FATILIA HISTORIA VIZURI HAKUNA KISIWA CHOCHOTE DUNIANI KILICHOKUWA NA WATU ILA WALIHAMIA
EBU NIAMBIE MWAKA 1700 NI KABILA LIPI LILIKUWA LINAISHI ZANZIBAR MAANA WATU WANAJITAHIDI KUBISHA WAKIDHANI HISTORIA YA ZANZIBAR IMEANZA MIAKA 2OO ILIYOPITA JUST GO BACK
Kwa kifupi nitakwambia kuwa wenyeji wa zanzibar ni makabila yanayoishi pembezoni mwa pwani ya Afrika mashariki,Zanzibar ni visiwa viwili yaani Unguja na Pemba,kuna "research" iliyofanywa na machuoni wa Daresalam University,iiliyokuwa na "Conclution" kuwa wenyeji wazanzibar walikuwa wamendelea sana kimaarifa kuliko wenzao wa Bara hapa naongela katika nyakati za "stone age" sio miaka 1700
Sasa Kisiwa cha Unguja wenyeji wake ni watu wa makabila kama
wazaramo,Wadigo,Wasegeju,Wagunya nk,Ukenda Pemba wenyeji wake wengi makabila yakutoka Tanga kule kuna
wazigua,wadigo,wasegeju,wagunya,wasomali nk
Sasa watu hao ambao wengi wao ni wavuvi walikuwa wanalala "
Dago" kwenye hivi visiwa,waliendelea hivyo mpaka wengine wakaanza kufanya maakazi kabisa katika hivi visiwa.
Je Unajua kuwa maji yakikupwa ukikaa zanzibar mjini unaweza kuuona mji wa Bagamoyo,je unajua kuwa inachukua saa moja tu kutoka Bagamoyo mpaka ras shangani Zanzibar kwa ngarawa inayotumia tanga, kama upepo wa matalai uko mzuri,Je unajua kuwa inachukua saa moja na nusu kutoka Pangani Tanga mpaka kufika Pemba...
Je unajua wakati Nyerere na Karume wanaunganisha nchi na kuunda muungano wao wa kisiasa Zanzibar "population" ilikuwa laki tatu tu hiyo ilkuwa 1964
kaka huu ni wakati wa information technology(IT) ingia katika google utapata habari zote,,,,,acha kukurupuka kuandika vitu huvijui
kama umesoma na kufahamu utaona kuwa katika hivi visiwa walikuwa wanaishi watu tangu enzi za "Stone age",vile hakuna masafa makubwa kutoka mrima(bara) mpaka kufika katika hivi visiwa kwahiyo watu waliweza kusafiri bila matatizo.
Kama nitapata wakati nitakujuzu kwanini kisiwa cha Pemba kukawa na mashombe wengi kuliko Unguja,vile vile nitakufahamisha kuwa Waswahili ni kabila,tafakari