Watu wanaoishi kwa kuwinda na kukusanya kama Wahdzabe wana afya kuliko wakulima, wafugaji na watu wengine

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,233
12,740
Mtaalamu mmoja alisema kuwa afya ya binadamu ilianza kuzorota pale alipoanza kulima. Huu ni ukweli kabisa. Babu zetu walipokuwa wanaishi kwa kuwinda na kukusanya walikula kila aina ya chakula. Walikula matunda, majani ya miti, nyama, asali, mayai ya ndege, wadudu, mizizi, samaki nk nk. Watu hawa kila kitu walipata kwa kiasi. Hawakujua upungufu wowote mwilini.

Alipoanza kulima akawa analima mazao ya aina fulani tu. Labda mahindi na maharage. Matokeo yake mwaka mzima anakula ugali maharage. Labda abahatike kula kuku mara moja au mbili kwa mwaka. matokeo yake afya yake ikawa duni kabisa. Mtu anashiba vyema lakini afya yake sifuri. Hali hii inaendelea hadi leo huko vijijini. Ndiyo maana mikoa ya nyanda za juu kusini inaongoza kwa uzalishaji wa chakula lakini pia inaongoza kwa utapiamlo.

Wakati wetu huu wa kisasa vyakula aina mbalimbali vinapatikana kirahisi hasa mijini. Lakini hili nalo limeleta matatizo. Inadaiwa kuwa wakati wa kuwinda na kukusanya, nyama, vyakula vya sukari na chumvi vilikuwa vitu adimu sana. Inasemwa ndiyo maana binadamu akajenga tamaa kali ya vyakula vya mafuta, sukari na kiasi chumvi. Hivi leo hii vimekuja kumharibia kabisa afya yake.

Nyama, sukari na chumvi vinapatikana kwa wingi mno. Na kwa vile alishajenga tamaa kali ya viti hivyo sababu vilikuwa adimu kwake, anaanza kuvifakamia kwa fujo. Matokeo yake ni kuporomoka kabisa kwa afya yake. Matunda yamefanyiwa modifications ili yawe na sukari zaidi. Na matunda yenyewe ni ya ina chache sana. Leo mjini ukisema naenda kula matunda tikiti na ndizi ndiyo hasa utavikuta.

Leo tunaona wahadzabe na wasandawe wanaishi maisha primitive sana, lakini kwenye afya wametuacha mbali sana. Tuna mengi sana ya kujifunza kutoka kwao kuhusu suala la lishe.
 
Life expectancy ya wahadzabe unaijua?

Nyanda za juu kusini wanapokuwa na utapiamlo ni KWA vile hawali chakula mfululizo ndani ya mwaka. Ni utapiamlo wa kutokula chakula cha kutosha.
 
Life expectancy ya wahadzabe unaijua?

Nyanda za juu kusini wanapokuwa na utapiamlo ni KWA vile hawali chakula mfululizo ndani ya mwaka. Ni utapiamlo wa kutokula chakula cha kutosha.
Hapana. Nyanda za juu wana msosi mwingi tu mwaka mzima. Tatizo ni ugali maharage na wakibadilisha ni viazi na ndizi.
 
Sio kweli. Hata wao wanatamani kuwa na mifugo na mazao na wanahitaji msaada wa serikali sana
Binadamu hakuanza kulima na kufuga kwa kupenda. Shida ndiyo zilinfanya aanze kulima. Ndiyo maana utaona kilimo kilianzia maeneo yenye uhaba wa vyakula vya kuwinda na kukusanya. So hao jamaa hawatamani kulima wala kufuga hata kidogo. Watafanya hivyo shida zikiwalazimisha.
 
Binadamu hakuanza kulima na kufuga kwa kupenda. Shida ndiyo zilinfanya aanze kulima. Ndiyo maana utaona kilimo kilianzia maeneo yenye uhaba wa vyakula vya kuwinda na kukusanya. So hao jamaa hawatamani kulima wala kufuga hata kidogo. Watafanya hivyo shida zikiwalazimisha.
Umewahi kufika wanapoishi Wahadzabe au hata kuwatembelea na kuwahoji?

Usiongee kitu usichokifahamu, Kipindi cha ukame wanapata shida sanaa na wanahitaji usaidizi sana...hakuna wanyama wa kuwawinda karibu, Asali haitoshi au haipo kabisa na wanafuata mbali sana mizizi ya miti...unakuta hapo wana watoto wachanga na yamkini wanaumwa

mpaka wapo wanaoshauriwa kuanza ufugaji
 
Umewahi kufika wanapoishi Wahadzabe au hata kuwatembelea na kuwahoji?

