Pundit
JF-Expert Member
- Feb 4, 2007
- 3,733
- 123
Urithi wa Kikwete na haiba iso sababu
Binadamu kwa kawaida hupenda kukumbukwa, hususan kukumbukwa kwa mazuri, au yale wanayotaka yaonekane kuwa mazuri. Nimekuwa nikifikiri kuhusu uongozi wetu, hususan rais wetu Jakaya Mrisho Kikwete na anavyofikiri mchango wake ulivyo seuze atakumbukwaje katika taifa letu.
Kama wana JF wengi wanaosoma michango yangu wanavyojua Kikwete si mtu niliyemtaka kuwa rais wa Tanzania, si mwaka 1995 wala muda mwingine wowote. Lakini katika kudekeza falsafa ya kupenda kuwa mtu wa matumaini na kulazimisha kuwa kila binadamu ana haiba, haiba ambayo hata mtu asiye na uwezo wa kuongoza au mfisadi inamfanya asiweze kuachia mambo yaendelee kutapanywa bila maangalizi, na hivyo kusababisha maangamizi. Haiba hii, kwa maneno mengine ikijulikana kama haya, soni, adabu na amneno mengine kama hayo ni moja kati ya vitu vinavyomtofautisha binadamu na mnyama.Kwa bahati mbaya kabisa, naona rais wetu hana haiba, woga, heshima, adabu wala haya juu ya hili.
Kwamba ameweza kusimama "uso mkavu" (nataka kuamini alikuwa hajajidunga kabla ya kuhutubia bunge, ingawa mara nyingine inaniwia vigumu) na kwa masaa takriban matatu kutoa hotuba iliyojaa upuuzi, na si upuuzi tu bali upuuzi unaojikanganya na kukinzana inaonyesha ni jinsi gani anavyojiamini kwamba hata akijikojolea mbele ya kadamnasi washairi na watunga tenzi watamsifia kuwa "Rais Kikwete aleta maji kwenye ukame". Kabla sijatulia vizuri nasoma ripoti kwamba kweli, bila utani, kuna watu wanataka kuandamana kumuunga mkono, kwa kipi kikubwa alichosema? Kukataa kuwashitaki watuhumiwe ambao ushahidi wa kuwafungulia kesi upo? Kushindwa kutoa uongozi katika suala la muungano na Zanzibar? Kuonyesha kutokuwa na imani na mfumo wa mahakama wake yeye mwenyewe?
Unahitaji ngozi ya mamba na upofu wa macho ili kuwa Kikwete.Kama uongozi ni kuwa kichwa ngumu basi rais tunaye.Hivi Kikwete anawezaje kuwaangalia watu machoni? Au kama alivyosema mwenyewe katika hotuba yake, kwamba anaweza kuamuru chochote kifanyike na kikafanyika, anajua kuwa karibu kila mtu anajua ukweli lakini yeye kwa sababu ni rais ana nguvu ya kuupindisha ukweli? Hili alilosema linaweza kuonekana dogo lakini linaweza kuwa ni njia nzuri ya kutuonyessha jinsi gani Kikwete anaamini katika ubeberu wa mabavu ya "Mshindi anachukua chote" na "Ninyi raia tu hamna usemi, mimi ndiye rais mwenye uwezo wote!"
Hili linatuleta katika swali lingine. Hivi kwa nini Kikwete atake kuupindisha ukweli? Huu ulikuwa ni wakati mzuri sana kwake wa kuonesha Watanzania milioni kadhaa waliomchagua kuwa hawakufanya makosa.Lakini badala yake anaendelea kuficha ugonjwa huku akijua mauti yatamuumbua (this is sadly true literally and metaphorically, a president with a nature to hide his own auilment will carry that into his functions and sweep wrongdoings under the carpet, burying his head in the sand like that naïve Australian Ostrich, hoping that what he does not see will not harm him!).Kwa kweli mimi sikutegemea mengi kutoka kwa Kikwete, lakini bado ningependa kuona mimi ndiye niliyekosea katika kumhukumu Kikwete mapema kuliko kumuona Kikwete anakosea katika swala linalohusu kukubalika kwake na imani ya wananchi kiujumla, mali ya umma na hata usalama wa taifa letu.
Kwa nini wananchi tusiamini kuwa Kikwete pamoja na rafiki zake wa karibu kabisa wanahusika na uozo huu wa EPA? Hivi kweli unataka kuniambia kuwa kama wanaohusika wangekuwa wakalamba wa kawaida tu walioweza kujua ujanja wa kufyonza hela BOT Kikwete angekuwa na simile hii? Kwa nini Kikwete hataki kufanya mkondo wa sheria ufuatwe? Katika nchi inayompa rais madaraka makubwa sana kama alivyosema yeye mwenyewe, kuna nafasi kuwa hata kama haya mambo yakifika mahakamani (if ever) basi hatua hizi za rais kutetea sana hawa watuhumiwa zitafanya hata vyombo vya sheria vifanye kazi kwa kuogopa.Nina mashaka kwamba hata kama sarakasi hizi zitafika mahakamani watakaoshitakiwa watakuwa wapambe tu na "wakubwa" wenyewe wataendelea kutanua katika mahekalu na mashangingi yao.
