Watanzania Tuache Kukurupuka Ovyo

Watanzania Tuache Kukurupuka Ovyo

Sheikh wangu haya mambo unapotaka kujadili kwanza uwe na akili zako timamu, bila kutia utimu, uchama wala udini.. kifupi uwe NEUTRAL

Ujue hata hao askari wanapoanza uchunguzi wao tuseme,mtu kafa kwa kupigwa kisu, ama kauwawa bila kuibiwa kitu. Kuna vitu huwa wanavishuku.
Mfano alikorofishana na nani, mawasiliano yake n.k

Kuna shida gani watanzania wanaohisi ni serikali kisa ametoka kuisema serikali.
Shida ipo kubwa sana kuna mentality moja tunaipandikiza katika nchi hii kwamba kila jambo baya ni la serikali au polisi

Kama kweli wananchi wanatoa hisia zao kwanini wote mnatoa lawama kwa serikali na polisi tu?

Sijaona hata mtu mmoja akiwa na.mtazamo tofauti juu ya kadhia hiyo

Busara ni kusubiri uchunguzi kisha ndio muwe na haki ya kujaji kutokana na matokeo ya uchunguzi huo

Mimi sipo upande wowote ule nimesimamia katikati nikisubir taarifa ya polisi,hapo sasa ntakuwa katika nafasi ya kupima taarifa yao
 
Hapo kwenye bold;
1. Wewe hujakurupuka
2. Wewe hujalaumu?
3. Wewe hujadandia mambo?
Kwa mtazamo wako kuwaambia ukweli ndio nimekurupuka? Au mlitaka niwe kama nyie nami niimbe wimbo ule ule "polisi hao"
 
Kwa mtazamo wako kuwaambia ukweli ndio nimekurupuka? Au mlitaka niwe kama nyie nami niimbe wimbo ule ule "polisi hao"
Wewe umeimba wimbo wa WATANZANIA HAO. Wengine wameimba wimbo wa polisi hao. Hapo tofauti yenu ni nani analaumiwa, lakini wote mmnalaumu
 
Shida ipo kubwa sana kuna mentality moja tunaipandikiza katika nchi hii kwamba kila jambo baya ni la serikali au polisi

Kama kweli wananchi wanatoa hisia zao kwanini wote mnatoa lawama kwa serikali na polisi tu?

Sijaona hata mtu mmoja akiwa na.mtazamo tofauti juu ya kadhia hiyo

Busara ni kusubiri uchunguzi kisha ndio muwe na haki ya kujaji kutokana na matokeo ya uchunguzi huo

Mimi sipo upande wowote ule nimesimamia katikati nikisubir taarifa ya polisi,hapo sasa ntakuwa katika nafasi ya kupima taarifa yao
kushambuliwa kwa Kitima polisi wamemkamata siku hiyohiyo mtu mmoja, LAKINI ALIMMIMINIA LISU RISASI HADI LEO HAJAJULIKANA
 
kushambuliwa kwa Kitima polisi wamemkamata siku hiyohiyo mtu mmoja, LAKINI ALIMMIMINIA LISU RISASI HADI LEO HAJAJULIKANA
Kwahiyo ulitaka nae achele kukamatwa au?

Nimeona watu wengi wanahoji haya,sasa kuna uhusiano gani wa kuchelewa kukamatwa kwa wahusikwa wa mheshimiwa Lissu na kesi ya padre?

Jamani ebu tusiendeshwe na hisia zetu,tukubaliane na ukweli kwamba kwa kila tukio kuna mazingira tofauti
 
Unaakili ndogo wewe, hulijui Hilo jeshi lilivyo na hila. Kama uswahilini ukizingua mtu anakukodia watu wakudhuru alafu anawalipa elfu 50 tu na wanakuja kukudhuru....itakuwa Hilo jeshi, mbona mambo madogo sana haya kuelewa au wewe Bado kichwa kizito sana ndg yangu😄
 
Unaakili ndogo wewe, hulijui Hilo jeshi lilivyo na hila. Kama uswahilini ukizingua mtu anakukodia watu wakudhuru alafu anawalipa elfu 50 tu na wanakuja kukudhuru....itakuwa Hilo jeshi, mbona mambo madogo sana haya kuelewa au wewe Bado kichwa kizito sana ndg yangu😄
Nikwambie kitu expert wangu?

Hakuna kitu rahisi hapa duniani kama kutoa lawama

Tafakari!
 
Shida ipo kubwa sana kuna mentality moja tunaipandikiza katika nchi hii kwamba kila jambo baya ni la serikali au polisi

Kama kweli wananchi wanatoa hisia zao kwanini wote mnatoa lawama kwa serikali na polisi tu?

