Waziri Lawrence Masha hana uwezo

Waziri Lawrence Masha hana uwezo

Naona si vyema kumshambulia mleta mada, badala yake tumuombe atupe data zaidi ili tumkome nyani vizuri. kwamfano katika mada yake kuna issue kuu mbili na mawili yatokanayo:

1) -Waandishi walikatiwa mshiko wa alfu 20 ili wasiandike maswali ya wapiga kura wake ya kwanini aliisajiri Deep Green? je aliwajibu majibu ya kutosheleza?
---Je waandishi kwa kupokea hiyo alfu 20 mkaacha kuandika habari nzito namna hii mnatutendea haki watanzania wenzenu?

2)-Jambo la pili ndo hilo la kutoa zawadi binafsi kwa ma miss, je ni jambo jema kwa waziri mwenye dhamana kufanya hivo? je anapo toa pesa hiyo kwa shughuli kama hiyo wakati wapiga kura wake kuna watoto wana shindwa kwenda shule kwa kukosa uniform ya alfu 5 ni sawa?

----Jambo la mwisho linatokana na baadhi ya wachangiaji wanao uliza kwamba alitoa sh ngapi na kama alikuwa kaisha onja mbili tatu kwani wanamjua tabia yake, wasi wasi wangu ni je, waziri mwenye dhamana hatakiwi kuwa na maadili fulani ya kulinda heshima yake na pengine kuwa katika mazingira na hali ambayo haihatarishi maslahi ya taifa?, mfano kama akionja anakuwa 'out of himself' hawezi kuliingiza Taifa mkenge kwakutoboa siri, ama kufanya maafikiano fulani ambayo hayana tija kwa Taifa?
Hawa ndiyo viongzo tulio nao,wewe haushangai ukienda pale Club 84 dodoma utawakuta wakivizia watoto wa CBE
 
Sijui inawezekana kuwa na viongozi wa namna hii ni maendeleo, na huenda alichokifanya kinastahili kuungwa mkono kwa mtazamo wa wengine. Lakini kamwe zawadi binafsi kutoka kwa Masha kama , shilingi 150,000 na Seti ya Tv, shilingi laki moja kwa mshindi wa Urembo wa Pili na Laki Moja kwa mshindi wa Tatu, na shilingi 50 kwa kila mmoja kati wengine tisa waliobakia, na hapo hapo kuna zawadi tayari zilikuwa zimetolewa na muaandaaji, lakini pia kuna wahitaji wengi wenye shida katika jimbo lake, hili haliingii akilini.

Lakini Pia tuangalia aina ya viongozi ambao tunawatarajia linapokuja suala la vitendo, mienendo na yale ambayo jamii inatarajia iwafanyie.

Wabunge wengi walishagundua kwamba njia rahisi ya kushinda kwenye chaguzi ni kwa kutumia vitu kama hivyo. Wapiga kura wa Bongo hawaangalii hoja/issues bali wanaangalia huyu anajichanganya vipi na wapiga kura wake, takrima za kutoa zawadi kama hizo, takrima kwa wamachinga/mamalishe/babalishe ambazo ziko kwenye mfumo wa misaada kwa wajasiriamali japo hatujiulizi hizo zinazotolewa zilipatikana kihalali ama kifisadi?

Sioni kosa la Masha kwa kuwa bado miaka 2 tu watu waingie kilingeni (kwenye uchaguzi). Hamjiulizi kwanini trip za wabunge wetu kwenda kwenye majimbo yao zimeongezeka sana. Hiyo ni one of the platforms za wanasiasa kuonyesha ukaribu wao na jamii.

Hoja kwamba ni mashindano ya kanda na hivyo Bwana Masha asitoe zawadi sidhani kama ni nzito sana, ukweli ni kwamba mashindano yamefanyikia Mwanza mjini ambako ni base ya Bwana Masha, kitendo cha yeye kutoa zawadi kwa wanyange ni pamoja na kuionyesha jamii kwamba yuko pamoja nayo.

Ukiwa Mbunge huwezi kuwa unagawa hela kwa kila unaekutana nae, bali unatakiwa kutumia platforms kama hizo ambazo kwa namna moja ama nyingine ni sehemu ya wapiga kura. Ukimpa mtu mmoja mmoja nani atakuona na atamtangazia nani kwamba Mbunge kampa hela. Hapo kwenye mashindano StarTV walikuwa hewani na Mheshimiwa akamwaga zawadi watu wote wakiona kwa macho na kusikiliza. Ndiyo maana wabunge ni wepesi sana kutoa hela kwa vikundi vya wamachinga/vijana/mamalishe/babalishe kuliko kutoa kwa mtu mmoja mmoja.

