Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,498
- 113,601
- Thread starter
- #141
Wenye kumbukumbu tunzeni posti hii, Job Ndugai ahukumiwe kwa haki, asipotendewa haki, karma itangilia kati.Wanabodi,
Kwa vile hili ya yeye kugombea 2025, rais Samia mwenyewe aliisha liweka vizuri kabisa ile siku anahojiwa na Salim Kikeke wa BBC, baada ya kuhojiwa kama atagombea urais 2025, rais Samia alijibu vizuri kabisa kuwa "kwa sasa tufanye kwanza kazi, ya 2025 tumwachie Mungu maana no one is shure kufika 2025", hivyo hata rais Samia aliposema 2025 tutamchagua mwanamke, hajamaanisha lazima mwanamke huyo awe ni yeye!. Hivyo ni busara kwa rais wetu Samia, hili la ugombea wa 2025, asilizungumze zungumze sana kwa sasa, ni vyema akaendelea na msimamo wake ule ule wa kwenye BBC kuwa ya 2025 tumuachie Mungu. Kwa sasa, rais aendelee ku deal na haya ya Kaizari, kwa kuchapa kazi na kazi iendelee na yale ya Kimungu tumuachie Mungu mwenyewe.
Paskali
Nashauri, kwa vile 2025 tumeamua kwenda na mgombea mwanamke, kwa vile tayari tunaye rais Mwanamke, lakini bado hatujajua Mungu ametupangia nani, nashauri kama tunao wanawake wengine ambao ni presidential material, wawe highlighted ili hata asipokuwa Samia, mwanamke mwingine awepo, maana...
P