Waziri Ndumbaro kama kweli wewe ni Mzalendo, kataza Nguo za Rais Samia uwanjani, amuru mabango ya kumtukuza Rais Samia na CCM yasikanyage uwanjani

Heparin

Senior Member
Sep 24, 2021
127
420
Waziri Ndumbaro ni msomi mkubwa wa Sheria, walau kwa kurejea historia ya elimu yake bila kujali uhalisia wa mambo anayofanya.

Kwamba Waziri Ndumbaro hajui kuwa FIFA hairuhusu serikali kuingilia masuala ya mpira wa miguu? na tangu lini uzalendo unalazimishwa? Ni kukosa ubunifu wa kuendeleza michezo nchini, au ni kiburi kinachokuzwa na tabia za wanasiasa kutoa matamko pasipo kujali sheria za nchi?

Binafsi nimeshangaa sana kuona anapiga marufuku mashabiki kuvaa jezi za timu pinzani zinazotoka nje ya Tanzania kwa hoja mufilisi za uzalendo na kwamba wanaovaa watatakiwa kuwa na passport za nchi hizo pamoja na watakaokaidi watashughulikiwa na Polisi.

Tangu lini uzalendo ukalazimishwa? kwa sheria gani?

Kwa maarifa yangu madogo ya Civics ya Form 2, Uzalendo wa mtu ni kuipenda nchi yake, siyo kupenda Chama wala Serikali. Waziri haoni kuwa kuvalisha watu tisheti za Samia na kuweka mabango ya Serikali na mama anaupiga mwingi uwanjani inakwaza watu wengine wasioipenda CCM? Nani alisema uzalendo ni kupenda mambo yanayoifurahisha CCM na Serikali pekee?

Nataka nimwambie Ndumbaro, kama kweli yeye ni mzalendo apige kwanza marufuku tabia hii. Hapo kweli atakuwa amekunywa maji ya bendera ya uzalendo wa Tanzania.

Lakini anapaswa kutambua kuwa hana uwezo wowote wa kufanya anachokipanga, pia Simba na Yanga ni kubwa kuliko yeye, na asipokuwa makini zitamng'oa kwenye uwaziri wake.

Pia soma: Mambo haya ndio yanaidharaulisha Nchi yetu hadi kuonekana imekufa
 
Viongozi wasioelewa maana ya uzalendo wanashida sana.
Yeye hapo anajiona ameshakua mzalendo.
Kama nimzalendo mbona husemi upunguziwe mshahara na marupurupu yako? Mbona hamtaki makocha wazawa? Uzalendo sio lelemama.
Mtu utampangiaje timu ya kushabikia?
 
Uzalendo kwenye vilabu sidhani kama ni busara sana kuulazimisha, ikumbukwe hivyo vilabu hata wimbo wa taifa havipigiwi. Kwa minajili hii sasa itafika wakati wachezaji wakitanzania wakiwa wanatumikia vilabu vya nje siku timu zao zikija kucheza na Simba au Yanga tutawaambia wasivae jezi za timu zao kwa ajili ya uzalendo la sivyo waoneshe pasport. Ladha ya Simba na Yanga ndio huo utanani, kuzidoana na kufitiniana na kusimangana. Wakiendelea kuweka haya makatazo yao ipo siku hizi timu zitabaki kama mtibwa na majimaji.
 
Waziri Ndumbaro ni msomi mkubwa wa Sheria, walau kwa kurejea historia ya elimu yake bila kujali uhalisia wa mambo anayofanya.

Kwamba Waziri Ndumbaro hajui kuwa FIFA hairuhusu serikali kuingilia masuala ya mpira wa miguu? na tangu lini uzalendo unalazimishwa? Ni kukosa ubunifu wa kuendeleza michezo nchini, au ni kiburi kinachokuzwa na tabia za wanasiasa kutoa matamko pasipo kujali sheria za nchi?

Binafsi nimeshangaa sana kuona anapiga marufuku mashabiki kuvaa jezi za timu pinzani zinazotoka nje ya Tanzania kwa hoja mufilisi za uzalendo na kwamba wanaovaa watatakiwa kuwa na passport za nchi hizo pamoja na watakaokaidi watashughulikiwa na Polisi.

Tangu lini uzalendo ukalazimishwa? kwa sheria gani?

Kwa maarifa yangu madogo ya Civics ya Form 2, Uzalendo wa mtu ni kuipenda nchi yake, siyo kupenda Chama wala Serikali. Waziri haoni kuwa kuvalisha watu tisheti za Samia na kuweka mabango ya Serikali na mama anaupiga mwingi uwanjani inakwaza watu wengine wasioipenda CCM? Nani alisema uzalendo ni kupenda mambo yanayoifurahisha CCM na Serikali pekee?

Nataka nimwambie Ndumbaro, kama kweli yeye ni mzalendo apige kwanza marufuku tabia hii. Hapo kweli atakuwa amekunywa maji ya bendera ya uzalendo wa Tanzania.

Lakini anapaswa kutambua kuwa hana uwezo wowote wa kufanya anachokipanga, pia Simba na Yanga ni kubwa kuliko yeye, na asipokuwa makini zitamng'oa kwenye uwaziri wake.
imeshaamuliwa vibaraka wote mje na passport 🐒

kuvaa gwanda la chanema, udp au chauma rukhsa 🐒

kuvaa jezi ya Kagera Suger, mtibwa au JKT Tanzania, Rukhsa 🐒

Tatizo ni vibaraka tu hao ndio watakaoshughulikiwa, usipotoshe.
Uzalendrooo ni pamoja na kupenda na kuheshimu viongozi hususani wa kitaifa 🐒
 
Kwa hiyo Yanga mnataka kuachiwa ule upuuzi wa kupokea uwanja wa ndege timu za wageni,kununua jezi na kuvaa jezi zao,kuwashangilia,kuwapa mbinu za kufungwa timu za nyumbani?

Ni ujinga ambayo hata hao wageni walituona wajinga! Utani wa Simba na Yanga haukuanza Leo na hakuwa na matukio ya kijinga huko nyuma. Haya Sasa mna stoo za jezi nyingi za Mamelody Sundown mmenunua eti kwa sababu zinafanana na za kwenu, mkanunua jezi za TP mazembe, Kaizer Chiefs pia mnazo zinawasaidia nini?
 
Viongozi wasioelewa maana ya uzalendo wanashida sana.
Yeye hapo anajiona ameshakua mzalendo.
Kama nimzalendo mbona husemi upunguziwe mshahara na marupurupu yako? Mbona hamtaki makocha wazawa? Uzalendo sio lelemama.
Mtu utampangiaje timu ya kushabikia?
Apunguziwe mshahara?
Wakati na umri ule ukimwambia leo ajiajiri,utaona atakavyo mwaga machozi,kumlilia kizmkazi,asimnyime ugali🤣🤣🤣
 
Kagushi wapi nyie watanzania kwa kuwa mmezoea vitu vya kugushi mnadhani kila mtu kagushi.huo ni ujinga uliopitiliza.
 
Back
Top Bottom