Watanzania, Msichaguwe Chama Chagueni Kiongozi

Watanzania, Msichaguwe Chama Chagueni Kiongozi

But Faiza michakato inaanzia kwenye vyama...
Yaani kama wewe Faiza nadhani unaweza kuwa diwani wangu siwezi kukuchagua hadi uombe kupitia chama chako, wakujadili kisha ndio waniletee mimi jina lako (pengine na la mshindani).
Pili ni vigumu sana uwezo wa mtu kujulikana kama hajapata fursa ya kuuonyesha. Hapo ndipo inakuwa advantage kwa waliopo kwenye uongozi wa vyama, serikali au harakati za kijamii.
 
Katika mambo yote sina ugomvi na binti wewe, hata katika kuitetea CCM au Rais Jakaya kikwete, maana ndiyo mapenzi yako.

Mahali pekee ambapo huwa unaudhi kupindukia ni udini, hasa pale anapotaka kila kitu tuongelee kwa mtazamo wa uislam na ukristo. Hupo pekee, wapo na wengine. Hawa wengine hawanikeri sana maana kadiri ya maandiko yao tu unajua kuwa huyu upeo wake ni mdogo au hana kabisa.

Kwenye hoja yako ya kutaka achaguliwe mtu na siyo chama, nakubaliana nawe kiasi lakini natofautiana nawe zaidi.

Nakubaliana nawe kwenye ngazi za chini, kama vile vijiji lakini unapokuja kwenye ngazi ya Taifa ni muhimu pia kutazama sera za chama, umadhubuti wa chama katika kusimamia maamuzi, kupiga vita rushwa na ubunifu wa chama katika kuandaa sera zinazotekelezeka kutokana na ubunifu wa mipango iliyopo.

Nchi kama Singapore imefanikiwa sana kiuongozi, kiutawala na kiuchumi kwa sababu wao mfumo wao ni wa kuchagua chama, na baada ya hapo chama kilichoshinda humchagua Rais baada ya kupitia mchakato mgumu na wa kina. Kuna wakati chama kilichokuwa kimeshinda kilitamka wazi kuwa hakikuwa na mwanachama ndani ya chama chao aliyewathibitishia kuwa ana uwezo wa kutimiza ambayo chama kiliwaahidi wapiga kura. Chama kilimwomba mfanyabiashara awe mwanachama, na kisha kikamkabidhi madaraka ya Urais. Singapore wanasema, siyo rahisi mwananchi wa kule Muze (Rukwa) au Nakapanya (Ruvuma) kufahamu kwa uhakika kabisa kama Kikwete ana uwezo wa kuwa Rais bora au hapana, wao ndani ya chama ndiyo wanaojua.

Utawala wa CCM umetupa fundisho kubwa kuwa ili tupate mabadiliko hatustahili tu kumpigia kura mgombea pekee yake bali ni pamoja na chama. Mara kadhaa tumewachagua wagombea wazuri kupitia CCM lakini wakifika bungeni au wanapoteuliwa kuwa mawaziri wameshindwa kabisa kutimiza yale waliyowaahidi wananchi. Ukikaa nao mmoja mmoja watakuambia kuwa wanashindwa kuleta mabadiliko kutokana na mfumo mbaya wa CCM wa kuwadhibiti wale wanaoenda kinyume na matakwa ya chama.

Kama tunataka kuleta mabadiliko katika nchi yetu, ni lazima tuangalie ubora wa mgombea, na tutazame mgombea huyo anatoka chama gani.

Nimesoma kitabu cha January Makamba, ukitazama aliyoyasema kuhusu Tanzania mpya ni mazuri sana lakini hayatekelezeki akiwa ndani ya CCM. Yeye anataka kuleta fikra mpya, je, CCM yenyewe ina fikra mpya? Tatizo hilo alilipata sana Mkapa na Kikwete, na kuna wakati marais hawa walijaribu kutaka kuwa na nguvu katika chama kwa kuwapeleka mawaziri wao wagombee ujumbe wa halmashauri kuu ili kuleta fikra mpya kuanzia kwenye chama, wote walipigwa chini, hawakupita. Kwa sababu wale wahafidhina wamejenga umoja fulani, na umoja wenyewe ni wa uovu. Wao wanawachagua watu kwa kuangalia nani amewapa bahasha, na huyo mgombea atampa fadhila gani. wale watu wasafi kwa sababu hawawezi kuhonga au kuahidi au kutoa upendeleo kwa wajumbe wanaopiga kura, hawapiti ndani ya CCM. Wengi wa wanaopita katika kugombea uongozi ndani ya CCM ni wale watoa rushwa, na mtoa rushwa hawezi kukosa kupokea rushwa.

