Wazazi wetu na kauli zao

Wazazi wetu na kauli zao

"Mbwa mzee hafundishwi sheria, nimesema utafanya kama nilivyosema" hapa kisingizio cha maagizo ya mwalimu shuleni nayaweka pembeni

"Utaleta fimbo nikuchape au nikaitafute mwenyewe" ... hapa nilikuwa nawahi kuitafuta nimpelekee

"Hako kadude kako nilikaona kabla hujakaona, sasa wewe kaendekeze nikuzike ukiwa na kilo mbili"

"Kama baba yako anakudekeza leo mwambie akupikie chakula"

Siku ya harusi yangu "Baba yako hajawahi kunyoosha mkono wako kanipiga, kama unamheshimu na kumpenda baba yako utafanya kama alivyofanya baba yako. Usimpige mkeo"... nina miaka 18 ya ndoa sijawahi kumpiga bibi yenu Sky Eclat

Ahsante sana mama yangu Matesha. Umenifikisha hapa nilipo... Nakuombea maisha marefu zaidi ili wajukuu zako wa kike waige hekima na busara zako
 
Ww hujapitia huko[emoji16]
Nimepita mkuu, mama yangu mpole ila alikuwa akiamua kukuamshia mziki ilikuwa sio poa. Kuna wakati alikuwa ananisema hadi najisemea moyoni kuwa 'kuanzia leo sikuiti mama na wewe siyo mama yangu, mama yangu hawezi kunisema hivi'. Nina kama mwaka tangu niondoke nyumbani kwa harakati za kimaisha, kila mara ananipigia simu kuwa amenimiss sana. Natamani nirudi nikamuone ila ndo hivyo tena..

Mungu wabariki wamama wote.
 
unaingia ingia kwenye hayo mashimo peku, unajua aliyafungua nani? acha upuuzi wako.

jitahidi sana shuleni, hela yenyewe hii ya kunyang'anyana na kaka zako
 
Hapana mkuu skupata asee hayo ndio yalikua maneno yake akiona mtaani mtu kapewa mimba ananambia umeiona faida ya kucheza na wanaume mwenzio kishahitim sasa wewe usipokua makini haya na mwenzio mama ake kamruhusu analea mjukuu mimi utajikuna upele hahahahhaha kwenye kunifundisha kupika nakumbuka nikapika majani ya kunde nkkadhani kama matembele nikaweka limao alinambia nataka ukae chini uile uimalize hiyo mboga niliila kwa kweli
[emoji3][emoji3][emoji3] umetisha boss. Majani kunde na ndimu.

Eehhh ukala yoote
 
"Mbwa mzee hafundishwi sheria, nimesema utafanya kama nilivyosema" hapa kisingizio cha maagizo ya mwalimu shuleni nayaweka pembeni

"Utaleta fimbo nikuchape au nikaitafute mwenyewe" ... hapa nilikuwa nawahi kuitafuta nimpelekee

"Hako kadude kako nilikaona kabla hujakaona, sasa wewe kaendekeze nikuzike ukiwa na kilo mbili"

"Kama baba yako anakudekeza leo mwambie akupikie chakula"

Siku ya harusi yangu "Baba yako hajawahi kunyoosha mkono wako kanipiga, kama unamheshimu na kumpenda baba yako utafanya kama alivyofanya baba yako. Usimpige mkeo"... nina miaka 18 ya ndoa sijawahi kumpiga bibi yenu Sky Eclat

Ahsante sana mama yangu Matesha. Umenifikisha hapa nilipo... Nakuombea maisha marefu zaidi ili wajukuu zako wa kike waige hekima na busara zako
Hahahaaa shemela wetu umetisha. Hako kadude kako nilikaona kabla yako[emoji3][emoji3]
 
Nimepita mkuu, mama yangu mpole ila alikuwa akiamua kukuamshia mziki ilikuwa sio poa. Kuna wakati alikuwa ananisema hadi najisemea moyoni kuwa 'kuanzia leo sikuiti mama na wewe siyo mama yangu, mama yangu hawezi kunisema hivi'. Nina kama mwaka tangu niondoke nyumbani kwa harakati za kimaisha, kila mara ananipigia simu kuwa amenimiss sana. Natamani nirudi nikamuone ila ndo hivyo tena..