Rais Kikwete anatuachia urithi gain? Hana hata uwezo wa kufikiri na kuona kwamba atakuja kuwa rais asiyekuwa na lolote la kukumbukiwa? Nyerere pamoja na mapungufu mengi ni muasisis wa Tanzania, Mwinyi pamoja na laisez-faire yake alisaidia nchi kutoka katika kufunga mkanda na akasimamia mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa. Hata Mkapa na ufisadi wake anaodaiwa aliurudisha mfumuko wa bei chini na kuanza kukusanya kodi.
Kikwete atatokaje kama mwanzo ndio huu? Wengi wa waliokuwa na matumaini wanaanza kuishiwa na sababu za kuendeleza kutumainia zinabaki miujiza.
Ngoja tumuweke Kikwete katika mizani ya uongozi bora kama walivyoiweka wajuzi tangu enzi. Hivi Kikwete anaweza kusema ana- inspire watu? Kwa kazi gani anayoifanya? Sana sana anavunja matumaini yote ya Watanzania juu ya uongozi wao.
Hivi Kikwete anaweza kusema kuwa hayumbishwi na tamaa jitaihada ya power? Nikimuangalia naona kama kuna kitu pekee alichofanikiwa katika maisha yake ni kutafuta na kuipata hiyo power, ingawa inaonekana hiyo haikuwa njia yake katika kufanya vitu vikubwa zaidi, alichotaka ni kupata uongozi mkubwa kabisa katika Tanzania, power, baada ya hapo hakujua na wala hana mpango afanye nini! Ukiwa unataka kuwa kiongozi tu, bila ya kuwa na ajenda, unataka ukubwa tu, ni vigumu kuwa na principle za kukuzuia kuchukua rushwa za WaIran na kina Rostam Aziz, ni vigumu kuiba hela benki kuu kwa kisingizio cha "usalama wa Taifa" ni vigumu pia kuwashitaki watuhumiwa ambao ushahidi wa wazi upo. Unaopgopa kuwa ukitingisha hili jahazi unaweza kukosa usukani na mlo wako ati!
Kuna watu wamesema kwamba moja ya matatizo ya mifumo ya demokrasia changa ni kwamba uchaguzi wa nani anakuwa kiongozi unatoka juu kuja chini. Watanzania hawamchagui rais, watu wachache wa CCM wanamchagua mgombea urais kwa tiketi ya CCM ambaye kwa hali ya kisiasa ya sasa ndiye anakuwa kama tayari rais hata kabla ya uchaguzi.Kwa hiyo ukiweza kuwafanya watu wachache wa CCM wakuchague unakuwa rais hata kama wewe ni bongolala ambaye hujafanya chochote kama Kikwete.
Kikwete amejionyesha kuwa na tabia hizi hatari kwa kiongozi yeyote kama zilivyotajwa na Van Hooser.
1. Kukosa nidhamu
Ni wazi hana nidhamu. Anakosa nidhamu katika kitu kidogo kama kutumia Kiswahili fasaha katika hotuba ya bunge. Kuna Member ameanzisha thread kuhusu hili. Sitegemei rais awe na nidhamu katika mambo makubwa kama hana nidhamu katika mambo madogo. Ukimsikiliza anavyosema kwamba rais anaweza kuamua mtu yeyote afungwe na kafungwa bila sababu unamsikia mtu asiye na nidhamu kwa Watanzania. Hili jambo la rais kuwa na nguvu sana ni la aibu, na si la kujivunia na kulitangaza, wenzake wote kina Nyerere mpaka Mkapa, ambao walikuwa na nguvu kuliko yeye hawajawahi kulisema wazi wazi hivi. Kikwete hana nidhamu.
2. Kutokuwa na maamuzi mazuri
Kuanzia anavyo mishandle maswala ya ufisadi mapaka teuzi zake Kikwete anajionyesha hana maamuzi mazuri.Ni kama mtu ambaye amezoea kufanyiwa maamuzi makubwa nay eye ni mtekelezaji tu na siku moja amejikuta yeye ndiye muamuzi. Atakalia maswala bila maamuzi, atakapofika sehemu ambapo ni lazima kufanya maamuzi ataongeza muda (EPA) au kutoa kauli zenye kutokuwa na maana kwa sababu zinakinzana (Zanzibar)
3. Kutojali shida za wenzake / wananchi.
Mtu anayeweza kuachia wezi wa mabilioni wakae kwa raha mustarehe kwa kisingizio cha "Haki za Binadamu" wakati wananchi wako hohehahe, na wengine wanafungwa katika jela zisizo za kibinaabamu na wala hajasema kitu kuhusu "Haki za binadamu". Inaonekana hizi "Haki za binadamu" si za binadamu wote ni za wakubwa na wenye hela tu.
4. Kuwa mkuda sana au mpole sana.
Kikwete anabwaka sana lakini hana matendo.Kila siku anatoa maonyo na makaripia bila ufuatiliaji.Mwisho wake anakuwa ni kama yule mzazi ambaye wanawe wanajua wazi kuwa baba/ mama akikuona unafanya kitu asichopenda atakwambia tu "hii iwe mara yako ya mwisho" bila lolote kutokea. Kwa nini watu wasigide bila kuogopa. In a way this is bigger than ruksa.
