Waziri anapewa heshima za mwisho Karimjee, Rais yuko Marekani

Waziri anapewa heshima za mwisho Karimjee, Rais yuko Marekani

Kikwete ni mtu wa matunuzi, sasa yuko kwa Obama subiri hizi siku 20, ataenda kwa Cameron (UK), Angela Markel (Ujerumani), France, Spain, Kenya, Rwanda etc
 
Ucfikirie kukaa NY ndio kuukata au kujua mengi hata ce tuko UK lkn tupo kimya penye ukweli tunawapa live

Huelewi context, huelewi theme, huelewi concept..,

Umetoa majibu ya kiwango chako cha elimu, ulipo, na unachofanya(nothing), in one reply.

Endelelea kupoteza muda mtandaoni, ukichoka, utarudis shule, usome, uelimike uanze upya kutafuta cha kufanya.

Sayonara.
 
Kwa akili yako waziri akifa mambo yasiendelee mbona watanzania tunaonyesha uwezo wetu wa kufikilia unakua mdogo
 
Nilipokuwa shule ya msingi niliwahi kuwasimulia wenzangu kuhusu usafiri wa ndege WEE waligeuka mbogo eti usitudanganye...leo hii watu wanaona rais kupanda ndege(usafiri wa kawaida tu! hasa kama unaenda nje ya nchi) kama ni anasa LOH.. Hivi angekuja alafu arudi tena si ndo mgechonga kuwa anatumia kodi vibaya.si lazima kwa mba angekuja,ndio maana kitu kama hicho hakipo kwenye katiba bali ni desturi tu!,mwisho ALITOA POLE NA ALITUMA MWAKILISHI(KUTOKA IKULU/SERIKALINI) Mbona povu ka vilaza na ma t-shirt yao pale jangwani,refer to his exellence hon.benjamin words hahahaa!
 
Unashangaa waziri anapewa heshima za mwisho rais yuko Marekani.

Lakini haukushangaa kiongozi na mgombea ubunge wa Chadema amefariki akitoka kwenye kampeni Lowassa alikuwepo Tanzania kashindwa kwenye kumzika mgombea ubunge ambaye alikuwa anampigia kampeni usiku kucha

Rais Kikwete atakwenda kumzika waziri wake akirudi kutoka safarini.

Msiwe wanafiki mnajifanya mna huruma wakati msiba wa Mtoi mmeukimbia.

We popoma ni mnafiki kwelikweli, unasema mgombea wa chadema hakuenda kumzika mtoi mgombea ubunge, je vp mbona husemi mgombea wa ccm urais wa ccm magufuli kwenda kumzika mgombea ubunge tena waziri mwenzie! Au magufuli naye yuko nje ya nchi?!
 
Kikwete ni mtu wa matunuzi, sasa yuko kwa Obama subiri hizi siku 20, ataenda kwa Cameron (UK), Angela Markel (Ujerumani), France, Spain, Kenya, Rwanda etc
Nina uhakika ashinde magufuli , ashinde lowassa. Jamani Safari za raisi lazima zipungue, semeni chochote lakini ukweli kwa uchumi wetu hatuwezi kungharimia raisi ajaye Safari zaidi ya 300 nje ya Nchi kwa miaka kumi. Tujifunze hapo, na hii lazima iwe kauli Mbiu ya watanzania wote. Tuwe tumejifunza hii miaka kumi
 
YAYA TOURE alipofiwa na kaka yake wakati wa mechi za kombe la dunia 2014 hakurudi ivory coast nyumbani kumzika kwa sababu sheria za kombe la dunia haziruhusu.tuwe fair rais hawezi kuhudhuria kila msiba by the way makamu wa rais alikuwepo
 
Hii ni fedheha kubwa kama rais wa Tanzania waziri wake anafariki akiwa nje ya nchi anashindwa kukatisha ziara na kurudi kujumuika na Watanzania kwenye maombolezo.

