Waziri Nchimbi hakuvamia kwa bahati mbaya maandamano ya waandishi wa habari leo Jangwani

Usipime!Muro alikuwa na pingu na kanunua duka la jeshi,jee unauhakika Duka hilo haliuzi mabomu ya machozi? Hii ni TZ bana
Hapa simaanishi kuwa waandishi walikuwa nayo ila namaanishi nchi haina taratibu za kueleweka
 
Nimesikitishwa na kauli ya Dr.Emanuel Nchimbi aliyoitoa leo Jangwani ya kutaka Jeshi la polisi likutane na Waandishi wa habari kumaliza tofauiti iliyopo baada ya jeshi hilo kumuua mwandishi wa chanel ten Daudi Mwangosi mbele ya kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda.

Nasema hoja hii ni dhaifu.Na kama waandishi wakikubali hoja hii watadharauliwa sana.Ushauri wangu, Ili mazungumzo hayo yawezekufanyika ni lazima kuwepo kwanza uwajibikaji kwa viongozi wa juu wa jeshi hilo akiwemo Kamuhanda.Tofauti na hapo mtaendelea kuuawa.

Alisema haya muda gani wakati alitimuliwa pale jangwani? Alisema akiondoka au?
 
Mimi ninaelekeza hasira zangu kwa KIKWETE.

Yeye ndiye anayeteua wasaidizi wake, na haiyumkiniki kuna majukumu maalumu anawaagiza, ukichukulia kwamba mawaziri wengi ni makada wa CCM basi wanahusika direct and indirectly na mauaji yaliyotokea. Lawama zangu kwa Vasco ni kuwa since upuuzi wa polisi umeanza kitambo sijasikia akitoa kauli kukemea au hata kuona chembe ya hatua aliyoichukua dhidi ya wahusika wanaonyofoa roho za raia...

Nchimbi ni dagaa ila sangara mnamkwepa kumwambia awajibike
 
PhD ya kwanza ni fake,lakini ndiyo mfumo huooo,tusitoke kwenye lengo.TANZANIA bila CCM inawezekana mwaka 2015
 
Usipime!Muro alikuwa na pingu na kanunua duka la jeshi,jee unauhakika Duka hilo haliuzi mabomu ya machozi? Hii ni TZ bana

hapana,pingu huuzwa kwa mtu yeyeto,hakuna mashariti.

Kitu hiki wengi hatujui.nilishawahi kwenda pale na zinauzwa 25,000 only,unless zimepanda last month.
 
Mie mwenyewe nilidhani mabadiliko ya kanunu CCM yalikuwa na lengo la kukiboresha chama...kumbe ilikuwa na janja ya wanamtandao ili wawapitishe nndugu na wanamtandao kirahisi bila challenge ili waingie CCM-NEC.

Kivuli kilikua eti wanataka kuwabana mafisadi, usanii mtupu uchaguzi unaoendelewa shv CCM ndio nimegundua ilikuwa danganya toto ni njia ya kujaza mtandao kwenye vyombo vya maamuzi CCm ili watawale wanamtandao tuu...kazi ipo sijui niende chama gani CDM kuna kanafiki kakijana kamoja kananifanya nisiende lbd wakatimue...nikifikiria ADC ndio chama kipya na kizuri lkn nasikia kuna libaba nafiki moja lipo nyuma ya pazia la ADc sijui niende TLP ...mh lkn napo kula yule jemedari anayefanya siasa kisanii na mie wasanii mbalimbali lbd mnisaidie niende wapi
Mkuu anzisha cha kwako!!!!
 
Mimi ninaelekeza hasira zangu kwa KIKWETE.

Yeye ndiye anayeteua wasaidizi wake, na haiyumkiniki kuna majukumu maalumu anawaagiza, ukichukulia kwamba mawaziri wengi ni makada wa CCM basi wanahusika direct and indirectly na mauaji yaliyotokea. Lawama zangu kwa Vasco ni kuwa since upuuzi wa polisi umeanza kitambo sijasikia akitoa kauli kukemea au hata kuona chembe ya hatua aliyoichukua dhidi ya wahusika wanaonyofoa roho za raia...

Nchimbi ni dagaa ila sangara mnamkwepa kumwambia awajibike
halafu la kombe lilikuwa utetezi dhaifu. Eti walimfananisha na jambazi, kudadadeki na jinsi tulivyo wawili wawili watatumaliza tubaki mmoja mmoja au tuishe kabisa. Wakutane nao wawaombe msamaha au..?! Mbona hawakuomba mkutano vilipotokea vifo vingine vya polisi kuua?
 
Mie mwenyewe nilidhani mabadiliko ya kanunu CCM yalikuwa na lengo la kukiboresha chama...kumbe ilikuwa na janja ya wanamtandao ili wawapitishe nndugu na wanamtandao kirahisi bila challenge ili waingie CCM-NEC.