Nasisitiza, ni lazima tuangalie ubora wa wagombea na ubora wa chama maana kwa mfumo wetu wa Tanzania chama kina nafasi kubwa sana katika uongozaji na usimamiaji wa serikali.

Uwanja ni wako na una haki ya kubwabwaja na kuhororoja upendavyo.

Slaa alibwagwa na Kikwete na kwa maadili mabovu aliyonayo huyo atakuwa ni chaguo lako lakini nnauhakaika hatokuwa chaguo la Watanzania wengi wanaopenda maadili mema.

Mimi sitomchaguwa Slaa hata akibaki kuwa ni mgombea pekee.
 
CCM ni chama bora katika Tanzania ni chama chenye mizizi kila kona ya Tanzania.

Ukifika uchaguzi, CCM kinakuwa na sera na ni wajibu kumchaguwa tunaeona anafaaa kuzisimamia hizo sera. Si kila mgombea anaefaa.

Mfano, Slaa anaweza kukukinaisha vipi kuwa atasimamia maadili ya mtoto wa Kitanzania wakati yeye mwenyewe kashindwa kusimamia hata maadili ya kanoni aliyoisomea? Fikiri.

Red highlighted line shows how much you're working up God anger and ua welcoming his punishement upon uaself.

Usi lazimishe hasira ya Muumba wako ikakupata, wacth out and stop ua idiotism
 
Haya ndiyo maazimio ya cc - ccm Zanzibar. Baada ya ccm kujua wamechafuka na chama chao hakikubaliki tena, waliazamia kupiga kampeni za kuchagua mtu ili watu wasiangalie maovu ya ccm!. Ff hii inajulikana.
a
Mara zote Kikwete amekuwa msaliti wa umma kwa kufuata maazimio ya chama chake. Mfano sahihi ni BMK. Amebariki mchakato na amepokea draft ya Warioba, ameikubali na akaenda mbele zaidi na ku isaini. Ccm walipoikataa kwamba haina maslahi kwao, wakapanga na namna ya kuivuruga, na bahati nzuri kwake wakamtask kuvuruga, AKAVURUGA KWA UTASHI WA CHAMA.

Amekaa na watetezi wa katiba ya wananchi, wamepatana mchakto wa katiba usitishwe, lakini ccm wakamgomea, wakaendeleza hadi hapo wlaipo sasa. Na yeye kama mwanaccm mwaminifu, ameshindwa kusimamia maazimio yale aas if hayakuwepo, na sasa anatekeleza matwaka ya ccm.

Hatutachagua mtu bila kuangalia chama chake kwa sababu chama ndicho kitakachomwongoza na kumpa dira katika uongozi wake wote!.

Acheni kudanganya watu Faizafoxy. Huyu mtu hataunda serikali nje ya chama chake, hatekelezi sera zake nje ya chama chake, hatengenezi mfumo nje ya misingi ya chama chake, hatekelezi ilani nje ya zile za chama chake. Iweje leo mseme tuchague mtu bila kuangalia chama? Hii ni nini?

Vinginevyo atangaze yeye ni mgombea binafsi hana chama, tutamwangalia kwa namna ile lakini tutahitaji kujua anaunda serikali kwa utaratibu upi iwapo anashinda.

Hii kampeni ninaona ni kutaka kuficha makovu ya ccm kwa sababu haitakiwi, halfu tujikute tumewapa uongozi waendelee kutunyonyoa wakavu wakavu!.

Aidha mtu ana chama tutamwangalia na chama chake, ama awe binafsi bila chama tutamtathimni muundo wake pendekezwa wa serikali yake ukoja.

Kuchanganyachanganya mambo hapa ni hila na hatukubali

Na mwaka 2005 Watanzania wa vyama tofauti na wasikuwa na vyama walipomchaguwa Kikwete walifata maazimio ya wapi? Au ni yale ya Askofu Kilaini "Chaguo la Mungu"? umesahau?
 
