Wazanzibar wote ni wageni

Wazanzibar wote ni wageni

....kwa hoja yako basi si visiwani tu walihamia...jamii ya wabantu, kush,nilotiki,na waongeaji wa kinguni(nguni speakers)...hao wote asili yao ni kituo kimoja katika sehemu fulani yatu afrika, na kwa kutokea hapo wakasambaa....nani anabakia kuwa mwenyeji wa asili, mfano ktk nchi kama kenya...au bagamoyo?
Mkuu naona unataka kuanzisha mada juu ya mada, mimi nimeongelea zanzibar na visiwa vyote duniani. Chunguza watu wa visiwani utagundua kuwa wengi ni machotara, wanaunganishwa na ukweli kuwa mababu zao walikutania visiwani. Hayo ya Bagamoyo na kwingineko mimi sijayaongelea wala sitaki nayaongelee kwa leo.
 
Kwa kifupi nitakwambia kuwa wenyeji wa zanzibar ni makabila yanayoishi pembezoni mwa pwani ya Afrika mashariki,Zanzibar ni visiwa viwili yaani Unguja na Pemba,kuna "research" iliyofanywa na machuoni wa Daresalam University,iiliyokuwa na "Conclution" kuwa wenyeji wazanzibar walikuwa wamendelea sana kimaarifa kuliko wenzao wa Bara hapa naongela katika nyakati za "stone age" sio miaka 1700

Sasa Kisiwa cha Unguja wenyeji wake ni watu wa makabila kama wazaramo,Wadigo,Wasegeju,Wagunya nk,Ukenda Pemba wenyeji wake wengi makabila yakutoka Tanga kule kuna wazigua,wadigo,wasegeju,wagunya,wasomali nk

Sasa watu hao ambao wengi wao ni wavuvi walikuwa wanalala "Dago" kwenye hivi visiwa,waliendelea hivyo mpaka wengine wakaanza kufanya maakazi kabisa katika hivi visiwa.

Je Unajua kuwa maji yakikupwa ukikaa zanzibar mjini unaweza kuuona mji wa Bagamoyo,je unajua kuwa inachukua saa moja tu kutoka Bagamoyo mpaka ras shangani Zanzibar kwa ngarawa inayotumia tanga, kama upepo wa matalai uko mzuri,Je unajua kuwa inachukua saa moja na nusu kutoka Pangani Tanga mpaka kufika Pemba...

Je unajua wakati Nyerere na Karume wanaunganisha nchi na kuunda muungano wao wa kisiasa Zanzibar "population" ilikuwa laki tatu tu hiyo ilkuwa 1964

kaka huu ni wakati wa information technology(IT) ingia katika google utapata habari zote,,,,,acha kukurupuka kuandika vitu huvijui

kama umesoma na kufahamu utaona kuwa katika hivi visiwa walikuwa wanaishi watu tangu enzi za "Stone age",vile hakuna masafa makubwa kutoka mrima(bara) mpaka kufika katika hivi visiwa kwahiyo watu waliweza kusafiri bila matatizo.

Kama nitapata wakati nitakujuzu kwanini kisiwa cha Pemba kukawa na mashombe wengi kuliko Unguja,vile vile nitakufahamisha kuwa Waswahili ni kabila,tafakari
...hapa, nimekuwa karibu sana kihoja na wewe ktk mjadala huu, ningekutana na bandiko lako hili kwanza, nisingeweka bandiko la kwanza nimekutumia...niseme ni kama vile alietangulia kufika visiwani nakuanzisha makazi anakuwa ndio
Ndio mwenyeji...lkn pia kuna nukta ya juu ya kweli kuwa zanzibar ni kipande cha afrika (siku zote), na asili ya mwenyeji wake ni mtu mweusi mwafrika....salute kamanda Chabuso!
 
Waarabu walikuja ktk visiwa vya zanzibar kibiashara tu na waliwakuta wenye ji ambao ni hao waliyotajwa. ...ndiyo Waarabu wakawa na mahusiano na wanawake wa kiafrika ndiyo wakazaliwa machotara!
Wakati ule Waarabu hawakuja kutawala walikuja kibiashara

Ovaaaa
Seyid said alihamia Zanzibar kama mtawala
 
Mabwana wenyewe wanatafuta wa kuwaowa maana dhiki hadi kwenye matako!!!!

Pia ukumbuke wazanzibar hasa WAPEMBA sio mizigo hivyo kwao kuiondoa dhulma inayoendelea zanzibar ni jambo rahisi mno, nikiasi ya kusubiri muda tu ufike!!! Wazanzibar sio waoga kama watanganyika na hili watawala wanalijua na ndio maana jambo dogo tu linapelekwa jeshi na vifaru zanzibar ili kupambana na watu ambao hata kisu hawana.


