Kama kweli CCM wamefanya hivi basi CHADEMA inachukua nchi 2015. Kwa watu wanaojua political strategies hii ni distraction tosha ya kuwafanya CCM waache kutekeleza mambo yatakayowafanya 2015 wapige kampeni kifua mbele. Mtu ukiwa kwenye madaraka hutakiwi kujibu hoja kwa propaganda bali kwa kufanya mambo ya maendeleo, maana ukisema hali ya maisha si ngumu wakati wapiga kura wanaumia na maisha unaonekana upo out of touch. Na kitendo chochote cha kuiongelea CHADEMA ni kuipa umaarufu. Mtu kwenda au kutokwenda kwenye maandamano si kazi ya serikali hiyo ni kazi mwandamanaji mwenyewe kulingana na nafasi yake, Kusema maandamano haya ni kama ya Misri au Libya ni kuhamasisha watu waone kuwa huenda kweli kuwa kuna ukombozi unaweza patikana kwa kuandamana na hivyo kuhamasisha watu wengi zaidi.
CCM walitakiwa kukaa kimya kabisa na wasiongelee CHADEMA hata kidogo, wao wahamasishe maendeleo kwa kuanzisha miradi isiyo ya kifisadi ya kusaidia maeneo mbali mbali na siyo kuonesha hamaki ya kinachoanywa na CHADEMA. Hii inaonesha wazi kwa wananchi kuwa CCM na serikali yake wanaangalia masilahi yao zaidi ya yale ya nchi. Waache demokrasia ifanye kazi, kama wanaogopa watangaze kufuta vyama vingi na kuendesha nchi kidikteta