Waziri Lawrence Masha hana uwezo

Wako wapi akina FMES na Kadampinzani jamani??
Mbona watu wanasema ukweli kuhusu masha na hawa jamaa hawaweki lao neno? Unataka kuniambia hawajaiona hii thread au?
Nimeuliza hivi kwa sababu walimtetea sana huyu masha siku za karibuni, wakidai the Guy is smart kwa sababu ni msomi, na vingine walivyovieleza wao
sasa leo wako wapi??
Mteteeni tena leo

Achana na ES ana kamtandao kake na yeye hutetea mrija wake then anajifanya mtetezi wa Taifa hana lolote msomeni vyema mtagundua na kama mmesha gundua basi mwangakieni kwa makini.Ukimgusa alipo na maslahi ata spin hadi anazeeka lakini sasa hoja imemshinda hii na kijana wake smart aliyekuwa anamtukuza .
 
sio kweli wasomi wanaifagilia ccm sana tu na angalia ni jinsi gani ccm ilivyojikita vyuoni

Unajua miaka ya 80 kurudi nyuma watu walikuwa wanajiunga na ccm ili kuweza kuwa na opportunities za mbeleni. Hivyo kwa kuwa mtu akitaka kuwa fisadi anaona ni budi ajiunge Chama Chawala ili aanze kujifunza kuongea na kutenda kama wao.....
 
Unajua miaka ya 80 kurudi nyuma watu walikuwa wanajiunga na ccm ili kuweza kuwa na opportunities za mbeleni. Hivyo kwa kuwa mtu akitaka kuwa fisadi anaona ni budi ajiunge Chama Chawala ili aanze kujifunza kuongea na kutenda kama wao.....

Umesema na kweli tu sina la kuongezea hapa .
 
Lunyungu,

Ulipotelea wapi? Hivi ina maana mtu hawezi kuwa CCM na asiwe fisadi?

Mtanzania mimi niko Comoro sasa .Kuna wachache sana kama wewe mzee wanaweza kuwa CCM na si Fisadi maana nakujua .Lakini walio wengi CCM ni njia ya kuelekea kwenye Neema bila ya wao kutokwa jasho .
 
In shot, aliyemzomea Masha na yule aliyemshangia Zitto, wote wana matatizo... Mpaka sasa sioni sababu ya Masha kuzomewa, wala sababu ya Zitto Kushangiliwa.
 
Wewe amka, amka, amka haraka. Hivi hujui tu yaliyotokea kiteto? Walahi watakucheka watu!!!!!

Huyu ana mawazo ya Kijinga .He is anti Zitto na Chadema hujamwelewa tu ?Yuko kazini mwenzio yeye kaja hapa kuipinga Chadema , Zitto na Mbowe ana siku kadhaa sasa .
 
Huyu ana mawazo ya Kijinga .He is anti Zitto na Chadema hujamwelewa tu ?Yuko kazini mwenzio yeye kaja hapa kuipinga Chadema , Zitto na Mbowe ana siku kadhaa sasa .

anapaswa kutambua kuwa ukibaraka wake unamfanya asiwe huru. hata kama anapendwa kutumwa, ni vema akubali kufanya yale ambayo watu wengi wanayaamini, atakuja kujikuta pabaya bila kujijua, maji ya mto hayapimwi kwa kijiti
 
Hussein Abdallah Re: Waziri Masha Azomewa Nyumbani Mwanza; Zito Ashangiliwa

Quote: BabaH
Wako wapi akina FMES na Kadampinzani jamani??
Mbona watu wanasema ukweli kuhusu masha na hawa jamaa hawaweki lao neno? Unataka kuniambia hawajaiona hii thread au?
Nimeuliza hivi kwa sababu walimtetea sana huyu masha siku za karibuni, wakidai the Guy is smart kwa sababu ni msomi, na vingine walivyovieleza wao
sasa leo wako wapi??
Mteteeni tena leo

Achana na ES ana kamtandao kake na yeye hutetea mrija wake then anajifanya mtetezi wa Taifa hana lolote msomeni vyema mtagundua na kama mmesha gundua basi mwangakieni kwa makini.Ukimgusa alipo na maslahi ata spin hadi anazeeka lakini sasa hoja imemshinda hii na kijana wake smart aliyekuwa anamtukuza .