5. Kuwa myabisi,mjivuni na kutojali.
Kikwete anasema wazi kuwa Watanzania nyie maskini hamna hela, serikali haihitaji michango yenu tutakuja kutafutana lawama tu. Huu ni mfano mmoja tu ambapo amechanganya uyabisi (being cold).Myabisi kwa sababu hakuguswa na jinsi gain maneno yale yangewafanya Watanzania wafikiri. Kutojali (aloofness) hakujali kwa sababu kama angejali asingesema maneno yaliyokosa hekima na heshima kama hayo.Mjivuni (arrogant) kwa sababu anajiona yeye ndiye yeye na nyie wengine hamna kitu, akisahau kuwa kawekwa pale kwa dhamana tu ya wananchi.
6. Kufanya mengi na kuongoza kidogo.
Kikwete yuko kila sehemu, AU, Comoro, Uingereza, Marekani, anzindua tume hii au ile kila siku, lakini ukiangalia anachoongoza ni nini unakuta karibu kabisa na sifuri. Anafungua shule nyingi lakini hazina walimu. Anaenda kufungua daraja ambalo halijakamilika. Anaunda tume ya kuwashikisha adabu mafisadi halafu analeta siasa na pardon ambayo hata haijaombwa. Anafanya mengi lakini haongozi hata kidogo.
7. Kuleta picha ya upendeleo.
Kuanzia habari ya mtandao vs the rest of CCM, CCM vs wapinzani, mafisadi wakubwa vs vibaka wadogo, you name it. Kikwete anapanda mbegu ya mgawanyiko kwa kudekeza picha ya upendeleo.
8. Kuhadaa imani ya Watanzania
Kikwete amekuwa mtu ambaye ameweza kufuja imani kubwa aliyoonyweshwa na Watanzania baada ya kuchaguliwa kwa ushindi wa "Tsunami" sasa anafanya mambo tofauti na alivyotegemewa, tofauti na ahadi na kiapo chake, tofauti na ahadi zake, ilani ya uchaguzi, miiko ya uanachama na uongozi wa CCM.
9. Kutokuwa na uwezo wa kufikiri mpango mkubwa
Kikwete hana "master plan" wala "strategic thinking". Kila kitu kinakwenda ama kwa ulimbwende tu au kwa mtindo wa zimamoto.Watu wanaotegemea kupata uongozi kutoka kwake serikalini wanabaki kushangaa na sarakasi kavu anazopiga kila kukicha.
10. Kuweka wafanyakazi wasioweza/ stahili kazi.
Viongozi wazuri wote wanajua umuhimu wa kuwa na timu nzuri katika kufanikisha mambo.Kikwete inaonekana kama at all anataka kufanya vizuri basi anataka kufanya hivyo kwa bahati nasibu. Teuzi zake zinachekesha sana, kuanzia vihiyo walioibia vyeti kutoka vyuo vya kubabia na "vinu vya stashahada" mpaka rafiki zake waliomsaidia katika kampeni zake chafu za urais. Watu hawana integrity na hawana hata nguvu za kumshauiri vizuri, matokeo yake kila mtu anayemzunguka ni "Yes man" ambaye hawezi kuwa tayari kuingiza kitumbua mchanga, au kufanya kibarua kiote majani kwa kumwambia ukweli rais, matokeo yake ndiyo utasikia "Kikwete anatisha" au watu wanarubuniwa na wapambe wake kuanzisha maandamano ya kumsifu. Mfalme yuko uchi lakini kila mtu anasifu joho lake, panya wanabishana, nani amfunge paka kengele. Labda Spika Sitta, ambaye naye hayuko above reproach kwenye ufisadi, kwa kumsema juzi baada ya hotuba atakuwa ameleta chachu mpya.
11 Kutotaka kubadilika.
Inawezekana wakati wa kina Nyerere Tanzania rais alikuwa ni mungumtu na chama kilishika hatamu.Mambo haya hayapo tena na si ajabu kwa mwendo huu wa shingo kavu na kichwa ngumu wa Kikwete, si watu wa mijini tu na wasomi watashtuka. Wanasema ukila na kipofu usimshike mkono, uinaonekana Kikwete anajisahau sana na kufikiri watanzania hawawezi kufanya lolote nay eye ataendelea kula bila kujali kama anawashika mkono au la. Ile hotuba yake ya kuwakingia kifua mafisadi ilikuwa ni kuwashika mkono hata wale vipofu wasiojua nini kinaendelea.Kwa kutokubali kubadilika, Kikwete anasaidia maendeleo ya vuguvugu la mapinduzi Tanzania.Si haba ndugu yangu Mchungaji Kishoka alisema "Thank God for Kikwete". Ni kauli tata kidogo, lakini kama unapata rais fisadi anayejificha ficha inawezekana kabisa watu wasijue na akaendeleza ufisadi bila matatizo, uzuri wa Kikwete anakwenda bungeni na kuwakingia kifua kabisa mafisadi watu wote muone. Anawaambia mafisadi wake "Msiogope kuitwa mafisadi". Kwa nini wasiompenda wasishukuru mungu kwa kuwapa juha majununi?
12. Kutoheshimu utawala wa sheria, taratibu za uongozi, manifesto na katiba
Kikwete anajionyesha kufanya mambo kiholela bila kufuata misingi ya uongozi bora na utawala wa sheria.Kutokana na kujiona "mshindi" anayeweza kufanya chochote bila backlash yeyote kutoka kwa Watanzania, Kikwete anashindwa kuonyesha uongozi wa sheria.Kutokana na mfano huu auonyeshao, na pia kutokana na teuzi zake dhaifu, baraza lake la mawaziri limejaa misuguano ambayo inaleta picha mbaya kwa wananchi.Ikiwa mawaziri na kiongozi wao wanashindwa.
