mdukuzi
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 22,312
- 55,969
Huyo ni wewe acha kuzuga huu si usimuliaji wa kuambiwaNimekwambia rafiki yangu ni miaka hiyo ya 90 ndo kwanza nilikuwa nimeanza shule
Huyo ni wewe acha kuzuga huu si usimuliaji wa kuambiwaNimekwambia rafiki yangu ni miaka hiyo ya 90 ndo kwanza nilikuwa nimeanza shule
Hako kaneno ka kizungu ka mwisho kamenikumbusha mbongo mmoja alipigwa risasi na majambazi huko majuuTatizo mkuu unazungumza kama mtu aliyeishi/anaishi huko.!
Ndugu, changamoto za maisha, utakutana nazo popote pale dunia.. Mbona watu wengi wapo hapahapa Tanzania na wakikusimulia changamoto wanazopitia iwe za kibiashara, ajira, afya.. wewe mwenyewe utashika tama..
Suala la kwenda kutafuta life nje ya mkoa uliozaliwa au nchi... inategemeana na comfort zone ya mtu husika
Exposure inajumuisha Kusikia, kusoma na kujifunzaKwa hiyo story ulizosikia zimekujaza hofu...?
Mtu yyte mwenye mipango yakusaka maisha nje ya Tz na aende tu!
Changamoto na Mafanikio ni moja wapo ya mchakato mtu kutikia malengo yake..
Leo hii wachina wana vuka bara ..lao kuja huku na biashara wanayoifanya ni yale madudue ya kamali wanayaocheza vijana uswahilini..
So kama kuna kijana anawaza kusaka life nje na kaona fursa kwanini asitoke?
Punguza stress mkuu, unaandika kwa stress sana , kuna mambo yanakutatiza?![]()
Mwenye kumfahamu Mtanzania huyu mkazi wa Magomeni, anateseka nchini Pakistan
Wakuu kuna "clip" na picha kadhaa zinasambaa mtandaoni za Mtanzania,mwanaume na mkazi wa Magomeni. Jamaa anasema kwao ni Magomeni mtaa wa Chemchem na Idrisa,Wazazi wake wanaishi hapo,Mama yake anaitwa Rukia Daudi na baba yake anaitwa Akida. Huyu jamaa ukiangalia video anaonekana yupo katikati...www.jamiiforums.com
Mkifika huko mnaishi kama mabata tu, mnarisk sana maisha halafu mnapeana moyo kijinga hapa
Atakuwa kanenwpa mno maana mbuzi ukitaka anenepe TOA corodaniKwahiyo mkuu hauna korodani?
Maisha kweli yana mengi dah.. hilo eneo ni gumu mno mno mkuuYah ni kati ya mikoa ya libya ambapo 91% ni jangwa. Jamaa anakwambia ukiwa katika lile jangwa hujui N, S, E, W ni wapi. Anakwambia maisha ya wakazi wa pale ambao nao ni wachache wamejenga vijumba vya udongo ni magumu sana sana sana. Ndiyo maana anasema hata nzi wa pale ni masikini sana. Anakwambia kuna mbuzi na kondoo chache nao wanaishi kwa kula karatasi na vitu vya ajabu na ajabu kusurvive
hivi weye bado upo??? Walikusema sana kwenye kikao cha juzi😃😃😃😃 Bwege bwana
Watu wanajilipua, miaka ya 2013/14 kuna jamaa flani alikuwa anasoma sauti alikuwa anaenda Somalia na Sudan huko kufuata bidhaa za magendo.Kuna jamaa yangu kaenda Kismayu Somalia kulikuwa na Kazi ya Kusimamia Boti, Kakaa mwezi amerudi mwenyewe maisha ya Kule yamemshinda.
Shukuru waliogundua mtandao, enzi hizo hakukuwa na vitu hivi.Ila kiukweli wazamiaji wengi wa enzi hizo walikuwa "wakurupukaji" sanaa labda ndio maana iliitwa "kujilipua", siku hizi mambo yanafanyika kwaakili zaidi kuliko kufuata mihemko.
Wema ni akiba, japo siku hizi wana sema tenda wema nenda zako maana huchelewi kusagiwa kunguni.Kuna mtu anaitwa Kaka Vale huyo.
Jamaa mweupe pee ukimuangalia utafikiri half cast.
Basi aliondoka Bongo kiajabuajabu miaka ya 1980 ya kati huko. Hapo airport walimbana anaenda wapi. Akasema yeye mtoto wa Gorbachev anarudi kwao, miaka hiyo Gorbachev anaongoza USSR. Basi watu wa airport wakaogipa wakamuacha apite.
Basi kazunguka sana Italy na Greece watoto wa Migomigo wa beach kawasaidia sana.
Kuna siku alikuja Bongo akatuachia Mercedes Benz atumie Aunt (Mama yake).
Basi yeye alivyoondoka, ile Benz tukawa tunapiga nayo misele Dar.
Siku moja tukawa tunapiga misele Magomeni. Kuna watoto wa Magomeni wakatufuata. Wakatuuliza hii gari ya Vale, nyie wadogo zake? Tukasema ndiyo sisi wadogo zake.
Basi wale jamaa walifurahi sana wakasema kaka yenu katusaidia saana Greece hapo beach. Wakapiga picha na sisi ikawa kama wamekutana na ma celebrities fulani wakawa wanaitana "Njooni muwaone wadogo zake Vale".
Nikasema kweli unaweza kumfanyia mtu wema halafu usijue huo wema utadumu vipi.