Watu wako kwenye kampeni, 2010 ni kesho tu wala si mbali. Wale watakaokuja 2009 mwishoni shauri yao, wataambulia pakavu. Wakati wa kusaka kura ni sasa!
 
Siku chache baada ya kusoma habari kuhusu Waziri Masha kubana na wapiga kura wake juu ya Kampuni Yake Kusajili Deepgreen naye kudai aliifungua Na Kuifunga Kwa Maagizo Ya Serikali, ameibuka Mwandishi mmoja swahiba wa Rostam ambaye ameanza kuzusha kuwa swali aliloulizwa Masha liliandaliwa na waandishi na kisha kuandikwa habari hiyo.

Kwa muda nimekaa kimya na kulifuatilia kwa makini na kubaini kuwa waandishi waliohudhuria hapo akiwemo na anayezusha kuwa swali hilo liliandaliwa na waandishi walifuata posho za Ufisadi na baada ya kulipwa sh. 20,000 hawakuandika habari hiyo isipokuwa mmoja aliyejitolea kuilima Mwananchi. Nampongeza.

1.Hii nadhani no moja ya mbinu ambazo wanaanza kutumia kuwadhoofisha waandoshi hasa wa mikoani na kuwatishia, john Maduhu ndiye aliyekwenda uwanja wa dege wa Mwanza asubuhi kumpelekea gazeti hilo Masha na kujadiliana kwa muda wa dk 30.
2.Ninavyomfahamu mwandishi huyo asingeshindwa kumhoji swali hilo Masha mpaka atumie mbunu za kutuma watu kumuuliza masha kisha andike kwa vile amewahi kuandika story nyingi kubwa na nzuri zaidi ya hizo.
3.Kilichomtuma mwandishi huyo kuonana na masha uwanja wa ndege ndicho kinachotokea kwa kujaribu kuzusha uongo kuwa sali hilo liliulizwa na mwandishi kisha kuandika hata kama alifanya hivyo nadhani hakuna ubaya kwani imetusaidia kujua Deep Green ilisajiliwa kwa mkono wa serikali na mmiliki wake ni serikali kama Masha alivyoeleza kama inavyozihirisha hapa.

"je Wewe Ni Mmiliki Wa Kampuni Ya Wanasheria Ya Imma Ambayo Imetoa Jaji Mmoja?????

masha:::ndiyo

charles::
kwa Ville Wewe Ni Msafi Na Utatumikaje Na Wananchi Huku Ukiwa Na Kampuni Ilioshirikiana Kuwaibiwa Watanzania Na Wewe Ni Kigogo Mkubwa Tu???

masha::
nashukuru Kwa Kuuliza Swali Hilo Katika Wilaya Hii..naljua Umelipata Kwenye """vigazeti""lakini Umelipamba Sana Kupita Kiasi
kweli Mimi Ni Mkurugenzi Wa Imma Lakini Kwa Sasa Nipo Likizo Bila Malipo Nakula Posho Tu..kuhusu Ujaji Wa Mh Mujulizi..yeye Ameteuliwa Na Raisi Kutokana Na Taaluma Yake...ni Kweli Kampuni Yangu Ilisajili Deepgreen Na Tukaifunga Kwa Maelekezo Ya Serikali,,imma Haikuchota Mabiliion,,naomba Iweleke,,
 
Mhe Masha na uvaaji wake wa Miwani Bungeni, umeniacha hoi leo, maana alikuwa ameipandisha juu kichwani wakati akisikiliza michango ya Wabunge kuhusu Bajeti ya Wizara yake.

Inanikumbusha Ubitoz, ucheck bob na zile enzi za ku stambalei
 
Haya mawazo mengine yanatakiwa kubaki kichwani.....na sio ya kuanzisha thread...tena muhimu!
 
HUKU kuna watoto na watu wazima,humu kuna kila aina ya watu wengine mafisadi wengine wanaililia nchi yao,hivyo kila kitu kinaweza kuwekwa humu.
 
Jamaa huyu ukimuona anaongea utadhani zimejaa, lakini nachelea kusema hapo alipo hazitoshi.

Natumia kigezo kimoja cha mauaji ya Albino. Inatosha maana hata kama ni makosa, tangu March mambo haya yalipoanza, angerekebisha kitambo.

Ktk mahojiano na BBC alionyesha hana lolote. Anachosema ni kueleimisha umma. Wakati umma unaelimishwa nini kifanyike maana haya ni mauaji na elimu yaweza kuwa ya miaka.

