Watu ndani ya Mlimani city Mall

Watu ndani ya Mlimani city Mall

ndo maana unaambiwa kuishi dar tu tayari ni elimu ya form four!

hadi kuingia mlimani city kununua bidhaa mule lazima uwe unaconfidence kwanza ya juu!

watu wanapanda magari temeke wanenda nunua ICE CREAM mlimani city!

mlimani city kama ulikuwa hujui chumba kidogo kabisa cha biashara kwa mwezi Mil 14!
Milioni 14? Peleka uongo wako Uyole huko
 
Kuna jambo nimekuwa nikiliobserve kila nikiwa nafanya manunuzi yangu pale Mlimani City..Idadi kubwa ya watu ninaopishana nao wengi utawasikia wakiongea kuhusu kuishi nje ya nchi,kuhusu kuondoka nchini siku sio nyingi,kuhusu kwenda China,India kufunga mzigo wa biashara na mengine mengi..

Najua inaweza kuwa kitu cha kawaida..na always tunashauriwa kumind our own bussiness lakini kwa hili limenifikirisha kidogo..

Hivi wakuu watu wengi wanaokuwa Mlimani City ni kwamba wana class au aina hiyo ya maisha au inakuwaje??..

Sent using Jamii Forums mobile app
Malengo ni tofauti na uwezo kila Mtu huwa na malengo hata mteja mvuta unga huwa na malengo pia


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu waswahili tunapenda sana maisha ya kuigiza kuliko uhalisia...kama unataka U-prove nenda kaangalie maisha ya wanafunzi wa vyuo vikuu,wengi wana-pretend kutoka familia bora,hata kama katoka kijijini ambako hata umeme hakuna.
 
FIKA CENTRAL JUMATATU ASUBUHI..
Ndiyo tatizo letu. Tumechelewa vitu vingi sana.
Ndiyo sababu ufunguzi wa Flyover inakuwa tukio kubwa la kitaifa. Hao wenye zaidi ya 50 watafanya nini?
Kupokea ndege moja au mbili ni tukio la kitaifa. Ethiopia wenye ndege zaidi ya 70 watafanya nini?

Vitu kama Mlimani City, vingekuwa kila pembe ya Dar, huo ushamba usingekuwepo.

Kusaini mkataba wa kuuziana mahindi nalo tukio la kitaifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usafi huficha umasikini sasa kama kapuku ndiyo umuonyeshe kila mtu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijasema umuoneshe kila mtu; ishi kwa uhalisia.
Majuzi kuna binti alipewa namba yangu akawa ana shida. Aliyemuekeza huwa tunakutana ofisini; binti nikamuelekeza aje nyumbani kwa kuwa sikuwa na mpango wa kutoka (Jumamosi - huwa nashinda kwenye banda la kuku kufanya usafi)
Binti alipokuja nikampa kiti hapo nje akaeleza changamoto zake nikamweleza tuonane ofisini J.tatu.

Ile anakuja J.tatu anakuta pale mbele kuna PS - kuingia ofisini kwangu - alinishangaa! Ananiuliza hivi kumbe we ni mtu mkubwa alafu ukiwa nyumbani unakuwa kama mchunga mfugo?
Nilimweleza hivi .. hizo pesa za kuwalipa vijana wa kufanya usafi ndo natumia jioni baada ya kutoka kwenye mabanda ya kuku.
Huko ndo kuishi maisha halisi - sio mtu unajifanya mfanyabiashara kumbe hata kibanda huna.
 
Back
Top Bottom