi kumbe miongoni mwa vitu mnavyotaka kuficha ni chupi??

Mbona huko sokoni wanazitandaza chini??

Mie kwangu tunaanika chupi zote nje...wazazi wana sehemu yao, watoto wa kiume na wasichana pia zao....

Kwani chupi ni big deal kiasi hicho?? Na hizi zinazooneshwa nje nje mitaani kama mbao zao matangazo je?

Halafu, nyaraka za siri haziwezi kuwekwa mahali salama kama kwenye kabati ikafungwa??

I still don't buy this package..lol!!

Babu DC!!

ha ha ha ha ha! hata mimi boksa huwa naanika nje tu ,ila mwenzangu yeye ni chumbani au kwa bathroom.
 
Sasa hivi ni kula, kunyonyesha mtoto na kulala tu. Tena ninamkanda mwenyewe maji ya moto!! Na usafi wa chumba nimeshika mwenyewe usukani.


Pole na hongera sana kaka,

Count down imebakisa kama siku ngapi Poti??


Hapa sasa naweza kuelewa kwa nini unawaogopa mabeki tatu........!! Hawakawii kukupa ndovu ya moto au baridi..lol!!

Babu DC!!
 
kweli eenh? Kuna kamsemo fulani kwamba wanao-take risk ndio wanaofanikiwa huenda ndio siri yako ya mafanikio. Ila mimi binafsi siwezi kuruhusu mke wangu awe exposed kwenye mazingira yenye risk ya kumfanya auze mechi.

ahsante kwa kunikumbusha hicho kisa cha ayubu mtumishi wa mungu.
hakunaga mazingira wala nini, sitamtetea mtu hata siku moja!! Ni kujiendekeza na matabia ya mtu yalivyo! Nilikuwa nafanya research repoa, tulikuwa tunalala na guys waume za watu saa nyingine, lakini nilikuwa namake sure siweki mazingira yoyote ya ukaribu baina yangu na wao, tunalala kama mtu na mama yake au baba yake, kunakucha tunaingia porini kuoga, WADADA KWETU KWANZA, TUKIMALIZA WAKAKA NAO WANAKWENDA na kuvaa, na kuanza safari kijiji kingine faster, tena for months!! Ni mawatu huwa yanajiendekeza!!
 
ha ha ha ha ha! hata mimi boksa huwa naanika nje tu ,ila mwenzangu yeye ni chumbani au kwa bathroom.


Kwa hiyo chupi za mkeo anaanika gizani (au kwenye mwanga hafifu) ili kufuga fungi??

Kamwambie kuwa siyo salama kaka...lol!!

Chupi ni nguo kama nguo nyingine mkuu!!

Babu DC!!
 
Kwa hiyo chupi za mkeo anaanika gizani (au kwenye mwanga hafifu) ili kufuga fungi??

Kamwambie kuwa siyo salama kaka...lol!!

Chupi ni nguo kama nguo nyingine mkuu!!

Babu DC!!


Babu chumba kina mwanga wa kutosha tu na hata bathroom kuna mwanga vizuri na hewa ya kutosha kote tu kwahiyo haziwezi zikaotesha fungi.

hlf kwanini unadhani siyo salama Babu?
 
Babu chumba kina mwanga wa kutosha tu na hata bathroom kuna mwanga vizuri na hewa ya kutosha kote tu kwahiyo haziwezi zikaotesha fungi.

hlf kwanini unadhani siyo salama Babu?

Kama mnaishi maeneo yenye joto sana, nguo kama hizo hushambuliwa kirahisi na fungi endapo zinaanikwa sehemu zenye mwenga hafifu. Ila kama mwanga unatosha na hazikai muda mrefu kabla ya kukauka hakuna neno.

But...anaogopa nini kuanika nje endapo siyo kwenye nyumba ya kupanga yenye watu wengi?

Babu DC!!
 
Baadhi ya wanaume wanawaona wake zao kama robbot! kwani ukimsaidia kutandika hicho kitanda utakuwaje?
yani mwanaume anajifanya utadhani ni disable hawezi kumsaidia mkewe hata kazi ndogo kisa tu YEYE NI MWANAUME ptuuuu na uanaume wako huko!!!!!

Kwenye red inaonyesha huo wajibu ni wa mwanamke. Mwanaume anaweza kusaidia kama atapenda mwenyewe
 
Back
Top Bottom