13. Kuweka mipaka na misimamo isiyo wazi.
Kikwete hakupanda ngazi kwa uchapa kazi au uwezo.Kikwete si kipanga au "policy wonk". Huyu rais wetu wa sasa amepanda ngazi kwa hadaa, kujifaragua na kujipendekeza kwa wakubwa wake. Mtu anayepanda ngazi kwa jinsi hii hawezi kuwa mtu wa "principle", mtu wa aina hii ni mtu wa kuficha makucha na kwenda na upepo.Kwa sababu hii Kikwete amejenga tabia ya kuwa vague, anataka kuila keki yake halafu abaki nayo mezani.Hii ndiyo sababu ameshindwa kulitolea msimamo swala la Zanzibar na kutoa kauli tata ambayo inataka kuwafurahisha watu wote.Kikwete hafahamu kuwa kwa kutaka kuwafurahisha watu wote atakuwa hajamfurahisha yeyote. Ukiongelea Zimbabwe au Zanzibar rais wetu hawezi kuwa kiongozi kwa sababu hayuko tayari kuwa na msimamo.
14. Kutoweza kuchukua hatua pale anapotakiwa.
Pengine zaidi ya swala lingine lolote hili swala la EPA limeonyesha rais asiyeweza kuchukua hatuapale inapotakiwa.Kikwete ni sawa na baba mwenye nyumba alieambiwa na watoto "Baba, tunasikia harufu ya gesi, inawezekana mtungi wa gesi ya kupikia unavuja" akaendelea kulala, akaambiwa "Baba, kuna cheche kwenye nyaya za umeme jikoni" bado akaendelea kulala, akaambiwa baba sasa zile cheche zimechanganyika na gesi na kufanya moto mdogo, bado akalala, na sasa hatima yake moto umeshaanza kuwaka jikoni, bado amelala. Anasubiri nini? Anasubiri moto umuwakie mbele ya mikono yake? Rais wetu kutoweza kuchukua hatua pale anapotakiwa na pacha wake kuachilia matatizo kuendelea kutatugharimu sana.
15. Kulewa madaraka
Kikwete anaonekana wazi kuwa mlevi wa madaraka, sio tu anayeweza kufanya lolote bila kuogopa, bali pia anayeweza kusema mbele ya bunge, Watanzania na dunia nzima kwamba anaweza kufanya lolote bila kuogopa. Huu ni wakati mzuri wa kuanzisha kampeni ya kupunguza madaraka ya rais, yale yaliyo rasmi na yasiyo rasmi. Haifai kuwa na urais wenye madaraka mengi kwa sababu hatujui kama kila siku tutapata rais mwenye uwezo wa kutoyumbishwa na vishawishi vya kutumia madaraka vibaya. Noblese Oblige, to whom much is given, much is required, responsibility to protect.Wenye nguvu wawe tayari kuhakikisha hakuna loopholes zitakazoruhusu matumizi mabaya ya madaraka, hii inajumuisha wenye nguvu, na rais yupo juu kabisa katika hawa, kuwa tayari kupunguza nguvu zao, siyo kuja ku "lord it over us" katika hotuba za bunge. Cheo ni dhamana, rais Kikwete anaonekana kusahau hili.
16. Umangimeza
Kama unaongelea kuhusu tume za kuchunguza tume, safari zisizoisha, hotuba za masaa matatu zisizo na mantiki wala kitu kipya na upuuzi mwingine unaofanana na huo, rais Kikwete amejidhihirisha kuwa ni bingwa wa umangimeza, anayejua sana kusema, hapana, anayejua kusema sana bila kutoa msimamo au kuwa na lolote jipya.Amejizolea majina lukuki kutoka "Muungwana" (hataki kuchafua mikono yake kwa matope ya kazi) mpaka kiongozi wa "Ze Comedy" kutokana na jinsi anavyoiendesha nchi.
Ninapomuangalia Kikwete ninajiuliza sana tena na tena, inawezekana kweli Kikwete ana nia nzuri lakini anashindwa kutokana na vitu vilivyo nje ya uwezo wake? Nikimuangalia Waziri Mkuu wa Uingereza Gordon Brown, naona ana matatzo kama ya Kikwete, Gordon Brown kama Kikwete, alikuwa anajiandaa kuwa rais kwa miaka 10.Baada ya miaka yote hiyo inaonekana kama Brown alikuwa mzuri sana katika kujiandaa kuwa Waziri Mkuu lakini baada ya kuupata uwaziri mkuu, hajui cha kufanya.Kikwete anaonekana alikuwa anasubiri kuwa rais kwa miaka kumi, lakini baada ya kupata urais hajui cha kufanya. .Lakini tofauti kubwa kati ya Brown na Kikwete ni kwamba Brown alifanya kazi nzuri sana alivyokuwa Waziri wa Fedha, na ingawa ana matatizo kisiasa, haandikwi vizuri, opinion polls ratings ziko chini sana, lakini Brown hajapata nafasi ya kuwa mbele ya goli na kushindwa kufunga kama alivyo Kikwete. Inawezekana kabisa matatizo ya Brown yanatokana na Waingereza kuchoshwa na chama chake cha Labor na "zero tolerance" ya Waingereza, Kikwete hana tatizo la "zero tolerance" kutoka kwa Watanzania, kama kuna tatizo basi ni "maximum tolerance".
Kwa nini Kikwete anaonekana kutofanya mambo yatakayopalilia ustawi wake kisiasa?
