Waziri Bashungwa: Mkandarasi ongeza kasi ukamilishe ujenzi wa jengo la Wizara

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987

Mjengo22.jpeg

Mjengo 2.jpeg
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemuagiza Mkandarasi Vikosi vya Ujenzi kuongeza kasi ya utekelezaji wa ujenzi wa jengo la Wizara linalojengwa katika Ofisi za Serikali Mtumba Jijini Dodoma ili kuendana na ratiba ya ukamilishaji.

Bashungwa ametoa agizo hilo Januari 29, 2024 wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo ambalo hivi sasa limefikia asilimia 71 na kusisitiza ubora na viwango katika utekelezaji wake.
Mjengo.jpeg
Bashungwa amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Mhandisi Aisha Amour, kuendelea kusimamia ujenzi huo ili kuhakikisha malengo na maelekezo ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya utekelezaji wa majengo ya Wizara katika mji huo yanafikiwa.

Aidha, amezipongeza Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi kwa ushirikiano wao walioutoa katika ujenzi huo kuanzia hatua za awali za usanifu hadi sasa ambapo Mkandarasi yupo katika hatua za mwisho za utekelezaji wa jengo hilo.

Bashungwa amemsisitiza Mkandarasi huyo kutekeleza hatua za mwisho za ujenzi vizuri (finishing) ili Ofisi hiyo kuwa ya mfano, sambamba na kuwa na mkakati wa kuwapa maarifa wataalamu wa Sekta ya Ujenzi ili kuwawezesha wataalamu hao kupata ujuzi na kuweza kutekeleza kazi hizo wenyewe.
Mjengo1.jpeg
“Wataalamu ambao watafanyakazi na Mturuki katika finishing wahakikishe wanarithisha ujuzi na utaalamu kwa Watanzania, ili kutumia wataalamu wetu katika majengo mengine,” amesema Bashungwa.

Upande wake Mtendaji Mkuu wa Vikosi vya Ujenzi, Mhandisi Simeoni Machibya, amemhakikishia Waziri huyo kuwa ujenzi wa jengo hilo utazingatia viwango na ubora ili kufikia malengo ya Serikali.

Mhandisi Machibya ameeleza kuwa asilimia 68 ya vifaa vitakavyofungwa katika jengo hilo vimetoka nchini kupitia makampuni mbalimbali.
 

Attachments

  • Mjengo1.jpeg
    Mjengo1.jpeg
    371 KB · Views: 2

MKANDARASI ONGEZA KASI UJENZI WA JENGO LA WIZARA: BASHUNGWA

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemuagiza Mkandarasi Vikosi vya Ujenzi kuongeza kasi ya utekelezaji wa ujenzi wa jengo la Wizara linalojengwa katika Ofisi za Serikali Mtumba, jijini Dodoma ili kuendana na ratiba ya ukamilishaji.

Bashungwa ametoa agizo Januari 29, 2024 wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo ambalo hivi sasa limefikia asilimia 71 na kusisitiza ubora na viwango katika utekelezaji wake.

Bashungwa amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Mhandisi Aisha Amour, kuendelea kusimamia ujenzi huo ili kuhakikisha malengo na maelekezo ya Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa ya utekelezaji wa majengo ya Wizara katika mji huo yanafikiwa.

Aidha, amezipongeza Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi kwa ushirikiano wao walioutoa katika ujenzi huo kuanzia hatua za awali za usanifu hadi sasa ambapo Mkandarasi yupo katika hatua za mwisho za utekelezaji wa jengo hilo.

Bashungwa amemsisitiza Mkandarasi huyo kutekeleza hatua za mwisho za ujenzi vizuri (finishing) ili Ofisi hiyo kuwa ya mfano, sambamba na kuwa na mkakati wa kuwapa maarifa wataalamu wa Sekta ya Ujenzi ili kuwawezesha wataalamu hao kupata ujuzi na kuweza kutekeleza kazi hizo wenyewe.

“Wataalamu ambao watafanyakazi na Mturuki katika finishing wahakikishe wanarithisha ujuzi na utaalamu kwa Watanzania, ili kutumia wataalamu wetu katika majengo mengine”, amesema Bashungwa.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Vikosi vya Ujenzi, Mhandisi Simeoni Machibya, amemhakikishia Waziri huyo kuwa ujenzi wa jengo hilo utazingatia viwango na ubora ili kufikia malengo ya Serikali.

Mhandisi Machibya ameeleza kuwa asilimia 68 ya vifaa vitakavyofungwa katika jengo hilo vimetoka nchini kupitia makampuni mbalimbali.
WhatsApp Image 2024-01-29 at 16.36.44.jpeg
WhatsApp Image 2024-01-29 at 16.36.45.jpeg
WhatsApp Image 2024-01-29 at 16.36.46.jpeg
WhatsApp Image 2024-01-29 at 16.36.46(1).jpeg
WhatsApp Image 2024-01-29 at 16.36.47.jpeg
WhatsApp Image 2024-01-29 at 16.36.47(1).jpeg
WhatsApp Image 2024-01-29 at 16.36.48.jpeg
WhatsApp Image 2024-01-29 at 16.36.48(1).jpeg
WhatsApp Image 2024-01-29 at 16.36.49.jpeg
 
Back
Top Bottom