Ni kweli siyo waoga ila pia kumbuka ile rasharasha ya wakati ule kuna wapemba.waliokimbilia baharini wakafa na wengine walikimbilia Kenya mpaka saa hizi hawajarudi Zenji
 
Mkuu naona unataka kuanzisha mada juu ya mada, mimi nimeongelea zanzibar na visiwa vyote duniani. Chunguza watu wa visiwani utagundua kuwa wengi ni machotara, wanaunganishwa na ukweli kuwa mababu zao walikutania visiwani. Hayo ya Bagamoyo na kwingineko mimi sijayaongelea wala sitaki nayaongelee kwa leo.


Mkuu hebu tupe na asili ya wale Aborigines wa Australia, je na wale ni machotara? Au asili yao ni wapi!
 
Waarabu walikuwa hawajui kutawala huo ni ujinga wa mwisho. Nenda katika Library of Congress katizame uone katiba ya mwanzo duniani aliiandika nani? Na hata baadhi ya vifungu vyake vimeitumika katika katiba ya Marekani. Waaarabu wametawala Europe hasa Spain kwa muda wa zaidi ya miaka 500.

Hapa Afrika Mashariki as of up to the 19th Century hata hizi nchi zinaozoitwa sasa Tanganyika, Kenya na Uganda hazikuwako. Wakati Zanzibar ipo ni dola tena Himaya kubwa. Eneo lote la Afrika ya Mashariki lilikuwa chini ya Himaya ya Zenj Empire isipokuwa Old Zimbabwe na Zululand. Tanganyika ilipata jina lake rasmi 1920. Kigoma ilitewa chini ya himaya ya Belgian Congo na kukabidhiwa Tanganyika mwaka huo huo. Ukoloni wa mzungu kwa ulaghai wa wamisheni hamuusemi nyinyi kama wao ndio waliigawa Afrika lwa kujikatia kila mtu pande lake. Zanzibar iliporwa eneo lote lilokuwa himaya yake na kubakishiwa visiwa vyake viwili. Halafu leo mnadiriki kusema Zanzibar si nchi.
Sasa basi na nyinyi mrudi kwenu Nigeria na Cameroon maana historia ndiyo inavyosema kuwa watu weusi waliingia Tanganyika kutoka Nigeria na Cameroon.
 
Kuna watu wamekuwa wakiwadanganya watu kwamba wao ndio wenyeji na wengine ni wageni, ukweli ni huu;

Hapa chuoni kuna historia nzuri sana ya nchi ya Zanzibar. Hakuna mtu mwenye asili ya Zanzibar; kuna Watwana na Mabwana.

Watwana ni watumwa kutoka Kongo wanaitwa Wamanyema na Mabwana ni waarabu kutoka Omani hao ndio wazanzibar, kwa maneno mengine zanzibar ni ya Wakongo, watumwa na waarabu wakoloni.

Siku moja nitaweka historia yote hapa. Nipo hapa ICC University Illinois, USA.
Wacha kudanganya umati... Akina Mwinyimkuu na Mwana Wa Mwana wao wanatoka wapi?????

Maana ukija kwa style hio basi hakuna mwenye kwao popote... maana sote asili yetu ni Adam, na Adam kashukia nchi gani? i am sure sio Tanzania...
 
Kuna watu wamekuwa wakiwadanganya watu kwamba wao ndio wenyeji na wengine ni wageni, ukweli ni huu;

Hapa chuoni kuna historia nzuri sana ya nchi ya Zanzibar. Hakuna mtu mwenye asili ya Zanzibar; kuna Watwana na Mabwana.

Watwana ni watumwa kutoka Kongo wanaitwa Wamanyema na Mabwana ni waarabu kutoka Omani hao ndio wazanzibar, kwa maneno mengine zanzibar ni ya Wakongo, watumwa na waarabu wakoloni.

Siku moja nitaweka historia yote hapa. Nipo hapa ICC University Illinois, USA.


chuo cha Kanisa Katoliki ??

Hapo utaipata historia kama hiyo bila shaka
 
kuna Wazanzibari ambao asili yao ni kutoka Kenya,Ushelisheli n.k.
ukisoma makaratasi fanya na utafiti.
nyie sijui nia yenu nini. eti wakongo na waomani ndio wako zenj wakati watu wa asili ya tanganyika ndio haswa waafrika waliopelekwa kwa wingi zanzibar kama watumwa na hao waarabu.
 