Itaendelea
Binadamu kwa kawaida hupenda kukumbukwa, hususan kukumbukwa kwa mazuri, au yale wanayotaka yaonekane kuwa mazuri. Nimekuwa nikifikiri kuhusu uongozi wetu, hususan rais wetu Jakaya Mrisho Kikwete na anavyofikiri mchango wake ulivyo seuze atakumbukwaje katika taifa letu.
Kama wana JF wengi wanaosoma michango yangu wanavyojua Kikwete si mtu niliyemtaka kuwa rais wa Tanzania, si mwaka 1995 wala muda mwingine wowote. Lakini katika kudekeza falsafa ya kupenda kuwa mtu wa matumaini na kulazimisha kuwa kila binadamu ana haiba, haiba ambayo hata mtu asiye na uwezo wa kuongoza au mfisadi inamfanya asiweze kuachia mambo yaendelee kutapanywa bila maangalizi, na hivyo kusababisha maangamizi. Haiba hii, kwa maneno mengine ikijulikana kama haya, soni, adabu na amneno mengine kama hayo ni moja kati ya vitu vinavyomtofautisha binadamu na mnyama.Kwa bahati mbaya kabisa, naona rais wetu hana haiba, woga, heshima, adabu wala haya juu ya hili.
Kwamba ameweza kusimama "uso mkavu" (nataka kuamini alikuwa hajajidunga kabla ya kuhutubia bunge, ingawa mara nyingine inaniwia vigumu) na kwa masaa takriban matatu kutoa hotuba iliyojaa upuuzi, na si upuuzi tu bali upuuzi unaojikanganya na kukinzana inaonyesha ni jinsi gani anavyojiamini kwamba hata akijikojolea mbele ya kadamnasi washairi na watunga tenzi watamsifia kuwa "Rais Kikwete aleta maji kwenye ukame". Kabla sijatulia vizuri nasoma ripoti kwamba kweli, bila utani, kuna watu wanataka kuandamana kumuunga mkono, kwa kipi kikubwa alichosema? Kukataa kuwashitaki watuhumiwe ambao ushahidi wa kuwafungulia kesi upo? Kushindwa kutoa uongozi katika suala la muungano na Zanzibar? Kuonyesha kutokuwa na imani na mfumo wa mahakama wake yeye mwenyewe?
Unahitaji ngozi ya mamba na upofu wa macho ili kuwa Kikwete.Kama uongozi ni kuwa kichwa ngumu basi rais tunaye.Hivi Kikwete anawezaje kuwaangalia watu machoni? Au kama alivyosema mwenyewe katika hotuba yake, kwamba anaweza kuamuru chochote kifanyike na kikafanyika, anajua kuwa karibu kila mtu anajua ukweli lakini yeye kwa sababu ni rais ana nguvu ya kuupindisha ukweli? Hili alilosema linaweza kuonekana dogo lakini linaweza kuwa ni njia nzuri ya kutuonyessha jinsi gani Kikwete anaamini katika ubeberu wa mabavu ya "Mshindi anachukua chote" na "Ninyi raia tu hamna usemi, mimi ndiye rais mwenye uwezo wote!"
Hili linatuleta katika swali lingine. Hivi kwa nini Kikwete atake kuupindisha ukweli? Huu ulikuwa ni wakati mzuri sana kwake wa kuonesha Watanzania milioni kadhaa waliomchagua kuwa hawakufanya makosa.Lakini badala yake anaendelea kuficha ugonjwa huku akijua mauti yatamuumbua (this is sadly true literally and metaphorically, a president with a nature to hide his own auilment will carry that into his functions and sweep wrongdoings under the carpet, burying his head in the sand like that naïve Australian Ostrich, hoping that what he does not see will not harm him!).Kwa kweli mimi sikutegemea mengi kutoka kwa Kikwete, lakini bado ningependa kuona mimi ndiye niliyekosea katika kumhukumu Kikwete mapema kuliko kumuona Kikwete anakosea katika swala linalohusu kukubalika kwake na imani ya wananchi kiujumla, mali ya umma na hata usalama wa taifa letu.
Kwa nini wananchi tusiamini kuwa Kikwete pamoja na rafiki zake wa karibu kabisa wanahusika na uozo huu wa EPA? Hivi kweli unataka kuniambia kuwa kama wanaohusika wangekuwa wakalamba wa kawaida tu walioweza kujua ujanja wa kufyonza hela BOT Kikwete angekuwa na simile hii? Kwa nini Kikwete hataki kufanya mkondo wa sheria ufuatwe? Katika nchi inayompa rais madaraka makubwa sana kama alivyosema yeye mwenyewe, kuna nafasi kuwa hata kama haya mambo yakifika mahakamani (if ever) basi hatua hizi za rais kutetea sana hawa watuhumiwa zitafanya hata vyombo vya sheria vifanye kazi kwa kuogopa.Nina mashaka kwamba hata kama sarakasi hizi zitafika mahakamani watakaoshitakiwa watakuwa wapambe tu na "wakubwa" wenyewe wataendelea kutanua katika mahekalu na mashangingi yao.
Rais Kikwete anatuachia urithi gain? Hana hata uwezo wa kufikiri na kuona kwamba atakuja kuwa rais asiyekuwa na lolote la kukumbukiwa? Nyerere pamoja na mapungufu mengi ni muasisis wa Tanzania, Mwinyi pamoja na laisez-faire yake alisaidia nchi kutoka katika kufunga mkanda na akasimamia mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa. Hata Mkapa na ufisadi wake anaodaiwa aliurudisha mfumuko wa bei chini na kuanza kukusanya kodi.