1. Hii nilikuwa sijaiona, okay, wakuu kuzomewa kwenye siasa sio kuondoa u-smart wa kiongozi, kwa sababu kuna sababu nyingi zinazoweza kushinikiza kuzomewa,

(a). kwa mfano Mwalimu Nyerere(RIP), alishawahi kuzomewa kule OAU Adis, kwenye kikao cha viongozi wake in 60s, kuhusiana na suala la vikwazo vya uchumi kwa makaburu na walowezi wa Zimbabwe,
hiki kitendo kilikuwa engeneered by Nkurumah, ambaye alikuwa najaribu kumpunguza nguvu Mwalimu, kutokana na tamaa zake za kutaka kuwa rais wa kwanza wa US Of Afrika, suala ambalo lilikuwa linajadiliwa sana, walimzomea kwa kudai kuwa anashirikiana na makaburu, baada ya kutoa hotuba nzito sana, sasa kwa argument yenu ina maana Mwalimu hakuwa smart, au aliupoteza u-smart baada ya kuzomewa, tena na marais wenziwe?

(b). Kuzomewa kwa Masha, kwenye huu mkutano ilikuwa ni mis-calculation ya Masha, kisiasa, kwa sababu alipaswa kuelewa kabla ya kwenda kwenye huu mkutano what time is, yaanai baada ya the mess ya kumtetea Ridhiwani, unaenda kwenye mkutano, tena ukumbi mmmoja na Zitto, that was a big time political mis-calculation, lakini pia sio ajabu ndio hasa maana kuwa rookie, sijui kuhusu the context kwa sababu sijaisoma yote, lakini kitendo cha kwenda pale kwenye mkutano hakikuwa thought very careful, lakini haimupunguziii anything, zaidi tu ya kumtaka awe careful in the future, kwa sababu no matter what asingeweza kuondoka pale bila kuzomewa, the political wisdom ilikuwa ni kumtuma waziri wake mdogo kumsomea paper kwa niaba yake.

2. Kuhusu la pili Mkuu mimi ni mtu ninaheshimika sana kuanzia hapa JF, mpaka nje ya hii forum, sasa jaribu kuwa muangalifu na maneno unayoyarusha on me kwa sababu huna ushahidi wa unayoyasema. I am not sorry kwamba wewe huna marafiki wanaofahamika ili uwatete kwenye ukweli hapa JF, na wala sio tatizo mimi kuwa nao, maaaana I am what I am and you are what you are, hapa tunakutanisha ideas zetu tu, lakini hunijui wala sikujui, isipokuwa ninajua majina yako yote hapa JF, if anything ninakuheshimu sana kwa ernegy, I mean how do you do it?

Maaana you have a name kila kona hapa forum, jina moja wewe ni CCM damu, lingine wewe ni Chadema damu, lingine wewe ni expert kwenye Obama thread, I mean man you are all over, halafu you know kwamba ninajua hilo na majina yako yote lakini husikii aibu WHY?

Unasema habari za kamtandao exactly unaongelea nini? Kwa nini unataka kunilaumu mimi kwa matatizo yako ya kutokuwa na marafiki ambao huwezi kuwa-claim hapa JF? Masilahi gani unayoyasema hayo ambayo Masha anaweza kunipa mimi? Ni wa-Tanzania wangapi unaowafahamu wenye Law Bar ya ku-practice Criminal Law New York kama Masha? Wewe kwenye maisha yako hujawahi kuzomewa?

In the future weka hoja mkuu, hizi za kujifanya unanijua sana acha mkuu, hapa tunaongelea taifa, sio mimi, unajua mkuu ninakushangaa sana na how you manouver na kujikita kila kona humu JF, I mean ninakuheshumu sana kwa hilo, lakini please ninaomba uniache na hizi personal attacks, ninarudia sina mtandao, wala masilahi ya mtu ninazo mali za kunitosha zangu mwenyewe bro, sihitaji masilahi yako wala ya mtu yoyote, laikini ninao marafiki wa hali ya chini na wahali ya juu, viongozi kwa wananchi, na wakisemwa hapa hata siku moja sitaogopa kusema kuwa ninawafahamu na kama ikibida nitawatetea, ninaruida ninamjua Masha, he is my friend as a human being kama mimi, ni waziri, amezomewa kwa sababu ndio hsasa mchezo wa siasa unavyochezwa inaonekana alikuwa hajui, na ninampa a benefit of the doubt, kwa kuwa ni roookie wa siasa.

Wakuu sijawahi kukimbia ishus, hii nilikuwa sijaiona tu, lakini kama kawaida inajadilika.
 
Hii chini ni extract kutoka ktk makala ya Saed Kubenea


Laurance Masha:

Huyu ni Waziri wa Mambo ya Ndani na Usalama wa Raia.

Huyu alikuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, wakati mkataba wa kinyonyaji wa Richmond unajadiliwa na kusainiwa. Masha hawezi kukwepa lawama kwamba alishiriki katika kuangamiza taifa kutokana na hatua yake ya kunyamazia Richmond hadi wakafanikiwa kuvuna wasichopanda.