Naona anaendesha wizara kama kikosi cha wanasheria na kesi zao mahakamani.

Siombei mabaya mtu yeyote, lakini akiwa bado ni Waziri naomba kifo cha waziri mmoja kwa imani yoyote ile! Hapo nadhani tutaona nchi nzima ikitanda Polisi.

Au ndo matokeo ya uwaziri wa bakshishi?
 
Jamaa huyu ukimuona anaongea utadhani zimejaa, lakini nachelea kusema hapo alipo hazitoshi.

Natumia kigezo kimoja cha mauaji ya Albino. Inatosha maana hata kama ni makosa, tangu March mambo haya yalipoanza, angerekebisha kitambo.

Ktk mahojiano na BBC alionyesha hana lolote. Anachosema ni kueleimisha umma. Wakati umma unaelimishwa nini kifanyike maana haya ni mauaji na elimu yaweza kuwa ya miaka.

Naona anaendesha wizara kama kikosi cha wanasheria na kesi zao mahakamani.

Siombei mabaya mtu yeyote, lakini akiwa bado ni Waziri naomba kifo cha waziri mmoja kwa imani yoyote ile! Hapo nadhani tutaona nchi nzima ikitanda Polisi.

Au ndo matokeo ya uwaziri wa bakshishi?

Kamanda mkuu kwanza hongera kwa kufikisha post 1.

Nadhani hapa humtendei haki Mh Masha, kweli kuna matatizo kufuatia vifo vya maalbino na hatua kadhaa zishachukuliwa na Wizara, jambo muhimu hapa ni kuwa suala hili ni matokeo ya imani za kishirikina ktk jamii na namna ya ku deal nalo kunahitaji ushirikiano wa pamoja baina ya serikali na sisi sote. Kuanza kunyoosha kidole kwa mtu mmoja kama ndio chanzo/solution ya jambo complex kama hili nadhani humtendei haki Mh Masha
 
Kamanda mkuu kwanza hongera kwa kufikisha post 1.

Nadhani hapa humtendei haki Mh Masha, kweli kuna matatizo kufuatia vifo vya maalbino na hatua kadhaa zishachukuliwa na Wizara, jambo muhimu hapa ni kuwa suala hili ni matokeo ya imani za kishirikina ktk jamii na namna ya ku deal nalo kunahitaji ushirikiano wa pamoja baina ya serikali na sisi sote. Kuanza kunyoosha kidole kwa mtu mmoja kama ndio chanzo/solution ya jambo complex kama hili nadhani humtendei haki Mh Masha


Nionavyo, siyo ajabu Waziri kutwishwa mzigo.
Kwa nini kuzima maandamano ya wanafunzi isiwe complex.

Kwa nini kupambana na CUF Pemba isiwe complex. Au majambazi. Mimi kama MchunguZI, nawezaje kuisaidia serikali ktk hili?

Kwa utendaji wa serikali zetu, Wizara inaweza kwenda vizuri kama una waziri mzuri na inaweza kuwa mbovu kama una waziri mbovu. Tumeyaona ELimu!

Tatizo langu kubwa siyo Masha ila tu naona sasa image ya nchi iko pabaya kabisa. Vyombo vikuu vya Habari Dniani vimelidaka hili. BBC wameonyesha ya kwao. Aljazeera wameahidi kuieleza Tz sunday.

Kwa takwimu, inaonyesha sisi TZ na Zimbabwe tunaongoza kwa idadi ya Albino Africa. Kweli hatusituki kuwalinda kwa njia za dharula.
 
Si vema ku-judge utendaji wa mtu kwa kuangalia suala moja tu. Kama mkiruhusu kufanya hivyo, basi mimi nitawatolea mfano wa mahabusu ambao siku hizi hupelekwa mahakamani katika mabasi yenye viyoyozi na muziki mkubwa, yaani hakuna kabisa makarandinga
 
tatizo la kitaifa na si la waziri muhusika kila mtu ana majukumu ya kuwalinda hawa maalbino tatizo ni njaa na maisha duni ambayo si masha walafaamilia yake wenye uwezo wa kutusaidia hili,,waziri endelea kuhali ni ngumu
 
Nionavyo, siyo ajabu Waziri kutwishwa mzigo.
Kwa nini kuzima maandamano ya wanafunzi isiwe complex.

Kwa nini kupambana na CUF Pemba isiwe complex. Au majambazi. Mimi kama MchunguZI, nawezaje kuisaidia serikali ktk hili?

Kwa utendaji wa serikali zetu, Wizara inaweza kwenda vizuri kama una waziri mzuri na inaweza kuwa mbovu kama una waziri mbovu. Tumeyaona ELimu!

