Lakini, hebu tujaribu kutenda haki katika kukosoa kwetu.
Ni haki kwa kila mmoja wetu kukosoa pale palipo na walakini.
Hivi, kwani kuongoza hiyo wizara waziri anatakiwa awe na sifa gani?
Kwanza unatakiwa uwe mchumi na mwenye shahada ya uchumi kutoka chuo kikuu ambapo ulikaa kwa miaka mitatu
Pili, uwe na uzoefu wa masuala ya uchumi na fedha kwa ujumla na mara nyingi unaanzia kazi Benki kuu au hazina moja kwa moja baada ya kupita usaili pale BOT au Hazina penyewe.
Na sifa zingine kama za kufahamu masuala ya ukaguzi wa ndani na nje na masuala yoote ya uchumi na fedha kwa ujumla.
Nne, mbunge wa kuchaguliwa na pia uwe mjumbe wa kamati mbalimbali za uchumi na fedha za bunge.
Hizo sifa zimeorodheshwa sehemu? Nani anazijua?
Sifa hizo zipo ofisi ya raisi na ni yeye ambae hupitia sifa hizo ingawa huweza kuziweka pembeni kutokana na maslahi fulanifulani. Sifa hizo zinaweza kuwa zipo sehemu zingine ambazo mhusika amewahi kufanya kazi na kuwa na rekodi kabisa ya performance yake, na ni rekodi hiyo ndio inayotakiwa mahali popote pale inapotokea unahitajika.
Na kabla hajawa waziri kamili huyu mama si alikuwa naibu waziri?
Ndio lakini jambo la kodi ya SIM card ni yeye aliekuwa na task ya kuhakikisha linapitishwa ili serikali ipate fedha za haraka haraka kutokana na kukosekana pesa ya kujiendesha, hivyo kuendelea kumwangamiza mwananchi wa kawaida na wachuuzi wa hizo SIM cards.
Sasa ina maana kwenye hiyo nafasi ya unaibu waziri hakupata uzoefu wowote?
Hakuwa na majukumu mengi zaidi ya kuandaa taarifa na kumsaidia alekuwa waziri marehemu Mgimwa ambae alikuwa ni nguli wa masuala ya uchumi na fedha na hata WB na IMF walimtambua.
Na kwani ili mtu awe mtendaji mzuri wa kazi ni lazima awe na mashahada yenye maherufi ya kutisha tisha?
Cha msingi ni shahada ya kwanza hasa ya uchumi, na iwe ya daraja la kwanza, pili uwe na shahada ya uzamili na mara nyingi pale Mlimani wanakuwa wanafahamu ni nani anafaa kwenda hazina. Kama una shahada za nje basi usaili wako utafanyiwa upembuzi yakinifu.
Na je, kuwa na mashahada lukuki ni sawa na utendaji bora?
Kama alivyosema mkuu Mchambuzi mara nyingi utendaji bora huingiliwa na siasa na matokeo yake ni kuharibu uchumi na kusababisha mifumuko ya bei na kupandd kwa gharama za maisha. Marehemu profesa kighoma malima alileta VAT na akaanzisha TRA ambayo tunaiona leo hii ni ishara ya kwamba aliona mbali kwamba ni lazima tuwe na chombo maalum cha kukusanya kodi.
Nae Profesa Simon Mbilinyi alikuja na masuala mbalimbali likiwemo la kodi kubwa kwa bia zinazotoka nje ya Afrika, ingawa kuna watu wakaja kuendeleza urafiki na wafanya biashara.
Wangapi wenye mishahada lukuki tena mikubwa mikubwa lakini utendaji wao ni mbovu?
Kwa serikali hii hao ni wengi na tumeona jinsi wanavyoboronga na kuendelea kuweka watu kwa visingizio vya usawa au mengine ni hatari.Mbona hata Kinana alisema kwamba kuna mawaziri mizigo humo?
Hiyo wizara si ilishawahi kuongozwa na profesa? Huyo profesa alifanya maajabu gani hapo wizarani?
Nimeeleza hapo juu
Na mawaziri wote (mpaka sasa) ambao wamewahi kuongoza hiyo wizara, wote walikuwa na mashahada mengi ya chuo kikuu?
Bila shaka, kuanzia Cleopa Msuya, Edwin Mtei, Kighoma Malima (marehemu) Simon Mbilinyi na Dr Mgimwa (marehemu) na wengine wenye ilm hasa ya uchumi na fedha au fwedha.