Red highlighted line shows how much you're working up God anger and ua welcoming his punishement upon uaself.

Usi lazimishe hasira ya Muumba wako ikakupata, wacth out and stop ua idiotism

Hebu andika Kiswahili, kama sikuelewi elewi vile unamaanisha nini, kwa hicho Kingereza chako cha Rombo.
 
Huyu Faiza amesoma upepo wameshaona kimbunga,wanaanza ujanja kupanga jinsi ya kupunguza Kura za Ukawa ili wapate nafuu.Nahuyo anayechaguliwa bila chama anaenda kusimamia ilani gani?.kama umeliona hilo lina maana mbona kwenye katiba yenu swala la mgombea binafsi mumelikanyaga kanyaga halieleweki? Siwezi kukuunga mkono kwa mawazo hayo yakutapatapa!
 
Huyu Faiza amesoma upepo wameshaona kimbunga,wanaanza ujanja kupanga jinsi ya kupunguza Kura za Ukawa ili wapate nafuu.Nahuyo anayechaguliwa bila chama anaenda kusimamia ilani gani?.kama umeliona hilo lina maana mbona kwenye katiba yenu swala la mgombea binafsi mumelikanyaga kanyaga halieleweki? Siwezi kukuunga mkono kwa mawazo hayo yakutapatapa!

Na mwaka 2005 Kikwete alipochaguliwa na Watanzania bila kujali vyama vyao mlikiona nyinyi kimbunga? Fikiri.

Maneno yangu yasome kwa umakini na uelewe kuwa nchi haiongozwi na chama, kwanza unajiongoza wewe mwenyewe kisha wewe ndiyo mwanachama na unatakiwa uelewe unataka chama chako kifanye nini, Siyo kuburuzwa kama msukule na akina Mtei.
 
But Faiza michakato inaanzia kwenye vyama...
Yaani kama wewe Faiza nadhani unaweza kuwa diwani wangu siwezi kukuchagua hadi uombe kupitia chama chako, wakujadili kisha ndio waniletee mimi jina lako (pengine na la mshindani).
Pili ni vigumu sana uwezo wa mtu kujulikana kama hajapata fursa ya kuuonyesha. Hapo ndipo inakuwa advantage kwa waliopo kwenye uongozi wa vyama, serikali au harakati za kijamii.

Vyama ni wanachama na si wenye vyama, kumbuka hilo.
 
Wanaanza kupunguza upana wa goli lao wakati wa match.Teh teh teh!.Subirini kiama kinakuja.Mbona swala hilo haukulisema tangu chaguzi zilizopita?.Au mgao wa buku 7 unaanza kuwa mashakani?
 
Ikiwa hata mtu akiiga sauti ya wachungaji wa jangwani unateseka basi hakika wewe FF una pepo mchafu. Fanya haraka ukaombewe hapo jangwani wachungaji wakiitisha mkutano.

Nakereka "siteseki", usitie maneno yako kinywani mwangu. Au ndivyo Sunday school unavyofundishwa? kubadili yaliyokuwepo ukaweka yasiyokuwepo?
 
Wakati tunaingia kwenye mwaka wa heka heka za uchaguzi wa Wabunge na wa Rais.

Nawaasa Watanzania wasichaguwe chama bali wachaguwe kiongozi.

Mfano mzuri ni kama tuliouonesha mwaka 2005, wakati tulipomchaguwa Kikwete kuwa kiongozi mkuu wa nchi hii. Ushindi alioupata Kikwete wa zaidi ya kura 80% ni dhahiri ulikuwa si kwa kuchaguliwa na wana CCM bali hata wa upinzani na wasio na vyama.

Mfano mwingine ni wa John Shibuda, pale alipoihama CCM na kuhamia Chadema, wana CCM wa jimbo lake wengi walimpa kura zao bila kujali yupo chama kipi. Huo ni uzalendo na unaonesha jinsi Tanzania tunavyoweza kufanya maamuzi bila ya kuburuzwa na chama au wenye chama.