Kivuli kilikua eti wanataka kuwabana mafisadi, usanii mtupu uchaguzi unaoendelewa shv CCM ndio nimegundua ilikuwa danganya toto ni njia ya kujaza mtandao kwenye vyombo vya maamuzi CCm ili watawale wanamtandao tuu...kazi ipo sijui niende chama gani CDM kuna kanafiki kakijan
 
usalama wenu ninyi raia wa Tanganyika na Zenjibara mnaofikia milioni 60/50 pamoja na mali mlizo nazo ziko chini ya DHAMANA YA VIONGOZI Mheshimiwa Dkt. William Nchimbi(mb) na IGP Saidi Mwema -mzee wa intelligensia na Ulinzi shirikishi.Polisi wenyewe wanaiishi huku uswazi na watuhumiwa wa uhalifuni binamu,kaka,mate,port,na mtoto wa mwenye nyumba.Hawa ukimtaja mtuhumiwa wanakufichua na viongozi wao wanataka wewe raia upeleke ushahidi wote kuhusu uhalifu husika.Kwa hapo si ajabu watu wakaanza kujilinda kwa kuchanjwa na waganga feki pia maana mfumo ushakuwa muflisi kwenye uzalendo ,mfumo uliopo ni wa kulinda wale waitwao viongozi waandamizi wa serikali.
Sasa huko Songea mjini wana wa Lizombe Mwaka 2015 fanyeni kile walichofanya Nyamagana halafu historia itakapoandikwa ninyimtakuwa mashujaa wa kweli wa mageuzi,mtandao or no mtandao muhakikishe M4C inashinda,watu wanashinda na mafisadi wabakie wakijifia wenyewe kwa KIHORO-STRESS!
 
Hivi ukikaa meza moja na mtu anayetaka kukuuwa utamwambia nini? Tafadhali usiniuuwe?

Daudi Mwangosi amekufa mikononi mwa polisi, tena RPC akiwepo, leo hii waandishi wa habari wataongea nini na polisi?

Last time I checked Tanzania ilikuwa na katiba!
 
Huyu hapa akisepa

427870_413390608723016_1858638376_n.jpg

Huyo mama aliengozana naye ni nani tena? au ndo uzinzi kama wa mwigulu?
 
Yaani kavaa kofia kama vile amejitwisha mzigo fulani hivi, yaani we acha tu!!
 
Likiletwa fungu la mpunga waandishi mtakataaa zile bahasha zetu zileeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!

MKUU umenikuna: waandishi wanasumbuliwa na unafiki, unafiki, unafiki ... unafiki kwa kwenda mbele. MIMI namlilia sana MWANGOSI kama BINADAMU lakini siyo kama mwandishi wa habari. WAANDISHI wangekuwa hawapokei bahasha na kupindisha ukweli, polisi isingetufikisha hapa: KUUWA WATU BILA SABABU, KINYUME NA SHERIA. KWA muda mrefu sana sasa polisi wamekuwa wakiuwa watu, na kuwatumia wanahabari kuficha ukweli. POLISI WANAUA kila siku ya MUNGU hapa nchini, lakini ni mwandishi gani, kwa mfano amewahi kuuliza polisi maswali haya: (1) je, huyu 'jambazi' mliyemuua mnayesema ni sugu, record za ujambazi wake ziko wapi? kafanya wapi ujambazi? alikuwa anatafutwa kwa muda mrefu, tangu lini? kwa kosa gani? (2) je, ni polisi au ni mahakama yenye mamlaka ya kumtangaza mtu kuwa ni jambazi? (3) je, bunduki na bastola mnazosema mmenyang'anya majambazi na mmetuonesha wenye nazo wako wapi? watafikishwa lini mahakamani? (4) je, jambazi hukamatwa au huuwawa? (5) je, ni sheria gani inayoruhusu kuuwa jambazi? kifungu gani cha sheria? nk

MIMI naamini, kwa kuwa waandishi kwa muda mrefu wametumiwa na dola kuficha ukweli wa mambo, basi HAWANA HAKI ya kulalamika na kutuomba tuwaunge mkono wakati huu baada ya mwenzao kuuwawa: HAWANA HAKI KABISAAAAAA. TUSIWAUNGE mkono kwani, ndg zetu walipokufa kwa risasi za polisi, waandishi walitumiwa kuhakikisha kwa vibahasha mayowe yetu hayasikiki zaidi ya VIBANDA VYETU vya nyasi ... NASIKITIKA KUSEMA KUWA kama ingewezekana kumuua mwandishi NYAMKANG'ILI lakini binadamu NYAMKANG'ILI akabaki; basi ningependa polisi iuwe waaaaaaaaaaandishi wengi zaidi, labda hili litasababisha waandishi kuachana na bahasha na kutusaidia kupiga vita maovu: UFISADI, MAUAJI YA POLISI, WIZI, MIKATABA MIBOVU, SIASA ZA VISASI, BUNGE LISILO MAAAAAAAANA, MAHAKAMA ILIYOJAA MAJAJI VIHIYO, MAWAZIRI WENYE PHD ZA KUFOJI, SERIKALI YA WIZI MTUPU ...
 
Huyo mama aliengozana naye ni nani tena? au ndo uzinzi kama wa mwigulu?[/

Nilishawahi korofishana na huyo mama, i didn't care to ask her name but she said kuwa yeye ni mwandishi/activist and anaweza nishtaki, nikamwambia go ahead. Kisa alikuta takataka getini kwake and she was claiming housegirl wetu ndio katupa nikajitahidi kwa ustaarabu kumwambia kuwa huwa hatutupi taka ovyo na jana yake tu watu wa taka walikusanya taka zetu, she kept insisting kuwa she is sure kuwa ni sisi na ushahidi mkuu ni kuwa aina za taka zilizotupwa ambazo ni mabox ya juice na makaratasi ya subway sisi pekee ndio wenye uwezo ya kununua vitu hivyo hapo mtaani.......alinikasirisha nikamweleza she can just go ahead with her activism na kuni sue but we are not going to remove mataka. Later on i found out she was going from door to door na kuwasemea mbovu watu like she did to me..........nilijishangalia if she is ok upstairs
 
Back
Top Bottom