Mkuu Mimi nilikaa kama miezi sita hivi,, pale maisha yanategemea kufanya kazi viwandani mfano viwanda vya nguo,,,nk,,au kuhangaika mitaani,,ni inchi nzr kwa raia,,lakini kwa wageni ni ngumu kidogo,,, maana kuna migrants wengi wakitokea Syria,, hata Egypt kwa njia za panya,,,pesa yao inaitwa milioni,,,ni strong kama ilivyo dola,,,ukiwa na dola moja,,sawa na milion moja,,,hazipishani sana,,,pale nilishindwa sababu ya haraka zangu,,nikaelekea Greece,, sababu sikuwa na viza ya Greece,,, nilikuwa na viza ya Turkey tu,,na Turkey sio inchi ya shengen ,,,ikanibidi nijiunge na migrants wanaokwenda Greece kwa njia za panya,,zilikuwa njia mbili za kuingia Greece,,baharini au kupitia mtoni,,,zote ni dola 500 kila migrants mmoja,,,nikachaguwa njia ya kuvuka mto,,niliona ndy salama zaidi,,Turkey ipo border na Bulgaria,, na Greece,,upende Fulani,,kuna mji Fulani unaitwa Izmir,,, upo close to Greece,,,tofauti yake ni mto tu,,,kwahyo tulifungiwa kwenye fuso moja tukiwa kama migrants 100 hivi,,,tulitembea usiku kwa usiku toka Istanbul hadi Izmir kuanzia saa mbili usiku hadi saa sita usiku tukafika lzmir,,,ilikuwa winter time hatari,,jinsi nilivyo vaa ni kama bag zima lipo mwilini,,,nilikuwa nimevaa jeans tatu na track suit ndani,,na Fulani tatu ,sweater na koti kubwa la ngozj,,na soksi ya kuzuia baridi juu,,baada ya kufunguliwa mlango wa fuso,,,ilikuwa baridi haswa,,eneo lote lilikuwa jeupe kwa theluji,,,basi haraka haraka tukaambiwa tuiname chini,,,,pale wale Wa Turkey wenye connection za kutuvusha,,,wakatoa boat Fulani ya kujaza kwa upepo,,wakaijaza pale baada ya kama nusu saa wakaiweka mtoni,,ulikuwa mto wa upana kama wa mita 50 hivi,,,huo MTO unatenganisha Turkey na Greece,, na huwa unalindwa pande zote wakati wa summer time,,lakini unakuwa haulindwi wakati wa winter time...kwahyo winter ndy watu wanakatisha hapo,,basi nikaingia kwenye boat,,ikapigwa kasia hadi upande wa greece ni kama dk 10 tu nipo upande wa Greece,,,baada ya kumaliza kutuvusha,,tukaanza safari kuitafuta mjini,,,tulipewa maelekezo na wale jamaa kwamba tufate maandishi,,ya kigiriki,,,maana maandishi ya kigiriki na maandishi ya Bulgaria ni tofauti lakini yanafanana sana,,so tufate barabara ambayo inaelekeza maandishi ya kigiriki,,,tukifata tofauti tutakuwa mikononi mwa askari wa Bulgaria,, na wakasema lazima tukamatwe na police wa kigiriki,, ili watupeleke vituoni,,tusipokamatwa tutatembea umbali mrefu sn kwa miguu,,,tusihofu tukiona police,,, basi tulitembea kuanzia saa nane usiku hadi saa mbili asubuhi,,, tukaanza kukamatwa kwa makundi na kupelekwa kituoni,,ule mji nimesahau kidogo,,, baada ya muda wakatupeleka camp,,,nikakomplain kama msomali,,,baada ya week mbili za pale camp,,,nikatolewa nikapelekwa kuna mji mmoja unaitwa ethlonic hapo tukapandishwa train,,,wakatwambiya you are free to go,,,,nikaingia Athens au Athena,,,huo ndy ulikuwa mwanzo wangu wa kuingia ulaya,,,2011.,.hivyo tu mkuu,,,ktk harakati za mbongo,.