Viongozi wazuri tunao, tena tusingoje wale wanaojitokeza tu kuzitaka hizi nyadhifa kwa udi na uvumba. Tutazame katika jamii, tunapomuona anaefaa kuongoza, hata kama si mwanasiasa, bali tukimuona kuwa haa huyu anafaa kuongoza, tumlazimishe, tumsimamishe, tumchaguwe.

Tukianza kuchaguwa viongozi na si chama tutakuwa sisi wenyewe tumeshakuwa viongozi.Tuanze kwa kujiongoza wenyewe kwa kuchaguwa tukitakacho na si kuburuzwa na wakitakacho wenye vyama.

Tukianza hivyo, hata vyama vyetu vitaweka viongozi tuwatakao na si wawatakao wenye vyama.

Nasema haya kwa kuwa nimeona katika vyama vyetu vya siasa vyote, kuna tabia ya kura za maoni. Wananchi wanaweza kuwa na mgombea wao wakampendekeza agombee lakini ikifika kwenye vyama wanakatwa na kuwekwa wale wawatakao wenye vyama. Hii si demokrasia tuitakayo na huleta uvunjifu wa amani.

Ni wakati muafaka sasa Watanzania tusikubali kuchaguwa wamtakae wenye vyama, tunataka tuwe na viongozi tuwatakao wananchi tulio wengi. Tunataka na wagombea huru, wasio na vyama pia wawepo, ili tuwachaguwe tuwaonao wanatufaa na si wanaowafaa wenye vyama.

Mmh!leo nimeona ajabu sana,anyway,wazo lako ni zuri sana mkuu,nakuunga mkono.Tukifanya hivyo,basi tutakuwa tumepiga hatua moja mbele na tz yetu.
 
Nafikiri labda haulewi maana ya Demokrasia, ngoja nikupe mwanga kidogo, unajua ni kwanini Nchi nyingi Duniani zina machafuko?
Ni kwa sababu hiyo uliyoipendekeza. Wananchi wa hizo Nchi wanachagua Watu na SIYO chama na mfano mzuri ni Kenya, Nchi hiyo ina shida kubwa ya vurugu kwa maana Wananchi wa hiyo nchi hawachagui Chama (sera) bali wanachagua Mtu/Watu!

Sisi nchini kwetu ni lazima tujione ya kuwa watu wenye Bahati sana angalau bado tunachagua Vyama kwa maana ya sera na SIYO Mtu!

Na hii inatusaidia sana pmj na matatizo yetu yote lkn hakuna mwenye hati miliki ya Watz kama unavyotaka kupendekeza, kwa mfano leo hii Wapinzani wengi wanampenda Bw.Slaa lkn wanampenda kwa maana yuko CHADEMA yaani wanapenda Sera za CHADEMA lkn Bw.Slaa akitoka CHADEMA basi ndiyo mwisho wake kwani hakuna atakayemfwata tumeona ya Zito Kabwe alipokuwa CHADEMA watu walimpenda sana lkn SIYO kwa sababu ya yeye kama ZIto Kabwe Hapana bali ni kwa sababu ya SERA za CHADEMA sasa akitoka (Zito) hakuna atayemfwata na huyo ndio mwisho wake na ndio maana amejaribu kutingisha kiberiti kuona kama CHADEMA ni yeye ama vipi lkn matokeo yake ameyaona ya kwamba CHADEMA SIYO Mtu bali ni Chama hata huko Kigoma anakotoka Wananchi wanapenda CHADEMA na SIYO Mtu(Zito), vile vile CCM watu wengi wanampenda Bw.Lowasa lkn ni kwa sababu yuko CCM na akitoka CCM ndiyo mwisho wake hakuna atayemfwata na watu watabaki CCM!

Mfano mzuri ni Mrema ndiyo watu walimpenda lkn pia Walipenda NCCR Mageuzi lkn alipotoka NCCR hakuna aliyemfwata!

Hivyo Tanzania sisi ni model ya Bara zima la Afrika kwani kwetu Siasa SIYO Mtu bali ni Chama na tunachagua Sera na hatuchagui Mtu, na hii ni bahati kubwa sana na Mungu azidi kutubariki kwa kuliona hili mapema! !

Wacha porojo wewe, Kenya hata vyama vyao ni vya kibaguzi na kikabila kama ilivyo chadema Tanzania.