Tatizo langu kubwa siyo Masha ila tu naona sasa image ya nchi iko pabaya kabisa. Vyombo vikuu vya Habari Dniani vimelidaka hili. BBC wameonyesha ya kwao. Aljazeera wameahidi kuieleza Tz sunday.

Kwa takwimu, inaonyesha sisi TZ na Zimbabwe tunaongoza kwa idadi ya Albino Africa. Kweli hatusituki kuwalinda kwa njia za dharula.

Mchunguzi,

Hivi unathubutu kufafanisha mauaji ya albino na maandamano ya wanafunzi? lets be serious for a minute.... sasa ikiwa jambo ambalo linaiweka "image" ya nchi pabaya na linashadidiwa na vyombo vya nje vikiwemo BBc na Aljazeera bado una thubutu kulifafanisha na maandamano ya wanafunzi!

Narudia hili jambo limechukua sura ya kitaiafa na linahitaji juhudi za kila mmoja wetu, mnakotupeleka ni sawa na kusema kwa kuwa watu wanakufa kwa Malaria au ukimwi basi waziri wa afya hana uwezo!
 
Ndugu yangu 'mwamba' masatu,
hapa ndipo watu wengi tunapokosea.Yaani unsema suala la maandamano ya wanafunzi sio complex like Albinos death?Hivi umeshawahi kukumbana na adha ya usafiri wa daladala dsm?au enzi hizo hazijawahi kukumba!
Unataka tuamini kuwa mathalani maandamano wanayofanya wanafunzi wa vyuo vikuu kudai serikali iwatekelezee baadhi ya mambo ambayo hayaendi sawa kwa mfano suala la mikopo kutoka Loan board we unaona sio jambo la maana kabisa.
Labda hauna mtoto na au hauna mpango wa kuwa na mtoto ndani ya nchi yetu ya danganyika.
Ulishawahi kukumbana na mabomu na risasi kama wanvyotwangwa watu wa pemba au nyamongo- Tarime?
Hebu jiulize ni kwanini serikali inatumia nguvu nyingi sana kupambana na wafuasi wa vyama vya upinzani.Jiulize ni kwanini serikali inatumia nguvu nyingi kupambana na wanafunzi wanapogoma au kuandamana.
Kisha jiulize kwanini serikali hiyo hiyo haitumii nguvu hizo hizo kupambana na wauaji wa waalbino? Kama mwandishi wa habari ameweza kufanya utafiti ukipenda ita upelelezi makini kiasi kile serikali inashindwa nini?
Au hukumsikia waziri Masha alivyokuwa anajikanyaga kanyaga siku ile alivyokuwa anahojiwa na Flora Nducha wa BBC?
Pamoja na utetezi wote unaotolewa na serikali na watu wengine kama wewe, bado haitoshi kutufanya tuamini kuwa serikali inalichukulia suala hili kwa umuhimu unaostahili. Bado wanahitaji kufanya kitu kwa maslhi ya hawa wenzetu waalbino.
 
Mchunguzi,

Hivi unathubutu kufafanisha mauaji ya albino na maandamano ya wanafunzi? lets be serious for a minute.... sasa ikiwa jambo ambalo linaiweka "image" ya nchi pabaya na linashadidiwa na vyombo vya nje vikiwemo BBc na Aljazeera bado una thubutu kulifafanisha na maandamano ya wanafunzi!

Narudia hili jambo limechukua sura ya kitaiafa na linahitaji juhudi za kila mmoja wetu, mnakotupeleka ni sawa na kusema kwa kuwa watu wanakufa kwa Malaria au ukimwi basi waziri wa afya hana uwezo!

Masatu,
Hebu niseme hivi;
If everybody is responsible then nobody is irresponsible and vice versa.

Usifanye kazi ikawa ni ya kila mtu. ikisha kuwa hivyo basi amini, hakuna wa kuifanya, na hakuna mwenye makosa. Waache wanasiasa waseme hivyo wanaposhindwa lakini mtendaji anayejua wajibu wake hawezi kusema hivyo.

Mtoa mada anaweza kuwa amekosea au kaonyesha hasira yake lakini hata mimi nasema Juhudi ya serikali ktk jambo hili hailinganmi na ukubwa wa tatizo. na Serikali kwa upande huo ni Wizara husika na ni Waziri muhusika, Lawrence Masha.

Tena ningependa tusiseme ni mauaji ya Albino. Tuseme ni mauaji ya raia wenzetu. Huko mbeya hatukusema mauaji wa Wanyakyusa au Wasafa au Wandali. Mtu akichunwa ngozi, akikatwa mkono, nk. ni raia basi!
 