Kikwete atatokaje kama mwanzo ndio huu? Wengi wa waliokuwa na matumaini wanaanza kuishiwa na sababu za kuendeleza kutumainia zinabaki miujiza.
Ngoja tumuweke Kikwete katika mizani ya uongozi bora kama walivyoiweka wajuzi tangu enzi. Hivi Kikwete anaweza kusema ana- inspire watu? Kwa kazi gani anayoifanya? Sana sana anavunja matumaini yote ya Watanzania juu ya uongozi wao.
Hivi Kikwete anaweza kusema kuwa hayumbishwi na tamaa jitaihada ya power? Nikimuangalia naona kama kuna kitu pekee alichofanikiwa katika maisha yake ni kutafuta na kuipata hiyo power, ingawa inaonekana hiyo haikuwa njia yake katika kufanya vitu vikubwa zaidi, alichotaka ni kupata uongozi mkubwa kabisa katika Tanzania, power, baada ya hapo hakujua na wala hana mpango afanye nini! Ukiwa unataka kuwa kiongozi tu, bila ya kuwa na ajenda, unataka ukubwa tu, ni vigumu kuwa na principle za kukuzuia kuchukua rushwa za WaIran na kina Rostam Aziz, ni vigumu kuiba hela benki kuu kwa kisingizio cha "usalama wa Taifa" ni vigumu pia kuwashitaki watuhumiwa ambao ushahidi wa wazi upo. Unaopgopa kuwa ukitingisha hili jahazi unaweza kukosa usukani na mlo wako ati!
Kuna watu wamesema kwamba moja ya matatizo ya mifumo ya demokrasia changa ni kwamba uchaguzi wa nani anakuwa kiongozi unatoka juu kuja chini. Watanzania hawamchagui rais, watu wachache wa CCM wanamchagua mgombea urais kwa tiketi ya CCM ambaye kwa hali ya kisiasa ya sasa ndiye anakuwa kama tayari rais hata kabla ya uchaguzi.Kwa hiyo ukiweza kuwafanya watu wachache wa CCM wakuchague unakuwa rais hata kama wewe ni bongolala ambaye hujafanya chochote kama Kikwete.
Kikwete amejionyesha kuwa na tabia hizi hatari kwa kiongozi yeyote kama zilivyotajwa na Van Hooser.
1. Kukosa nidhamu
Ni wazi hana nidhamu. Anakosa nidhamu katika kitu kidogo kama kutumia Kiswahili fasaha katika hotuba ya bunge. Kuna Member ameanzisha thread kuhusu hili. Sitegemei rais awe na nidhamu katika mambo makubwa kama hana nidhamu katika mambo madogo. Ukimsikiliza anavyosema kwamba rais anaweza kuamua mtu yeyote afungwe na kafungwa bila sababu unamsikia mtu asiye na nidhamu kwa Watanzania. Hili jambo la rais kuwa na nguvu sana ni la aibu, na si la kujivunia na kulitangaza, wenzake wote kina Nyerere mpaka Mkapa, ambao walikuwa na nguvu kuliko yeye hawajawahi kulisema wazi wazi hivi. Kikwete hana nidhamu.
2. Kutokuwa na maamuzi mazuri
Kuanzia anavyo mishandle maswala ya ufisadi mapaka teuzi zake Kikwete anajionyesha hana maamuzi mazuri.Ni kama mtu ambaye amezoea kufanyiwa maamuzi makubwa nay eye ni mtekelezaji tu na siku moja amejikuta yeye ndiye muamuzi. Atakalia maswala bila maamuzi, atakapofika sehemu ambapo ni lazima kufanya maamuzi ataongeza muda (EPA) au kutoa kauli zenye kutokuwa na maana kwa sababu zinakinzana (Zanzibar)
3. Kutojali shida za wenzake / wananchi.
Mtu anayeweza kuachia wezi wa mabilioni wakae kwa raha mustarehe kwa kisingizio cha "Haki za Binadamu" wakati wananchi wako hohehahe, na wengine wanafungwa katika jela zisizo za kibinaabamu na wala hajasema kitu kuhusu "Haki za binadamu". Inaonekana hizi "Haki za binadamu" si za binadamu wote ni za wakubwa na wenye hela tu.
4. Kuwa mkuda sana au mpole sana.
Kikwete anabwaka sana lakini hana matendo.Kila siku anatoa maonyo na makaripia bila ufuatiliaji.Mwisho wake anakuwa ni kama yule mzazi ambaye wanawe wanajua wazi kuwa baba/ mama akikuona unafanya kitu asichopenda atakwambia tu "hii iwe mara yako ya mwisho" bila lolote kutokea. Kwa nini watu wasigide bila kuogopa. In a way this is bigger than ruksa.
5. Kuwa myabisi,mjivuni na kutojali.
Kikwete anasema wazi kuwa Watanzania nyie maskini hamna hela, serikali haihitaji michango yenu tutakuja kutafutana lawama tu. Huu ni mfano mmoja tu ambapo amechanganya uyabisi (being cold).Myabisi kwa sababu hakuguswa na jinsi gain maneno yale yangewafanya Watanzania wafikiri. Kutojali (aloofness) hakujali kwa sababu kama angejali asingesema maneno yaliyokosa hekima na heshima kama hayo.Mjivuni (arrogant) kwa sababu anajiona yeye ndiye yeye na nyie wengine hamna kitu, akisahau kuwa kawekwa pale kwa dhamana tu ya wananchi.
