Lipumba hajitambui. Yeye pamoja na elimu yake kubwa chama kimemfia mikononi. Alichukua chama kikiwa imara na kikiwa namba 2 baada ya ccm. Sasa ni kama hakipo. Viongozi wake wamebakia porojo kama hizi za kutathmini vyeti vya wenzao. Na wengine wameona bora wafanye kazi na ccm ili waishi. If u can't fight them join them. Nani alijua hili laweza kutendeka la cuf kushirikiana na ccm? Haya yote ni kwa kuwa prof. Ameshindwa kuongoza chama. Cuf kwisha kabisa. 2015 ndo kabisa hata wabunge 7 hawatawapata labda wawatoe pemba tu. Sasa basi nauliza elimu isio na matunda kwa mtanzania ina faida gani? Mbona mbowe elimu finyu lakini chama chake charuka juu kama ndege na kuifanya ccm iingie kiwewe? Ngoja 2015 kama hawataibiwa kura zao uone watavyoingia ikulu kilaini.