Ni kweli siyo waoga ila pia kumbuka ile rasharasha ya wakati ule kuna wapemba.waliokimbilia baharini wakafa na wengine walikimbilia Kenya mpaka saa hizi hawajarudi Zenji

Wewe unaita rasharasha kwa kuwa hujui unaongelea kitu gani!! Jaribu kumtafuta japo polisi mmoja aliekuwepo wakati ule pemba atakusimulia vizuri sana wapemba ni watu gani!!

Mara ngapi polisi wamekiri kuwa waandamanaji walipoanza kupigwa risasi za moto katu hawakurudi nyuma bali walisonga mbele hadi wakafanikiwa kuviteka vituo vyote vya polisi vilivyopo pemba na kuweka bendera ya CUF ndipo alipokuja Mahita na helkopta akawa anashambulia kupitia angani.

Pamoja na wao kukimbilia kenya tayari walikwisha kujikomboa katika dhulma ya uonevu wa kila mara wa polisi!! Si umeona au kusikia kuwa tokea wakati ule wapemba wanachagua wawakilishi, wabunge, madiwani na maraisi bila ya yeyote yule kubuguziwa!!! Ujinga wa MASHEHA NA MAZOMBI wanaonyanyasa na kutesa watu umebakia Unguja tu na sio Pemba.

Mazombi wanaotesa watu unguja wanazijua vizuri tactic za wapemba wanapoamua kulinda maeneo yao, kama hujui mbinu zao waulize wale usalama wa taifa ambao walikuwa wanakawaida ya kuweka vinyesi katika visima, mashule na masoko ya Pemba!! Walipoamua waliliondoa kwa mikono yao.
 
Kuna watu wamekuwa wakiwadanganya watu kwamba wao ndio wenyeji na wengine ni wageni, ukweli ni huu;

Hapa chuoni kuna historia nzuri sana ya nchi ya Zanzibar. Hakuna mtu mwenye asili ya Zanzibar; kuna Watwana na Mabwana.

Watwana ni watumwa kutoka Kongo wanaitwa Wamanyema na Mabwana ni waarabu kutoka Omani hao ndio wazanzibar, kwa maneno mengine zanzibar ni ya Wakongo, watumwa na waarabu wakoloni.

Siku moja nitaweka historia yote hapa. Nipo hapa ICC University Illinois, USA.
Wewe katika watu wajinga basi ni mmoja wao.. kwa maelezo yako unamaanisha historia ya Zanzibar imeanza baada ya kuja waoman 1698. Sasa kabla ya hapo hakuna mtu katika kisiwa cha Zanzibar. kwa sababu biashara ya utumwa ilikuwaja baada ya waoman kutwala Zanzibar.. kabla ya kuandika kwanza soma na sifikirii kama upo kweli ICC university kama kweli umeweza kuingia hapo hiyo university must be joke..

History of Zanzibar - Wikipedia, the free encyclopedia

People have lived in Zanzibar for 20,000 years. History proper starts when the islands became a base for traders voyaging between the African Great Lakes, the Arabian peninsula, and the Indian subcontinent. Unguja offered a protected and defensible harbor, so although the archipelago had few products of value, Omanis and Yemenis settled in what became Zanzibar City (Stone Town) as a convenient point from which to trade with towns on the Swahili Coast. They established garrisons on the islands and built the first mosques in the African Great Lakes.

During the Age of Exploration, the Portuguese Empire was the first European power to gain control of Zanzibar, and kept it for nearly 200 years. In 1698, Zanzibar fell under the control of the Sultanate of Oman, which developed an economy of trade and cash crops, with a ruling Arab elite and a Bantu general population. Plantations were developed to grow spices; hence, the moniker of the Spice Islands (a name also used of Dutch colony the Moluccas, now part of Indonesia). Another major trade good was ivory, the tusks of elephants that were killed on the Tanganyika mainland - a practice that is still in place to this day. The third pillar of the economy was slaves, which gave Zanzibar an important place in the Arab slave trade, the Indian Ocean equivalent of the better-known Triangular Trade. The Omani Sultan of Zanzibar controlled a substantial portion of the African Great Lakes coast, known as Zanj, as well as extensive inland trading routes.

Sometimes gradually, sometimes by fits and starts, control of Zanzibar came into the hands of the British Empire. Part of the political impetus for this was the movement for the abolition of the slave trade. In 1890, Zanzibar became a British protectorate. The death of one sultan and the succession of another of whom the British did not approve later led to the Anglo-Zanzibar War, also known as the shortest war in history.
 