6. Kufanya mengi na kuongoza kidogo.
Kikwete yuko kila sehemu, AU, Comoro, Uingereza, Marekani, anzindua tume hii au ile kila siku, lakini ukiangalia anachoongoza ni nini unakuta karibu kabisa na sifuri. Anafungua shule nyingi lakini hazina walimu. Anaenda kufungua daraja ambalo halijakamilika. Anaunda tume ya kuwashikisha adabu mafisadi halafu analeta siasa na pardon ambayo hata haijaombwa. Anafanya mengi lakini haongozi hata kidogo.
7. Kuleta picha ya upendeleo.
Kuanzia habari ya mtandao vs the rest of CCM, CCM vs wapinzani, mafisadi wakubwa vs vibaka wadogo, you name it. Kikwete anapanda mbegu ya mgawanyiko kwa kudekeza picha ya upendeleo.
8. Kuhadaa imani ya Watanzania
Kikwete amekuwa mtu ambaye ameweza kufuja imani kubwa aliyoonyweshwa na Watanzania baada ya kuchaguliwa kwa ushindi wa "Tsunami" sasa anafanya mambo tofauti na alivyotegemewa, tofauti na ahadi na kiapo chake, tofauti na ahadi zake, ilani ya uchaguzi, miiko ya uanachama na uongozi wa CCM.
9. Kutokuwa na uwezo wa kufikiri mpango mkubwa
Kikwete hana "master plan" wala "strategic thinking". Kila kitu kinakwenda ama kwa ulimbwende tu au kwa mtindo wa zimamoto.Watu wanaotegemea kupata uongozi kutoka kwake serikalini wanabaki kushangaa na sarakasi kavu anazopiga kila kukicha.
10. Kuweka wafanyakazi wasioweza/ stahili kazi.
Viongozi wazuri wote wanajua umuhimu wa kuwa na timu nzuri katika kufanikisha mambo.Kikwete inaonekana kama at all anataka kufanya vizuri basi anataka kufanya hivyo kwa bahati nasibu. Teuzi zake zinachekesha sana, kuanzia vihiyo walioibia vyeti kutoka vyuo vya kubabia na "vinu vya stashahada" mpaka rafiki zake waliomsaidia katika kampeni zake chafu za urais. Watu hawana integrity na hawana hata nguvu za kumshauiri vizuri, matokeo yake kila mtu anayemzunguka ni "Yes man" ambaye hawezi kuwa tayari kuingiza kitumbua mchanga, au kufanya kibarua kiote majani kwa kumwambia ukweli rais, matokeo yake ndiyo utasikia "Kikwete anatisha" au watu wanarubuniwa na wapambe wake kuanzisha maandamano ya kumsifu. Mfalme yuko uchi lakini kila mtu anasifu joho lake, panya wanabishana, nani amfunge paka kengele. Labda Spika Sitta, ambaye naye hayuko above reproach kwenye ufisadi, kwa kumsema juzi baada ya hotuba atakuwa ameleta chachu mpya.
11 Kutotaka kubadilika.
Inawezekana wakati wa kina Nyerere Tanzania rais alikuwa ni mungumtu na chama kilishika hatamu.Mambo haya hayapo tena na si ajabu kwa mwendo huu wa shingo kavu na kichwa ngumu wa Kikwete, si watu wa mijini tu na wasomi watashtuka. Wanasema ukila na kipofu usimshike mkono, uinaonekana Kikwete anajisahau sana na kufikiri watanzania hawawezi kufanya lolote nay eye ataendelea kula bila kujali kama anawashika mkono au la. Ile hotuba yake ya kuwakingia kifua mafisadi ilikuwa ni kuwashika mkono hata wale vipofu wasiojua nini kinaendelea.Kwa kutokubali kubadilika, Kikwete anasaidia maendeleo ya vuguvugu la mapinduzi Tanzania.Si haba ndugu yangu Mchungaji Kishoka alisema "Thank God for Kikwete". Ni kauli tata kidogo, lakini kama unapata rais fisadi anayejificha ficha inawezekana kabisa watu wasijue na akaendeleza ufisadi bila matatizo, uzuri wa Kikwete anakwenda bungeni na kuwakingia kifua kabisa mafisadi watu wote muone. Anawaambia mafisadi wake "Msiogope kuitwa mafisadi". Kwa nini wasiompenda wasishukuru mungu kwa kuwapa juha majununi?
12. Kutoheshimu utawala wa sheria, taratibu za uongozi, manifesto na katiba
Kikwete anajionyesha kufanya mambo kiholela bila kufuata misingi ya uongozi bora na utawala wa sheria.Kutokana na kujiona "mshindi" anayeweza kufanya chochote bila backlash yeyote kutoka kwa Watanzania, Kikwete anashindwa kuonyesha uongozi wa sheria.Kutokana na mfano huu auonyeshao, na pia kutokana na teuzi zake dhaifu, baraza lake la mawaziri limejaa misuguano ambayo inaleta picha mbaya kwa wananchi.Ikiwa mawaziri na kiongozi wao wanashindwa.