Usiongee kitu usichokifahamu? Kipindi cha ukame wanapata shida sanaa na wanahitaji usaidizi sana...hakuna wanyama wa kuwawinda karibu, Asali haitoshi au haipo kabisa na wanafuata mbali sana mizizi ya miti...unakuta hapo wana watoto wachanga na yamkini wanaumwa

mpaka wapo wanaoshauriwa kuanza ufugaji

Wameanza kuelimika sasa hivi kwa kuingiliana na watu,na kuanza kuwekeza katika vyakula vinavyohifadhika.

Video za instagram zinaonyesha wakipika mpaka ugali na uji,mpaka coca wanapelekewa wanakunywa,khanga na vitenge wanavaa kwa sasa.

Ni kweli binaadam hawezi kuona umuhimu wa kitu mpaka aelekezwe,wakati wa sensa walipoambiwa wakae wasubiri kuhesabiwa waliomba wapelekewe nyama ili wasishinde njaa,wakapelekewa nyati.
 
Umewahi kufika wanapoishi Wahadzabe au hata kuwatembelea na kuwahoji?

Usiongee kitu usichokifahamu? Kipindi cha ukame wanapata shida sanaa na wanahitaji usaidizi sana...hakuna wanyama wa kuwawinda karibu, Asali haitoshi au haipo kabisa na wanafuata mbali sana mizizi ya miti...unakuta hapo wana watoto wachanga na yamkini wanaumwa

mpaka wapo wanaoshauriwa kuanza ufugaji
Hata wakulima na wafugaji kuna kipindi huwa wanahitaji msaada wa chakula. Tena maeneo mengine kila mwaka wanapelekewa msaada wa chakula. Pia Wahadzabe ni mfano tu. Kuna hunter gatherers huko misitu ya Congo, Amazon, huko Arctic nk nk.
 
Mtaalamu mmoja alisema kuwa afya ya binadamu ilianza kuzorota pale alipoanza kulima. Huu ni ukweli kabisa. Babu zetu walipokuwa wanaishi kwa kuwinda na kukusanya walikula kila aina ya chakula. Walikula matunda, majani ya miti, nyama, asali, mayai ya ndege, wadudu, mizizi, samaki nk nk. Watu hawa kila kitu walipata kwa kiasi. Hawakujua upungufu wowote mwilini.

Alipoanza kulima akawa analima mazao ya aina fulani tu. Labda mahindi na maharage. Matokeo yake mwaka mzima anakula ugali maharage. Labda abahatike kula kuku mara moja au mbili kwa mwaka. matokeo yake afya yake ikawa duni kabisa. Mtu anashiba vyema lakini afya yake sifuri. Hali hii inaendelea hadi leo huko vijijini. Ndiyo maana mikoa ya nyanda za juu kusini inaongoza kwa uzalishaji wa chakula lakini pia inaongoza kwa utapiamlo.

Wakati wetu huu wa kisasa vyakula aina mbalimbali vinapatikana kirahisi hasa mijini. Lakini hili nalo limeleta matatizo. Inadaiwa kuwa wakati wa kuwinda na kukusanya, nyama, vyakula vya sukari na chumvi vilikuwa vitu adimu sana. Inasemwa ndiyo maana binadamu akajenga tamaa kali ya vyakula vya mafuta, sukari na kiasi chumvi. Hivi leo hii vimekuja kumharibia kabisa afya yake.

Nyama, sukari na chumvi vinapatikana kwa wingi mno. Na kwa vile alishajenga tamaa kali ya viti hivyo sababu vilikuwa adimu kwake, anaanza kuvifakamia kwa fujo. Matokeo yake ni kuporomoka kabisa kwa afya yake. Matunda yamefanyiwa modifications ili yawe na sukari zaidi. Na matunda yenyewe ni ya ina chache sana. Leo mjini ukisema naenda kula matunda tikiti na ndizi ndiyo hasa utavikuta.

Leo tunaona wahadzabe na wasandawe wanaishi maisha primitive sana, lakini kwenye afya wametuacha mbali sana. Tuna mengi sana ya kujifunza kutoka kwao kuhusu suala la lishe.
Wewe unaetafuta hela ya kula ndio ukajifunze na hujakatazwa kujiunga nao. Umaskini unakufanya usile vizuri na usile mlo kamili kwakua pesa unayopata inatosha kula tena kwa bajeti.

Angalizo: ukiona mtu anabajetia hadi hela ya chakula hapo kuna njaa kali na upungufu wa madini unaopelekea uzezeta
 
Wewe unaetafuta hela ya kula ndio ukajifunze na hujakatazwa kujiunga nao. Umaskini unakufanya usile vizuri na usile mlo kamili kwakua pesa unayopata inatosha kula tena kwa bajeti.

Angalizo: ukiona mtu anabajetia hadi hela ya chakula hapo kuna njaa kali na upungufu wa madini unaopelekea uzezeta
Hao wamewazidi lishe hata matajiri wanaokula mafuta na sukari kwa wingi. Hujasoma uzi na kuelewa?
 
Back
Top Bottom