JaxenDL
JF-Expert Member
- May 17, 2022
- 325
- 672
(CHANZO CHA PICHA, REUTERS)
Mkuu wa huduma za dharura anasema idadi ya watoto waliouawa nchini Iran tangu vita kuanza Februari 28 imeongezeka hadi 208.
Katika taarifa ya video iliyochapishwa na mtangazaji wa kituo kinachomilikiwa na serikali IRIB, Jafar Miadfar alisema kwamba kati ya watoto 208 waliouawa, sababu ya 168 kufariki dunia kati ya hao ilikuwa ni mashambulizi la makombora ya Marekani kwenye shule ya wasichana katika mji wa Minab mwanzoni mwa vita.
Miadfar aliongeza kuwa watoto 13 waliouawa walikuwa na umri chini ya miaka mitano, na mdogo alikuwa na siku tatu.
Zaidi ya raia 1,500 wameuawa kote nchini hadi sasa, kulingana na serikali ya Iran.
Video zilizothibitishwa na picha za setilaiti zilionyesha uharibifu mkubwa karibu na shule ya msingi ya Shajareh Tayebeh huko Minab na eneo la karibu la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Irani (IRGC).
Pia inaonyesha kuwa eneo hilo "lilishambuliwa vibaya wakati mmoja au karibu wakati mmoja", alisema mtaalamu wa silaha NR Jenzen Jones.
# BBC swahili