13. Kuweka mipaka na misimamo isiyo wazi.
Kikwete hakupanda ngazi kwa uchapa kazi au uwezo.Kikwete si kipanga au "policy wonk". Huyu rais wetu wa sasa amepanda ngazi kwa hadaa, kujifaragua na kujipendekeza kwa wakubwa wake. Mtu anayepanda ngazi kwa jinsi hii hawezi kuwa mtu wa "principle", mtu wa aina hii ni mtu wa kuficha makucha na kwenda na upepo.Kwa sababu hii Kikwete amejenga tabia ya kuwa vague, anataka kuila keki yake halafu abaki nayo mezani.Hii ndiyo sababu ameshindwa kulitolea msimamo swala la Zanzibar na kutoa kauli tata ambayo inataka kuwafurahisha watu wote.Kikwete hafahamu kuwa kwa kutaka kuwafurahisha watu wote atakuwa hajamfurahisha yeyote. Ukiongelea Zimbabwe au Zanzibar rais wetu hawezi kuwa kiongozi kwa sababu hayuko tayari kuwa na msimamo.
14. Kutoweza kuchukua hatua pale anapotakiwa.
Pengine zaidi ya swala lingine lolote hili swala la EPA limeonyesha rais asiyeweza kuchukua hatuapale inapotakiwa.Kikwete ni sawa na baba mwenye nyumba alieambiwa na watoto "Baba, tunasikia harufu ya gesi, inawezekana mtungi wa gesi ya kupikia unavuja" akaendelea kulala, akaambiwa "Baba, kuna cheche kwenye nyaya za umeme jikoni" bado akaendelea kulala, akaambiwa baba sasa zile cheche zimechanganyika na gesi na kufanya moto mdogo, bado akalala, na sasa hatima yake moto umeshaanza kuwaka jikoni, bado amelala. Anasubiri nini? Anasubiri moto umuwakie mbele ya mikono yake? Rais wetu kutoweza kuchukua hatua pale anapotakiwa na pacha wake kuachilia matatizo kuendelea kutatugharimu sana.
15. Kulewa madaraka
Kikwete anaonekana wazi kuwa mlevi wa madaraka, sio tu anayeweza kufanya lolote bila kuogopa, bali pia anayeweza kusema mbele ya bunge, Watanzania na dunia nzima kwamba anaweza kufanya lolote bila kuogopa. Huu ni wakati mzuri wa kuanzisha kampeni ya kupunguza madaraka ya rais, yale yaliyo rasmi na yasiyo rasmi. Haifai kuwa na urais wenye madaraka mengi kwa sababu hatujui kama kila siku tutapata rais mwenye uwezo wa kutoyumbishwa na vishawishi vya kutumia madaraka vibaya. Noblese Oblige, to whom much is given, much is required, responsibility to protect.Wenye nguvu wawe tayari kuhakikisha hakuna loopholes zitakazoruhusu matumizi mabaya ya madaraka, hii inajumuisha wenye nguvu, na rais yupo juu kabisa katika hawa, kuwa tayari kupunguza nguvu zao, siyo kuja ku "lord it over us" katika hotuba za bunge. Cheo ni dhamana, rais Kikwete anaonekana kusahau hili.
16. Umangimeza
Kama unaongelea kuhusu tume za kuchunguza tume, safari zisizoisha, hotuba za masaa matatu zisizo na mantiki wala kitu kipya na upuuzi mwingine unaofanana na huo, rais Kikwete amejidhihirisha kuwa ni bingwa wa umangimeza, anayejua sana kusema, hapana, anayejua kusema sana bila kutoa msimamo au kuwa na lolote jipya.Amejizolea majina lukuki kutoka "Muungwana" (hataki kuchafua mikono yake kwa matope ya kazi) mpaka kiongozi wa "Ze Comedy" kutokana na jinsi anavyoiendesha nchi.
Ninapomuangalia Kikwete ninajiuliza sana tena na tena, inawezekana kweli Kikwete ana nia nzuri lakini anashindwa kutokana na vitu vilivyo nje ya uwezo wake? Nikimuangalia Waziri Mkuu wa Uingereza Gordon Brown, naona ana matatzo kama ya Kikwete, Gordon Brown kama Kikwete, alikuwa anajiandaa kuwa rais kwa miaka 10.Baada ya miaka yote hiyo inaonekana kama Brown alikuwa mzuri sana katika kujiandaa kuwa Waziri Mkuu lakini baada ya kuupata uwaziri mkuu, hajui cha kufanya.Kikwete anaonekana alikuwa anasubiri kuwa rais kwa miaka kumi, lakini baada ya kupata urais hajui cha kufanya. .Lakini tofauti kubwa kati ya Brown na Kikwete ni kwamba Brown alifanya kazi nzuri sana alivyokuwa Waziri wa Fedha, na ingawa ana matatizo kisiasa, haandikwi vizuri, opinion polls ratings ziko chini sana, lakini Brown hajapata nafasi ya kuwa mbele ya goli na kushindwa kufunga kama alivyo Kikwete. Inawezekana kabisa matatizo ya Brown yanatokana na Waingereza kuchoshwa na chama chake cha Labor na "zero tolerance" ya Waingereza, Kikwete hana tatizo la "zero tolerance" kutoka kwa Watanzania, kama kuna tatizo basi ni "maximum tolerance".
Kwa nini Kikwete anaonekana kutofanya mambo yatakayopalilia ustawi wake kisiasa?
Itaendelea