mitindo huru
JF-Expert Member
- Apr 26, 2016
- 1,607
- 1,596
Tumefatilia sana mdau, Tatizo ni kwamba huyo masawe anatumia sana Polisi kutisha wananchi wanapotaka kuchonga hiyo barabara, pia anatumia baadhi ya watu Idara ya ardhi ofisi ya Halmashauri Wilaya ya Ilala kupotosha hilo jambo ili hiyo barabara ionekane haina maana kwa wananchi.Kama pamepimwa na kweli barabara ipo.. sioni kwanini mnamchekea... Kama unauthibitisho kuwa barabara hiyo wananchi wa ubavuni mwake wamepima.. na kama ipo inayokatisha katikati ya shamba na ilikuwepo kabla yeye hajamailikishwa hilo ni swala la wazi na lazima waliomilikisha na kumpimia na yeye mwenyewe wawajibike.. na ikibidi mnamdai fidia ya kuwanyima haki ya kupita kwa kipindi hiki chote... Mnaogopa cheo kwenye mambo straight forward!?
Pia huyo masawe anataka kuweka zuio mahakamani kutaka kuzuia hiyo barabara isichongwe na anafanya makusudi kutaka kuweka zuio ili akamilishe mipango yake ya kuuza hilo eneo.
Hilo eneo ni zaidi ya ekari tano lipo katikati ya Makazi ya watu eneo la Kinyerezi pia ni pori kubwa ambalo uhalifu unafanyika usiku wananchi wanaporwa vitu vyao, wezi wanajificha. Imefika hatua wezi wanaiba mifugo maeneo mengine halafu wanakuja kuchinjia kwenye hilo eneo, wananchi tunakuta kwato, vichwa na ngozi za mifugo asubuhi.
Ndio maana tunaomba serikali kuu kupitia Wizara ya Ardhi watusaidie kupata hiyo barabara sababu wananchi hatuna barabara ya kupita pia wamshauri huyo masawe aendeleze hilo eneo ili kuepusha uhalifu katika hilo eneo sababu sasa ni zaidi ya miaka 15 tangu ameanza kulimiliki hilo eneo huyo masawe.
Tunaomba Mh Waziri Lukuvi pia Mh Rais Magufuli waweze kutusaidia katika hili jambo sababu baadhi ya watendaji kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Ilala sio waaminifu kwa kua wanamsaidia huyo masawe.