Pakome
JF-Expert Member
- Dec 8, 2024
- 1,541
- 916
Watanzania tunapotembelea nchi za kigeni na kuwaeleza asili yetu, wanafurahi sana nakututania wajukuu wa Mwl Nyerere na hii ndiyo sababu kubwa inayonifanya niheshimu sana nchi ya Tanzania na nishindwe kamwe kukosea adabu Chama Cha Mapinduzi cha Babu yetu Mwl Nyerere
Ni vigumu sana kutamka Chama Cha Mapinduzi pasipokutamka baba wa Taifa
Inawezekana ningekosa adabu labda kama nisingekuwa nimesafiri kwenda nchi za Kigeni lakini kwa heshima ya wageni wanayotupatia na hasa wakigundua sisi ni Watanzania hakika inatugusa sana
Safari yangu ya mwisho ya Afrika katika nchi ya Rwanda ilinigusa sana kwasababu raisi wa Rwanda Paul Kagame alimzungumzia Mwl Nyerere kwa hisia kubwa akilenga namna gani Tanzania imekuwa nchi ya kuigwa mfano hasa wanapokumbuka undugu na ujamaa kati yetu
Wakati mwingine tunapofika Wiingereza na Marekani tunatokwa na machozi kwasababu Wazungu wanatueleza historia ya uhusiano wao na baba wa Taifa Mwl Nyerere na hasa Chama cha Mapinduzi wakitueleza jinsi baba wa Taifa alivyokuwa akiwasumbua wakati akiomba uhuru
Tulipokuwa Wiingireza Wazungu walituonesha sare za Chama cha Mapinduzi za mwaka 1995 kwakweli tukapigwa butwaa
Walitueleza baba wa Taifa aliwapa sare hizo kama zawadi ili wajionee hatua za maendeleo ya Chama chake na Tanzania kwa ujumla
Kwakweli kitendo hicho kilitutoa machozi kila mmoja wetu, akina dada tuliokuwa nao walilia sana hata tukashindwa tufanyaje
Na hii ndiyo sababu pekee katika maisha yangu inayonifanya niheshimu sana Chama Cha Mapinduzi nikiamini kuwa napaswa kumpa baba yetu wa Taifa heshima yake
Kwahiyo binafsi naheshimu CCM kwasababu ya heshima ya baba wa Taifa na sio uchawa kama baadhi ya Watanzania wanavyonituhumu
Naamini kuwa baba wa Taifa anapaswa kupewa heshima yake na hasa katika mambo yake yote aliyoanzisha hasa Chama Cha Mapinduzi na miradi ya Taifa la Tanzania
Labda kama vijana tungekuwa na Chama chetu cha kisela sela tungeweza kudhalilishana humo na kukabana koo lakini Chama cha Mwl Nyerere kamwe sithubutu, mtanisanehe!
Babu apewe heshima yake!
Vijana mkianzisha Chama cha kisela sela niiteni lakini cha Mwl Nyerere CCM tukipe heshima yake
Ni vigumu sana kutamka Chama Cha Mapinduzi pasipokutamka baba wa Taifa
Inawezekana ningekosa adabu labda kama nisingekuwa nimesafiri kwenda nchi za Kigeni lakini kwa heshima ya wageni wanayotupatia na hasa wakigundua sisi ni Watanzania hakika inatugusa sana
Safari yangu ya mwisho ya Afrika katika nchi ya Rwanda ilinigusa sana kwasababu raisi wa Rwanda Paul Kagame alimzungumzia Mwl Nyerere kwa hisia kubwa akilenga namna gani Tanzania imekuwa nchi ya kuigwa mfano hasa wanapokumbuka undugu na ujamaa kati yetu
Wakati mwingine tunapofika Wiingereza na Marekani tunatokwa na machozi kwasababu Wazungu wanatueleza historia ya uhusiano wao na baba wa Taifa Mwl Nyerere na hasa Chama cha Mapinduzi wakitueleza jinsi baba wa Taifa alivyokuwa akiwasumbua wakati akiomba uhuru
Tulipokuwa Wiingireza Wazungu walituonesha sare za Chama cha Mapinduzi za mwaka 1995 kwakweli tukapigwa butwaa
Walitueleza baba wa Taifa aliwapa sare hizo kama zawadi ili wajionee hatua za maendeleo ya Chama chake na Tanzania kwa ujumla
Kwakweli kitendo hicho kilitutoa machozi kila mmoja wetu, akina dada tuliokuwa nao walilia sana hata tukashindwa tufanyaje
Na hii ndiyo sababu pekee katika maisha yangu inayonifanya niheshimu sana Chama Cha Mapinduzi nikiamini kuwa napaswa kumpa baba yetu wa Taifa heshima yake
Kwahiyo binafsi naheshimu CCM kwasababu ya heshima ya baba wa Taifa na sio uchawa kama baadhi ya Watanzania wanavyonituhumu
Naamini kuwa baba wa Taifa anapaswa kupewa heshima yake na hasa katika mambo yake yote aliyoanzisha hasa Chama Cha Mapinduzi na miradi ya Taifa la Tanzania
Labda kama vijana tungekuwa na Chama chetu cha kisela sela tungeweza kudhalilishana humo na kukabana koo lakini Chama cha Mwl Nyerere kamwe sithubutu, mtanisanehe!
Babu apewe heshima yake!
Vijana mkianzisha Chama cha kisela sela niiteni lakini cha Mwl Nyerere CCM tukipe heshima yake