Tumeona kwa wenzetu huko alipo ingetokea rais wao akiwa hapa kwa vyovyote angekatiza ziara na kurudi kujumuika na raia wake.
Lakini rais wetu bila kujali ameendelea kula raha nje, huku tukidanganywa kuwa yupo kwenye shughuli za kiserekali. Hata kama yupo katika shughuli za kiserikali lakini inapotokea kifo katika taifa lako ni jukumu lako rais kuhairisha msafara na kurudi kujumuhika na raia wako. Kwani kundi aliloongozana nalo hakuna anaeweza kubaki na kuendelea na ziara mpaka awepo yeye.

Siku zote mnasema Kikwete ni mpenda watu ikitokea misiba anahudhuria, hakuna inategemeana na misiba na nyingine zinamkuta akiwa hapa nchini. Lakini ukifuatilia misiba na matukio mazito ya nchi yetu yaliyowahi kutokea ambazo rais anatakiwa awepo Kikwete hajawahi kukatiza ziara na kurudi. Anachojali sasa hivi ni kuhakikisha anamalizia ziara zake kwa mgongo wa urais.

tUNAMSHUKURU MUNGU KWA KIKWETE KUMALIZA AWAMU YAKE LA SIVYO WATANZANIA TUNGEENDELEA KULIA NA KUSAGA MENO. KIKWETE RAHA YAKE NI KWENDA KUOMBAOMBA MISAADA NJE WAKATI KATIKA NCHI YETU TUNA KILA KITU.

nina wasiwas na uwezo wako wa kufikir.
Ww unaona ni bora kuhangaika na mtu aliyekufa kuliko kuangalia mistakabali ya waliohai?

Nyinyi ndio mnaonyesha ufahari misiban wakat huyo marehem alipokuwa anaumwa hukuonesha jitihada zozote za kuokoa uhai wake.

Yaan ww kichwan n mr zero kama sumaye
 
Halafu vilevile amekaimisha ofisi kwa makamu wa Rais. Zinfatieni itifaki yeye hatembei na ikulu jamani. Ni vyema mkawa na hoja za mashiko
 
yuko kwenye mkutano wa UN,jamani kifo hakinaga taarifa.RAIS WETU MWACHENI
AHUDHULIE BARAZA LA UN

Kuna siku Mheshimiwa alishawahi katisha ziara ya kikazi mwaka 2014, soma:

Rais Jakaya Kikwete Akatisha Ziara ya Kikazi Davos,Uswisi na Kurejea Nchini ili kujiunga na wananchi wa jimbo la Chalinze katika msiba wa Mbunge wa jimbo hilo Marehemu Said Bwanamdogo, ambaye amefariki dunia alifariki dunia Januari 22, 2014 katika wodi ya Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu (MOI) alikokuwa akitibiwa. Mazishi yamepangwa kufanyika leo nyumbani kwa marehemu Miono, Bagamoyo’ Haki Ngowi Friday, January 24, 2014


Picha Maalum kutoka IKULU:Rais Jakaya Kikwete Akatisha Ziara ya Kikazi Davos,Uswisi na Kurejea Nchini ili kujiunga na wananchi wa jimbo la Chalinze katika msiba wa Mbunge wa jimbo hilo Marehemu Said Bwanamdogo, ambaye amefariki dunia alifariki dunia
 
YAYA TOURE alipofiwa na kaka yake wakati wa mechi za kombe la dunia 2014 hakurudi ivory coast nyumbani kumzika kwa sababu sheria za kombe la dunia haziruhusu.tuwe fair rais hawezi kuhudhuria kila msiba by the way makamu wa rais alikuwepo

rais wa nchi unamfananisha na YAYA TOURE
 
Vasco Da Gama,katika ubora wake!!..Waacheni wafu wawazike wafu wao!!Mbunge wa Ulanga anazikwa Moro Mjini,hili nalo limenistua!!Iko wapi dhana ya Uwakilishi wa wananchi ukiwa mmoja wao?
 
Back
Top Bottom