Ni jambo la wazi kuwa Masha alikuwa anafahamu kila kitu juu ya Richmond. Ndiyo maana hakujihangaisha kwenda mbele ya Kamati ya Bunge kusema kilichofanyika.

Bila shaka, Masha alifanya hivyo kwa lengo la kumlinda swahiba wake mkubwa, Waziri Mkuu ‘aliyefukuzwa na Bunge,’ Lowassa.

Masha alijua, kama sisi wengine tulivyojua, kwamba Richmond haikuwa kampuni ya Marekani, bali ilikuwa kampuni ya mfukoni ya hapahapa nchini.

Aidha, Masha anatajwa kuwa ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya mawakili ya IMMA Advocate ya jijini Dar es Salaam, ambayo inatuhumiwa kushiriki katika mikataba ya kifisadi.

Kampuni hii inatajwa kuwa ndiyo iliyoandaa na hatimaye kupitisha mkataba kati ya serikali na kampuni ya kitapeli ya Deep Green Limited.

Taarifa za Wakala wa Usajili wa Kampuni (BLERA), zinawataja wakurugenzi wawili wa IMMA kuwa wakurugenzi waanzilishi wa Deep Green.

Ni Deep Green iliyochotewa na BoT na Wizara ya Fedha, mabilioni ya shilingi za umma kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Kwa maneno mengine, Masha hawezi kukwepa tuhuma kwamba ameshiriki kuangamiza uchumi wa taifa hili.

Ama ameshiriki, au alinyamazia makampuni hewa kusajiliwa na kuchota mamilioni ya fedha za wananchi.

Hata panga la Kikwete la kung’oa wafanyabiashara na watu wenye maslahi binafsi ndani ya serikali yake, lisingeweza kupita bila kumkata Masha.

Kampuni ya Masha ndiyo mshirika mkubwa wa kampuni za uchimbaji madini nchini, hasa Barick.

Adam Kigoma Malima:

Ni naibu waziri wa Wizara ya Nishati na Madini.

Malima ni mmoja wa Watanzania na wabunge waliojifanya vipofu na viziwi katika kushughulikia suala la mikataba ya kinyonyaji; kwa mfano ule wa Buzwagi.

Si mara moja wala mbili, Malima kusikika akisema, “Hii ni mikataba mizuri na yenye tija kwa taifa.”

Ni Malima aliyetembelea vituo kadhaa vya redio na televisheni kwa lengo la kuupaka mafuta mkataba wa kinyonyaji wa Buzwagi ili uonekane unafaa mbele ya wananchi. Hakufanikiwa.

Alipoulizwa na wananchi: “Je, unaufahamu mkataba huo? Umeuona?” Hakuwa na la kujibu mbali na kuendelea kung’ang’ana “Mkataba ni nzuri na una manufaa kwa taifa.”

Kama dhamira ya Kikwete ya kupitia upya mikataba ni ya dhati, basi asitegemee kupata ushauri wa maana kutoka kwa Malima, ambaye si muumini wa dhamira hiyo ya Kikwete na haonekani kuwa na upeo mzuri katika eneo hili.

Profesa Juma Kapuya:
Moja ya tuhuma zake kubwa ni kutumia rasilimali za umma kwa maslahi binafsi.

Kapuya anatuhumiwa kutumia vifaa vya jeshi, ikiwamo ndege na magari kinyume cha taratibu. Ni majuzi tu, chini ya uongozi wake, helikopta ya jeshi ilitolewa kwa matumizi ya raia wa kigeni.

Aidha, Kapuya ni mmoja wa wafanyabiashara wakubwa hapa nchini, akitajwa kumiliki mmoja wa migodi ya madini mkoani Arusha.

Kama helikopta ya jeshi ilivyoanguka watu wakapata fursa ya kujua matumizi yasiyo rasmi ya zana za jeshi; ilikuwa pale wezi walipomwibia Kapuya ndipo ikajulikana kuwa ni mfanyabiashara ya kuchimba madini.
 
kikwete jiulize maneno yanatoka wapi,maisha yanakuwa magumu sana kutokana na mikataba feki,mafisadi wamekuzidi nguvu.
 
