Waziri wa Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto Mh.Sophia Simba amejikuta kwny wakati mgumu pale alipowalaumu vikali CHADEMA kwa kuendesha maandamano kanda ya ziwa na kusema kua huko ni kuiga Misri na Libya!! Mama huyo badala ya kuzungumzia kilichompeleka studio kuzungumzia Siku ya wanawake duniani yeye akaanza na kusema wanawake wasiende kwny maandamano ya CDM maana wao wana kazi nyingi za kufanya kuliko wanaume ambao hawana kazi ndio maana wanaenda kwny maandamano hayo!!! Ulipofika muda wa watazamaji kuchangia ndipo huyo mama alipoanza kushambuliwa na kila mchangiaji kwamba afute kauli zake za kwamba "wanaume hawana kazi ndio maana wengi wanaenda kwny maandamano hayo" na "kufananisha maandamano ya CHADEMA na yale ya nchini Misri au Libya" Ninachojiuliza hapa wana JF wenzangu hivi hawa viongozi wetu kwann wanakua mambumbumbu kiasi hiki na ufinyu wa uelewa? Kuhusisha maandamano ya CDM na yale ya Misri au Libya huu si ndio uchochezi wenyewe!!! Halafu napenda kuuliza wana JF wenzangu nini maana ya JINSIA?! Nawakilishaa.
Labda nikuulize swali mtoa bandiko hapo juu.
Kuna tofauti gani kati ya maandamano ya Misri yaliyoasisiwa na Muslim Brotherhood na haya ya Tanzania yanayoasisiwa na Chadema?
naomba majibu tafadhali kama kweli umefuatilia habari za kimataifa na si kukurupuka.