aleesha
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 833
- 1,212
Suala la Wazanzibari kuwasilisha petition kwa katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kutaka kurejeshewa kiti chake na mamlaka yake yaliyoporwa na Taifa la Tanganyika kwa kisingizio cha kuwepo kwa Muungano uliokosa misingi ya kisheria katika kuanzishwa kwake, ambapo hivi sasa suala hilo liko Mahakamani kwa kuhojiwa kisheria. petition hiyo, itawasilishwa kwa utaratibu maalumu wa kisheria za kimataifa mbele ya katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) ili nae aiwasilishe mbele ya baraza kuu la Umoja wa Mataifa iweze kujadiliwa kwa mujibu wa utaratibu wa baraza hilo.
Hata hivyo, wasimamizi wa suala hili wanawaomba Wazanzibari walio ndani na nje ya Zanzibar waendelee kufuatilia hatua zinazoendelea kuchukuliwa kwa misingi ya sheria za kitaifa na kimataifa ili kwa muda mfupi ujao nchi yetu irejee kuitumia haki yake ya uhuru,uwanachama wake wa kudumu UN na mamlaka yake kitaifa na kimataifa, na kuwa na ushirikiano wa kirafiki na watu na Mataifa ya jirani Tanganyika, Kenya, Uganda, Burundi, Ruwanda, Sudani na nchi zote za Umoja wa Afrika na ulimwengu mzima.
Kwa heshima ya sheria za kimataifa za ushirikiano bila ya ubaguzi wa aina yoyote, kazi hii inaendelea kufanywa na viongozi wetu wanao simamia hizi kesi, na baadhi ya wanasheria wa ndani ya Zanzibar na nje ya Zanzibar kwa manufaa ya Wazanzibari wote.
# AjendaYaZanzibar
Hata hivyo, wasimamizi wa suala hili wanawaomba Wazanzibari walio ndani na nje ya Zanzibar waendelee kufuatilia hatua zinazoendelea kuchukuliwa kwa misingi ya sheria za kitaifa na kimataifa ili kwa muda mfupi ujao nchi yetu irejee kuitumia haki yake ya uhuru,uwanachama wake wa kudumu UN na mamlaka yake kitaifa na kimataifa, na kuwa na ushirikiano wa kirafiki na watu na Mataifa ya jirani Tanganyika, Kenya, Uganda, Burundi, Ruwanda, Sudani na nchi zote za Umoja wa Afrika na ulimwengu mzima.
Kwa heshima ya sheria za kimataifa za ushirikiano bila ya ubaguzi wa aina yoyote, kazi hii inaendelea kufanywa na viongozi wetu wanao simamia hizi kesi, na baadhi ya wanasheria wa ndani ya Zanzibar na nje ya Zanzibar kwa manufaa ya Wazanzibari wote.
# AjendaYaZanzibar