Wazazi si kila filamu ya katuni inawafaa watoto, tuwe makini

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566
1679570973415.png

Salaam ndugu zangu,

Katuni imekuwa ni michezo/ Filamu muhimu sana katika kusaidia malezi na kuwafariji watoto wetu. Baadhi ya katuni maarufu ni kama Tom and Jerry, Moana, Zootopia, Luca, Sing, Rango na nyinginezo.

Ni kweli kwamba filamu nyingi za katuni zimeundwa kwa ajili ya watoto. Lakini kutokana na kukua kwa teknolojia filamu hizi zimevamiwa na zimekuwa si zenye maudhui ya kitoto pekee. Kuna katuni ambazo zina maudhui ya ngono, matumizi ya lugha ya matusi au mafundisho ya mapenzi ya jinsia moja n.k mfano Familyguy na Bad cat.

Hivyo, pamoja na uzuri na mchango wa katuni katika kulea na kutengeneza furaha za watoto wetu, tunapaswa kuangalia rating ya filamu hizo, kusoma maoni na ushauri kutoka kwa wataalamu kisha kuchagua kilicho bora.
 
Salaam ndugu zangu,

Katuni imekuwa ni michezo/ Filamu muhimu sana katika kusaidia malezi na kuwafariji watoto wetu. Baadhi ya katuni maarufu ni kama Tom and Jerry, Moana, Zootopia, Luca, Sing, Rango na nyinginezo.
Samahani ndugu waweza orodhesha baadhi ya hizo katuni unazozifahamu zenye maudhui yasiyo rafiki kutazamwa na watoto kama hutajali.
 
Samahani ndugu waweza orodhesha baadhi ya hizo katuni unazozifahamu zenye maudhui yasiyo rafiki kutazamwa na watoto kama hutajali.
Kingine zingatia PG yake inakupa umri kabisa wa mtu wa kuangalia. Under 5 wote wanapaswa kuangalia zaidi vitu vya kuwafundisha kuzungumza, kuchora, kusoma, kutambua vitu.

Kwa kifupi kabla ya kumruhusu mtoto aangalie katuni YOYOTE ihakiki kwanza. Dunia imekuwa ya ajabu sana kuna agenda za ajabu sana zinaingizwa siku hizi humo humo kwenye za kusoma na kuandika au kuimba.
 
Kingine zingatia PG yake inakupa umri kabisa wa mtu wa kuangalia. Under 5 wote wanapaswa kuangalia zaidi vitu vya kuwafundisha kuzungumza, kuchora, kusoma, kutambua vitu. Kwa kifupi kabla ya kumruhusu mtoto aangalie katuni YOYOTE ihakiki kwanza. Dunia imekuwa ya ajabu sana kuna agenda za ajabu sana zinaingizwa siku hizi humo humo kwenye za kusoma na kuandika au kuimba.
Ahsante sana well noted ndugu......
 
Halafu unajua kuna kitu inabidi mfahamu. Hawa watengeneza hizi katuni wanazozipa maudhui ya kiutu uzima wengi huwa wanazitengeneza kwaajiri ya audience ya wale watu wazima ambao wanapenda katuni ndio maana katuni zinakuwa na materials ambazo si za kitoto.

Shida inakuja ni namna masoko yanafanyika kwenye hizi products. Mfano ukitazama vitu kama PlayStation games, kwa vitu wanafanya mle ndani ni dhahiri mtumiaji anatakiwa kuwa at least miaka 18 au zaidi maana zile games sio za kuchezwa na watoto chini ya miaka 18.

So nadhani katuni kama Family guy, American Dad, etc hawa watengenezaji wanakuwa na audience wameitarget ila ilishafika sokoni sasa hiyo bidhaa sababu ya mazingira yetu ya kijamii kuna sehemu watoto wanazitazama sababu hakuna parental control wala guardians.

Kimsingi tutengeneze utaratibu wa kuwalimit watoto wetu vitu wanavyotazama kama vile tunavyowalimit kuvuta sigara, kuonja beer, au kufanya vitendo vya ngono wakiwa wadogo.

Kuwa mzazi na mlezi si kazi ndogo. Tupambane.
 
Bad Cat Tena Ile Namba Moja Ina lugha Za Matusi Sana Kama Mzazi Haupo Karibu Na Limoti Ni Mbaya Sana

Sema Sijui Niseme BAHATI Nzuri Au Mbaya Watoto Wetu Wengi Hawajui English Hususani Katika Lugha Za Matusi Kwa HIYO Hata Likitukanwa Tusi Halifuatilii Sana Mana Yeye Ana focus Kwenye Kuangalia Picha TU.
 
Halafu unajua kuna kitu inabidi mfahamu. Hawa watengeneza hizi katuni wanazozipa maudhui ya kiutu uzima wengi huwa wanazitengeneza kwaajiri ya audience ya wale watu wazima ambao wanapenda katuni ndio maana katuni zinakuwa na materials ambazo si za kitoto.


Kuwa mzazi na mlezi si kazi ndogo. Tupambane.
i agree with the terms and conditons kwa hili.................
 
nashukuru ngoja nizipitie kwenye ''VAR'' yangu kabla ya kumwachia ankoli wangu aziangalie.....
Makinika na cartoon zote za Disney channel nk.

Kuna cartoon inaitwa Little demon, hii inawafunza watoto uchawi, isipokuwa makini mtoto wako anaweza Anza kuwanga bila we kujua, mtoto akiangalia cartoon za aina hii, usiku hutoka mapepo kupitia tv Yako na kumuingia mtoto kupitia NDOTO sababu umrfungua mlango.

Channel hiyo zipo cartoon zenye kufundisha USHOGA, baada ya muda utaona mtoto akianza kupractice Kwa wenzie, darasa linatoka kwenye tv.

Ibilisi alipoona wazazi hawana muda na watoto, anawafundisha Yeye kupitia cartoon.

Kwa Hali ilivyo, ni Bora utazame kwanza wewe cartoon hizo ujue maudhui.
 
Hii dini inataka kuifanya hii dunia iwe sehemu ya kutisha kuishi,kila kitu imekataza,mbona hii dini ingine hatuhangaiki na nyie,mnataka kujivika ukiranja wa dunia hii wakati uwezo hakuna
 
Samahani ndugu waweza orodhesha baadhi ya hizo katuni unazozifahamu zenye maudhui yasiyo rafiki kutazamwa na watoto kama hutajali.
Utamaliza Katuni zote? Cha muhimu hakikisha una access ya internet mara nyingi, kila filamu ina rating kuna rating kama U, PG, 12, 18 etc.

Filamu zenye rating za U ina maana yoyote anaweza kuangalia.

PG ni miaka 8 kuendelea ila mzazi inabidi awepo ama wewe mwenyewe uamue aangalie ama asiangalie, kwenye pg kunaweza kuwa na maswali ambayo wewe umjibu mtoto,

Zilizobakia hizo za no 18, 16, 13 etc weka mbali na watoto.

Kwa uhakika zaidi google jina la filamu na neno parental review kwa mbele.
 
Makinika na cartoon zote za Disney channel nk.

Kuna cartoon inaitwa Little demon, hii inawafunza watoto uchawi, isipokuwa makini mtoto wako anaweza Anza kuwanga bila we kujua, mtoto akiangalia cartoon za aina hii, usiku hutoka mapepo kupitia tv Yako na kumuingia mtoto kupitia NDOTO sababu umrfungua mlango.

Channel hiyo zipo cartoon zenye kufundisha USHOGA, baada ya muda utaona mtoto akianza kupractice Kwa wenzie, darasa linatoka kwenye tv.

Ibilisi alipoona wazazi hawana muda na watoto, anawafundisha Yeye kupitia cartoon.

Kwa Hali ilivyo, ni Bora utazame kwanza wewe cartoon hizo ujue maudhui.

Utamaliza Katuni zote? Cha muhimu hakikisha una access ya internet mara nyingi, kila filamu ina rating kuna rating kama U, PG, 12, 18 etc.

Filamu zenye rating za U ina maana yoyote anaweza kuangalia.

PG ni miaka 8 kuendelea ila mzazi inabidi awepo ama wewe mwenyewe uamue aangalie ama asiangalie, kwenye pg kunaweza kuwa na maswali ambayo wewe umjibu mtoto,

Zilizobakia hizo za no 18, 16, 13 etc weka mbali na watoto.

Kwa uhakika zaidi google jina la filamu na neno parental review kwa mbele.
Sawa nimekuelewa nipo naperuzi hapa
 
Msiangalie katuni, rudini kwenye UMIZIMU na UNYAGO.

Watoto wote wapelekwe unyagoni wakajifunze kulea mume. Hiyo ndio safi.

Katuni hazina maadili, watoto wetu wanajifunza denda.

Denda ni mbaya, inahatarisha uchumi wa nchi.
 
Back
Top Bottom