Masatu,
Hebu niseme hivi;
If everybody is responsible then nobody is irresponsible and vice versa.

Usifanye kazi ikawa ni ya kila mtu. ikisha kuwa hivyo basi amini, hakuna wa kuifanya, na hakuna mwenye makosa. Waache wanasiasa waseme hivyo wanaposhindwa lakini mtendaji anayejua wajibu wake hawezi kusema hivyo.

Mtoa mada anaweza kuwa amekosea au kaonyesha hasira yake lakini hata mimi nasema Juhudi ya serikali ktk jambo hili hailinganmi na ukubwa wa tatizo. na Serikali kwa upande huo ni Wizara husika na ni Waziri muhusika, Lawrence Masha.

Tena ningependa tusiseme ni mauaji ya Albino. Tuseme ni mauaji ya raia wenzetu. Huko mbeya hatukusema mauaji wa Wanyakyusa au Wasafa au Wandali. Mtu akichunwa ngozi, akikatwa mkono, nk. ni raia basi!

Sawa mkuu nimekusikia, kwa kuongezea hapo hapo kwenye uwajibikaji Mwenyekiti Mbowe awajibike nae pia iweje yeye Mwenyekiti anatumia gari la kifahali ( Vogue ) na kuzunguka nchi nzima na hellicopter wakati Makamu wake wa Mwenyekiti anapanda Corolla limited E100 mbovu inapita ikichomoka matairi ovyo na kupelekea kifo cha Kiongozi mkubwa wa chama.

Talk abt uwajibikaji....
 
Si vema ku-judge utendaji wa mtu kwa kuangalia suala moja tu. Kama mkiruhusu kufanya hivyo, basi mimi nitawatolea mfano wa mahabusu ambao siku hizi hupelekwa mahakamani katika mabasi yenye viyoyozi na muziki mkubwa, yaani hakuna kabisa makarandinga

Mpita njia utakuwa unaishi Dar. Mahabusu wanasafirishwa kwa basi hapo Dar tu! Ile mikoa ya nje au hata hapo Kibaha, bado wako ndani ya Karandinga.

In short, Kusafirishwa kwa basi au baiskeli hakuna impact kwa mwananchi wa mitaani au mpiga kura wako na siyo kazi ya msingi ya hiyo Wizara.

Mauaji ni fundamental. ULINZI WA RAIA (Period). Hata afanye yooote ajuwayo! bila hili la ulinzi wa raia, hatumuhitaji.
 
Mtu mmoja tu katika baraza lako la mawaziri anayetupa matumaini ni Magufuli tu. Anadiriki kuwanyooshea kidole hata mawaziri wenzake. Kinakuzuia nini kumpa uwaziri mkuu huyo mtu? Tanzania inahitaji PM mwenye guts kama hizi.
PM wako ni playboy hamna kitu. Sawa na Sumaye tu. Mng'oe kabla hajakutia aibu. Mambo yake yoote yanajulikana.

SOURCE: Alasiri

...Siwezi kuamini kama mpaka leo kuna watu hawajamjua magufuli kuwa ni mshenzi na hafai kuwa kiongozi wa level aliyopo...ni mropokaji,mwongo na mtaka sifa...zile takwimu anazotoaga,ukiwauliza wataalamu wenyewe wanaohusika wanakwambia ni kanyaboya...wadanganyika wengi hawana uwezo wa kumchambua mtu...ndio uzuri wenu...anachofanya huyu jamaa ni kucheza na vyombo vya habari na kupiga kelele then wajinga wanamshangilia.....amka !!!wacha ujinga!!!
 
Sawa mkuu nimekusikia, kwa kuongezea hapo hapo kwenye uwajibikaji Mwenyekiti Mbowe awajibike nae pia iweje yeye Mwenyekiti anatumia gari la kifahali ( Vogue ) na kuzunguka nchi nzima na hellicopter wakati Makamu wake wa Mwenyekiti anapanda Corolla limited E100 mbovu inapita ikichomoka matairi ovyo na kupelekea kifo cha Kiongozi mkubwa wa chama.

Huyu jamaa wa ajabu kweli kawafanya watz mbun'go au nzige! kuwazungukia kwa helikopta! ukiondoa Ian Smith (zimbabwe) hakuna mwanasiasa alishaomba kura kwa staili hiyo.
 
huyu naye tumesikia ni MU AMERICA na si mtanzania ndio maana hana uchungu na maalbino wanaochinjwa huko kwao Mwanza
 
Back
Top Bottom