Noona hii historia ya zanzibari kila mtu ana "version" yake,wengine watanganyika ndio wako wengi kwasababu wamepelekwa kama watumwa,wengine wakongo ndio wengi,wengine wangaija ndio wenyeji wa zanzibar,wengine wanyawemwezi ndio wako wengi,,.......

Kweli hayo makabila yamechangia kuleta uatamaduni wa nani kuwa mzanzibari lakini mkumbuke tu kila kabila lilikuwa na waledi wake,kila kabila lilikuwa na mchango wake katika historia ya Zanzibar

Mfano wangazija ni wahamiaji wa mwishom kuhamia kwa wingi Zanzibar katika kisiwa Cha Unguja,hawa watu walikimbia njaa iliyowakumba katika vita vya kwanza vya Dunia,wengi wao walikuwa wanaenda kupokewa Bandari ya Malindi Funguni na wenyeji wa Zanzibar walikuwa katika hali mbaya sana,wengine uchi wa kuzaliwa.,hawa walikuja wenyewe zanzibar

Wanyamezi hawa watu walikuja kwa wengi baada ya Sultani kuhamisha maakazi yake kutoka Kilwa na kuyaweka Zanzibar,Kabila hili watu wake walikuwa "Loyal" sana kwa Sultan,Sultani aliwatumia hawa watu kama walinzi wake,hawa jamaa waliletwa na mwarabu Zanzibar.

Wamanyema hili kabila linalotoka bara ya mbali wanawake zake walliwavutia sana warabu,Famili yote ya Sultani wa Zanzibar ni machanganyikai wa hili kabila,Sultan aliekuwa anaitwa sayd Khalife aliowa mwanamke wa kimanyema alieitwa bi Matuka,kuanzia hapo generation ya famila ya Kisltani ikawa ni mchangyiko wa warabu na wamanyema "Half Cast",Wamanyema waliletwa kam watumwa na mwanarabu zanzibar

Kumbuka kuwa Mwarabu aliitwa zanzibar na wenyeji ili waje wawasaidie kumtoa Mreno,vile vile ukumbuke kuwa Zanzibar ilikuwa sehemu kubwa ya Biashara,warabu,wahindi,wachaina,wapasia wote walikuwa wanakuja zanzibar kufanya biashara wakari wa wa pepo za mosoon.
ujue vile vile Wairani(Persianias) walifika mwazo katika visiwa vya Zanzibar kuliko mwarabu..

Kuna kabila la Wayao,hili kabila liko kusini mwa Tanganyika,Kilwa kama sikosei,hili kabila waliletwa na warabu,warabu walpohamisha makazi yao kutoka kilwa kwenda Zanzibar waliondoka na hawa watu kwenda nao zanzibar.

Sasa cha kujiuliza nani hasa mwenyeji wa Zanzibar,mwarabu aliitwa na akina nani kuja kuwasaidia kumuondosha Mreno.Jibu ni rahisi kabisa Zanzibar kulikuwa na mchanganyiko wa wamakabila hasa yale ya pwani za Afrika mashariki,wasegeju,wadigo,wazaramo, na nusu ya wahadimu ambao hajulikani wanatokea wapi,au labda ndio hao wazuoni walioona vifaa vyao walivyokuwa wanatumia wakati wa stone age,kwavile Zanzibar ilkuwa tayari na mzungo wa wafaya biashara kutoka sehemu mbali mbali za dunia na wengi wao walikuwa wanaume hii ilileta watu wa zanzibar wawe "Cosmopolitan"..Hawa makabila ya pwani waliofanya makazi yao zanzibar ndio wenyeji wa Zanzibar hawa walihamia mwanzo kabla hata binadamu wa pwani za mbali hawajanza kusafiri na kufanya biashara na visiwa vya Zanzibar,hawa watu ni walikuwa
wafanya biashara.....

Hiyo ni simulizi ndo ndogo za historia ya zanzibar kutoka kwa wazee wetu.......

You want more ask for more,Tafakari 🙂
 
Idara ya mambo ya kale UDSM ilifanya uchunguzi Zanzibar na kugundua mafuvu ya watu wa kale Sana kwenye mapango
Mafuvu hayo yalipimwa Marekani na kuonyesha Ni ya miaka zaidi ya elfu tatu iliyopita.
Hi Ina maana kulikuwepo watu kabla ya hawa wanaojiita wa Zanzibari wa sasa
Inasadikiwa walifika na hawa kima wekundu wa Zeni
Source: utalii wa ndani Chanel ten (archives)

Weka hiyo source na vielelezo vya hayo unayoyasema na kwani hayo mafuvu hayako makumbusho wala archive ya Zanzibar?
 
Back
Top Bottom