Kwa mtu kama kapuya , kweli sasa ajiuzuru tu, kwani yeye anamiliki mgodi kibaya zaidi hali hata kodi
 
---ni Kuhusu Kampuni Yake Kusajili Deepgreen
---yeye Asema Aliifungua Na Kuifunga Kwa Maagizo Ya Serikali


""waziri Wa Mambo Ya Ndani Mh Masha Ameonja Joto Ya Jiwe Baada Ya Kuulizwa Maswali Na Wapigakura Wake Na Kuishia Kumumunya Kama Waziri Mkuu Pinda..kuhusu Usajili Wa Kampuni Ya Deep Green Kwenye Kampuni Yake Ambayo Inadaiwa Kuchota Mabillion Ya Pesa!!!
wapiga Kura Hao Walimbana Masha Katika Mkutano Wa Hadhara Uliofanyika Butimba Sokoni Nje Kidogo Ya Jiji La Mwanza!!walitaka Majibu Ya Papo Kwa Papo ,mmoja Wawaliohudhuria Mkutano Huo Bwa Peter Charles Alimuuliza
""je Wewe Ni Mmiliki Wa Kampuni Ya Wanasheria Ya Imma Ambayo Imetoa Jaji Mmoja?????

masha:::ndiyo

charles::
kwa Ville Wewe Ni Msafi Na Utatumikaje Na Wananchi Huku Ukiwa Na Kampuni Ilioshirikiana Kuwaibiwa Watanzania Na Wewe Ni Kigogo Mkubwa Tu???

masha::
nashukuru Kwa Kuuliza Swali Hilo Katika Wilaya Hii..naljua Umelipata Kwenye """vigazeti""lakini Umelipamba Sana Kupita Kiasi
kweli Mimi Ni Mkurugenzi Wa Imma Lakini Kwa Sasa Nipo Likizo Bila Malipo Nakula Posho Tu..kuhusu Ujaji Wa Mh Mujulizi..yeye Ameteuliwa Na Raisi Kutokana Na Taaluma Yake...ni Kweli Kampuni Yangu Ilisajili Deepgreen Na Tukaifunga Kwa Maelekezo Ya Serikali,,imma Haikuchota Mabiliion,,naomba Iweleke,,

'''''!@@###swala Hilo Limeelezwa Na Waziri Mkuu Bungeni Kuwa Ni La Usalama Wa Taifa''swali Hili Linahusu Usalama Wa Taifanami Nasema Basi Na Full Stop..na Kuendelea Kuongelea Ni Kulivua Nguo Taifa..na Kuhitimisha Mkutano Huo Saa Kumina Mbili Kabla Ya Muda..#$$%^&&&&*

masha Ahsante Sana Kwa Ufafanuzi Wako Ambao Kwa Wakati Mmoja Umetufungua Macho Kidogo

1)))ukiwa Kama Waziri Mwenye Kulinda Mamlaka Ya Nchii Hii Huoni Si Busara Kusema Kuendelea Kuongelea Kutaivua Nguo Taifa

2))kaka Yangu Masha Na Furahi Wote Tuna Proff Moja...naomba Kukuelekeza Huoni Taifa Lilishavuliwa Nguo Na Hawa Walioiibia Nchi Kupitia Kampuni Yako

3))nimeona Umekataa Pesa Za Deepgreen Hukuzitumia!!nakuuliza Unsaidie Kujibu Ulikuwa Na Undugu Gani Hiyo Kampuni Mkaifanyia Kazi Bure???na Vipi Kama Walikupatia Hela Mkawa Na Nguvu Yakwenda Pale Kempo!!!1kuganga Glass..huoni Hizo Hela Ulizopokea Ni Za Wananchi?????????

4))huoni Unalitukana Bunge Unaposema Wakiongelea Wanalivua Nguo Taifa Wakati Hivi Sasa Taifa Mmeshalivua Nguo Na Kampuni Ya Imma &deep Green....nafikiri Hivi Sasa Mnachotakiwa Ni Jinsi Ya Kutafuta Nguo Ya Kuwatosha Maana Mmeshakaa Uchi Vya Kutosha,,na Vimini Haviwatoshi Ndio Maana Nduguzo Wanatumia Kujhonga Bunge Sasa Kujisafisha


5))))jitakase Kabla Hayajalipuka Kaka Yangu Jumatano Deadline Kazi Mnayo!!!!kila La Kheri Br

bwabeja Sana!!
 
Hivi shudhuri za IMMA na ushirika wake na DeeGreen na lenyewe ni suala la usalama wa TAIFA! Tumekwisha na usalama wetu hauna maana kwani unatumika kutuhumiza zaidi badala ya kutulinda.
 