Mungu wabariki wamama wote.
Sure mkuu
 
[emoji3][emoji3][emoji3] umetisha boss. Majani kunde na ndimu.

Eehhh ukala yoote
Ndio nikala yote nitafanya nn mana ningekula kichapo kuna muda alikua akinichapa namwambia nakuja kukusemea kwa baba anambia sasa ukishamwambia mwambie akuweke kwenye mfuko wake wa suruali uende naye kazini hapa nyumbani usishinde hahhahahahaha lakini alhamdulillah Mungu aendelee kuwapa umri hawa wazazi jamani
 
Nimepita mkuu, mama yangu mpole ila alikuwa akiamua kukuamshia mziki ilikuwa sio poa. Kuna wakati alikuwa ananisema hadi najisemea moyoni kuwa 'kuanzia leo sikuiti mama na wewe siyo mama yangu, mama yangu hawezi kunisema hivi'. Nina kama mwaka tangu niondoke nyumbani kwa harakati za kimaisha, kila mara ananipigia simu kuwa amenimiss sana. Natamani nirudi nikamuone ila ndo hivyo tena..

Mungu wabariki wamama wote.

Rudi kamuone mzazi..harakati hazina mwisho..mimi ninaishi nae hapa Dar but kila mwisho wa mwaka naenda home Mpanda kuwasalimia waliobaki kule.
 
Usifikri unasoma uje kutusaidia, hiyo ni kwa faida yako mwenyewe cheza tu.

Usiposoma utaishi maisha magumu sana, shauri yako angalia sana.

Mpira unaocheza utakupeleka wapi endelea utakua kibaka mtaani.

Mtembezi hula miguu yake hakuna chakula hapa nenda ukale ulipokuwa.

Ulipokuwa hukula?
 
Ndio nikala yote nitafanya nn mana ningekula kichapo kuna muda alikua akinichapa namwambia nakuja kukusemea kwa baba anambia sasa ukishamwambia mwambie akuweke kwenye mfuko wake wa suruali uende naye kazini hapa nyumbani usishinde hahhahahahaha lakini alhamdulillah Mungu aendelee kuwapa umri hawa wazazi jamani
Teh teh teh bi maza katisha. Mfukoni tena
 
Usifikri unasoma uje kutusaidia, hiyo ni kwa faida yako mwenyewe cheza tu.

Usiposoma utaishi maisha magumu sana, shauri yako angalia sana.

Mpira unaocheza utakupeleka wapi endelea utakua kibaka mtaani.

Mtembezi hula miguu yake hakuna chakula hapa nenda ukale ulipokuwa.

Ulipokuwa hukula?
Mtembezi hula miguu yake hii ni kwa wacheza mpira chandimu[emoji3][emoji3][emoji3]
 
"Wewe kamanda wa uchafu njoo uoge" daa navidemu vilikuwepo niliaibika sana bimkubwa akikukata jicho lilikuwa lnatoa maelekezo yote bila wageni kujua nn kinaendelea heshima kwako Bi Mkubwa
Hahhahaha mimi mama alikua mkali had basi kuliko baba
 
"Wewe kamanda wa uchafu njoo uoge" daa navidemu vilikuwepo niliaibika sana bimkubwa akikukata jicho lilikuwa lnatoa maelekezo yote bila wageni kujua nn kinaendelea heshima kwako Bi Mkubwa
Hii ya kukata jicho umenikumbusha mbali..kukiwa na wageni ukizngua hakugombi wala kukupiga ila jicho lake tuu utajua umezingua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom