Mkuu, any 2 substances mixed together can be separated. Kwaio hakuna icho unachosema kuwa eti huwezi kuseparate new compound formed.
Mfano, H na O. kwa pamoja zimeleta new compound ambayo ni H20, hii ni new compound na inaweza kuwa separated bila wasiwasi.
Tukichukulia hivo unavotaka wewe, katika Muungano wetu huu, element moja tu ndio imepotea, nayo ni Tanganyika, lakini element ya Zanzibar ipo palepale. Tanganyika haina muhimili wowote wa dola unaojua wewe, hauna rais, hauna bunge, hauna kikosi, kikubwa ina mawaziri ambao hawana rais!
Inatakiwa Zanzibar iwe na mamlaka kamili, na tanganyika iwe koloni letu kwa sababu hamuna serikali. Huu Muungano ukivunjika, Zanzibar tayari inaserikali na tanganyika itabaki taharuki, hajulikani rais nani wala waziri mkuu nani, jaji mkuu hajulikani, na ndio maana mnaung'ang'ania huu mungano kwa hofu ya kuchafuka kwa Tanganyika. Hata waziri mkuu hamuna, vyama vya upinzani vitajitokeza na kujipa mamlaka na fujo kuzuka. Majirani zetu Kenya, Uganda, rwanda na Burundi baada ya kuona kuwa Muungano umevunjika na tanganyika kutokuwa na serikali, basi kila mmoja atajimegea kipande chake kwenye ardhi ambayo haina muhimili wa dola, Tanganyika itakuwa free land for anyone to grab! 😀
Ukiachilia hofu nyengine mlokuwa nayo kama vile zanzibar kupiga hatua kubwa kimaendeleo, mna hofu juu ya usalama wa Tanganyika. Nani ataiongoza Tanganyika? kwa vile Muungano ukivunjika, Serikali ya JPM itakuwa kwishnei, haina mamlaka, ili kuokoa tanganyika, itabidi musalimu tanganyika kwa wazanzibari, na tena hapo kwa hekma zetu wazanzibar na busara na kw vile tunawapenda ndugu zetu, tunaanza process ya kuwatafutia serikali yenu wenyewe!
😀 sijui unaipata hii movie?