---ni Kuhusu Kampuni Yake Kusajili Deepgreen
---yeye Asema Aliifungua Na Kuifunga Kwa Maagizo Ya Serikali


""waziri Wa Mambo Ya Ndani Mh Masha Ameonja Joto Ya Jiwe Baada Ya Kuulizwa Maswali Na Wapigakura Wake Na Kuishia Kumumunya Kama Waziri Mkuu Pinda..kuhusu Usajili Wa Kampuni Ya Deep Green Kwenye Kampuni Yake Ambayo Inadaiwa Kuchota Mabillion Ya Pesa!!!
wapiga Kura Hao Walimbana Masha Katika Mkutano Wa Hadhara Uliofanyika Butimba Sokoni Nje Kidogo Ya Jiji La Mwanza!!walitaka Majibu Ya Papo Kwa Papo ,mmoja Wawaliohudhuria Mkutano Huo Bwa Peter Charles Alimuuliza
""je Wewe Ni Mmiliki Wa Kampuni Ya Wanasheria Ya Imma Ambayo Imetoa Jaji Mmoja?????

masha:::ndiyo

charles::
kwa Ville Wewe Ni Msafi Na Utatumikaje Na Wananchi Huku Ukiwa Na Kampuni Ilioshirikiana Kuwaibiwa Watanzania Na Wewe Ni Kigogo Mkubwa Tu???

masha::
nashukuru Kwa Kuuliza Swali Hilo Katika Wilaya Hii..naljua Umelipata Kwenye """vigazeti""lakini Umelipamba Sana Kupita Kiasi
kweli Mimi Ni Mkurugenzi Wa Imma Lakini Kwa Sasa Nipo Likizo Bila Malipo Nakula Posho Tu..kuhusu Ujaji Wa Mh Mujulizi..yeye Ameteuliwa Na Raisi Kutokana Na Taaluma Yake...ni Kweli Kampuni Yangu Ilisajili Deepgreen Na Tukaifunga Kwa Maelekezo Ya Serikali,,imma Haikuchota Mabiliion,,naomba Iweleke,,

'''''!@@###swala Hilo Limeelezwa Na Waziri Mkuu Bungeni Kuwa Ni La Usalama Wa Taifa''swali Hili Linahusu Usalama Wa Taifanami Nasema Basi Na Full Stop..na Kuendelea Kuongelea Ni Kulivua Nguo Taifa..na Kuhitimisha Mkutano Huo Saa Kumina Mbili Kabla Ya Muda..#$$%^&&&&*

masha Ahsante Sana Kwa Ufafanuzi Wako Ambao Kwa Wakati Mmoja Umetufungua Macho Kidogo

1)))ukiwa Kama Waziri Mwenye Kulinda Mamlaka Ya Nchii Hii Huoni Si Busara Kusema Kuendelea Kuongelea Kutaivua Nguo Taifa

2))kaka Yangu Masha Na Furahi Wote Tuna Proff Moja...naomba Kukuelekeza Huoni Taifa Lilishavuliwa Nguo Na Hawa Walioiibia Nchi Kupitia Kampuni Yako

3))nimeona Umekataa Pesa Za Deepgreen Hukuzitumia!!nakuuliza Unsaidie Kujibu Ulikuwa Na Undugu Gani Hiyo Kampuni Mkaifanyia Kazi Bure???na Vipi Kama Walikupatia Hela Mkawa Na Nguvu Yakwenda Pale Kempo!!!1kuganga Glass..huoni Hizo Hela Ulizopokea Ni Za Wananchi?????????

4))huoni Unalitukana Bunge Unaposema Wakiongelea Wanalivua Nguo Taifa Wakati Hivi Sasa Taifa Mmeshalivua Nguo Na Kampuni Ya Imma &deep Green....nafikiri Hivi Sasa Mnachotakiwa Ni Jinsi Ya Kutafuta Nguo Ya Kuwatosha Maana Mmeshakaa Uchi Vya Kutosha,,na Vimini Haviwatoshi Ndio Maana Nduguzo Wanatumia Kujhonga Bunge Sasa Kujisafisha


5))))jitakase Kabla Hayajalipuka Kaka Yangu Jumatano Deadline Kazi Mnayo!!!!kila La Kheri Br

bwabeja Sana!!

sijapenda ulivyo iweka humu stori hii, hebu tuwekee habari kamili kama ilivyoandikwa kwanza, kwani nina hakika hukuwepo katika mkutano huo
 
Mkuu FMES,
Tulipoliongelea hili la Masha + Imma + Deepgreen + Ridhiwani Kikwete, ulijitokeza kumtetea kijana Masha kuwa ni safi, je huu msimamo bado unao au kuna mabadiliko?? Mimi bado nawaona kuwa wote hawa wameshonwa pamoja kutengeneza mduara mzuri wa ufisadi.
 
Back
Top Bottom