Sijaona hata mtu mmoja akiwa na.mtazamo tofauti juu ya kadhia hiyo

Busara ni kusubiri uchunguzi kisha ndio muwe na haki ya kujaji kutokana na matokeo ya uchunguzi huo

Mimi sipo upande wowote ule nimesimamia katikati nikisubir taarifa ya polisi,hapo sasa ntakuwa katika nafasi ya kupima taarifa yao
Shida historia inawahukumu, matukio mangapi yametokea, wao wanakana!?

We unaamini kama wamefanya wao, uchunguzi utaleta jibu la maana,
Hebu jaribu kukumbuka matukio yoote utapata jawabu.
 
Hivi wewe na akili timamu unaweza kukaa na kukubaliana na report ya polisi wa Tanzania hii?? Hasa kwenye maswala yenye mlengo wa kisiasa?

Kwanini ashambuliwe siku chache baada ya kuikosoa serikali ya mama Yako kuhusu uonevu kukithiri nchini??

Kama ambayo mama Yako anapenda sifa kwenye Kila jambo zuri linalofanyika nchi hii kwa Nini mabaya tumkwepeshe??
Na hiyo ndio hoja yenu kubwa,je kila anaye kukwambia nitakushughulikia ni lazima ni huyo tu ndiye atakushughulia

Je vipi kama padre ana uhasama na watu fulani fulani wakatumia nafasi hiyo kumdhururu kwa kujua lawama zitakuja kwa polisi na serikali

Umeshaliwaza hilo?
 
Shida historia inawahukumu, matukio mangapi yametokea, wao wanakana!?

We unaamini kama wamefanya wao, uchunguzi utaleta jibu la maana,
Hebu jaribu kukumbuka matukio yoote utapata jawabu.
Ndio maana natoa ushauri kwamba,mlaumu pale watakapotoa ripoti,hapo mtakuwa mpo sahihi

Mfano Mnyika baada ya polisi kusema kuna watu haijawakamata,lakini baadae ikagundulika kuwa wapo walio kamatwa lakini hawakufikishwa kituoni na ushahidi ukatolewa

Sasa na nyie msubiri ripoti kisha mje na hoja zenu pamoja na ushahidi,hapo mtakuwa na haki ya kutoa lawama

Tuache kujenga msingi wa yaliyopita,maana ukijengea hapo basi kila lawama mtaipeleka kwa polisi na serikali

Tusubiri
 
Umenena vyema

Umenenepa vyema sana,lakn wananchi wanaonekana wamechoka na hiz kauli za uchunguz unaendelea kila sku ,mfano Ben Saa 8 ,alipotea na uchunguz unaendelea,Lissu alitandiea risas mchana Tena makao makuu ya nchi na Bado uchunguz unaendelea ,Azory nae alichukuliwa na watu na Bado uchunguz unaendelea, mzee Kibao naye alichukuliwa kwenye basi akauliwa mchana kwepie na uchunguz unaendelea,tukaona watu wakijarb kuteka kjana mmoja juz juz wakashndwa na jaribio,alaf Wazir nape aliwahi tolewa bastola mchana kweupe mbele ya waandish wa habar na camera zao lakn pakawa kimya,,!! Ni vzur JPT likajitenga na huu uovu mbali na ivyo uenda watu wakafkia mwsho wakaona Bora wajilinde wao
Asante sana expert wangu,nakubaliana na wewe moja kwa moja kwamba polisi kwa upande wao wanastahiki lawama kwa hayo unayo yazungumzia,maana habari ni zile zile kila kukicha,na ndio maana wananchi wanafikia tamati ya hayo wanayo sema

Mimi sisemi serikali wala polisi haina makosa kwa baadhi ya mambo,ni kweli wana mazuri na mabaya yao,lakini napinga kwa kila tukio basi ndio iwe fimbo ya kuwachapia,hapana hii sio sawa

Ifike kipinde tuyaangalie mambo katika mtazamo tofauti na ule tuliozoea
 
Kwa bahati mbaya unazidi kuwachafulia.
Hakuna marefu yasiyo na ncha.

Anyway ajaye ni me (mkristo)
 
Siku zooote hakuwahi kujeruhiwa baada tu ya kuanza kukosoa mwenendo wa Serikali ghafla kajeruhiwa, mtuhumiwa namba moja ni nani?
Tatizo kakutwa na tatizo katika wrong place,alikuwa anakunywa kinywaji,je kuna anayejua baada ya kulewa aligombana na nani?

Pili ninaweza nikawa nina uadui na wewe,nasubiri mtu mwingine akosane na wewe kisha nami nifanye yangu

Je umeshawi kuliwaza hilo?
 
Back
Top Bottom