Na hiyo sera unayoichaguwa imeandikwa na nyani si watu? na wakuitekeleza na kuisimamia hiyo sera ni nani kama si mtu? Fikiri.
 
Na mwaka 2005 Kikwete alipochaguliwa na Watanzania bila kujali vyama vyao mlikiona nyinyi kimbunga? Fikiri.

Maneno yangu yasome kwa umakini na uelewe kuwa nchi haiongozwi na chama, kwanza unajiongoza wewe mwenyewe kisha wewe ndiyo mwanachama na unatakiwa uelewe unataka chama chako kifanye nini, Siyo kuburuzwa kama msukule na akina Mtei.

Kiukweli hata leo nimechangia uzi wako kwa bahati mbaya tu kwa sababu huwa sioni point kwenye mijadara unayoanzisha tofauti na propaganda za kuwagawa wasioelewa hasa za Udini,Ukanda na Ukabira.Kwa kifupi tu huwa nakudharau sana kwa sbb kichwa chako kimefugia nywele tu na ndio mana umekifunika nahilo tambala jeusi, lakini ndani kiko wazi.Na hivi sichangii tena kwa leo Uzi huu
 
Wacha porojo wewe, Kenya hata vyama vyao ni vya kibaguzi na kikabila kama ilivyo chadema Tanzania.


Nimekwambia Kenya watu hawachagui Chama bali wanachagua Watu na wanawafwata na ndio maana kuna vurugu, sisi kwetu hatuchagui Mtu bali tunachagua Chama na ndio maana (mpaka sasa) hatuna vurugu!
Sasa hilo la Ukabila na CHADEMA sikuelewi unamaanisha nini embu fafanua kwa maana ni geni kwangu!
 
Swali moja ambalo ukipenda jibu usipopenda unaweza kulipotezea, kwa udhaifu huu unaouna kwenye mgombea binafsi, kwenye kura ya maoni ya katiba mpya utapiga kura ya ndio ama hapana. Kumbuka ukisema ndio itakuwa imetoka na udhaifu huo lakini ukisema hapana tutapata mwanya wa kurekebisha udhaifu huo na kukuweka kifungu hiki cha mgombea binafsi sawa. Kuanzia hapo huu ushauri wako wa wananchi wachague mtu na sio chama itakuwa imepata ufumbuzi. Nangoja mtazamo wako. Nikupongeze kwa kuleta mada yenye tija leo. Asante

Siipigii kura yoyote Katiba inayopendekezwa si kwa sababu hiyo uliyoiweka bali ni kwa sababu haijatambuwa kiuwazi uwepo wa Mahakama ya Kadhi Tanzania. Kumbuka hilo.

Kwa hiyo hakuna atakaeipata kura yangu, si wa ndiyo wala si wa hapana.
 
...Nasema haya kwa kuwa nimeona katika vyama vyetu vya siasa vyote, kuna tabia ya kura za maoni. Wananchi wanaweza kuwa na mgombea wao wakampendekeza agombee lakini ikifika kwenye vyama wanakatwa na kuwekwa wale wawatakao wenye vyama...

Well said dada FaizaFoxy. I hope Kinana, Mangula na Dr. Slaa ujumbe huu umewafikia.
 
Hebu andika Kiswahili, kama sikuelewi elewi vile unamaanisha nini, kwa hicho Kingereza chako cha Rombo.

Utaelewaje wakati umefaulu darasa la saba hujui kusoma, kuandika na kuhesabu.

Form 6 English course nenda.
 
Nimekwambia Kenya watu hawachagui Chama bali wanachagua Watu na wanawafwata na ndio maana kuna vurugu, sisi kwetu hatuchagui Mtu bali tunachagua Chama na ndio maana (mpaka sasa) hatuna vurugu!
Sasa hilo la Ukabila na CHADEMA sikuelewi unamaanisha nini embu fafanua kwa maana ni geni kwangu
!

Sasa wewe unachobisha nini? nakwambia Kenya hata vyama vyao ni vya kikabila, unafikiri mgombea atakuwaje?

Tanzania ni lini kikachaguliwa chama? kasome tena post namba moja uone mifano niliyokuwekea, na hili nililolileta hapa si jipya, ni kuwakumbusha tu, msidanganyike mkachaguwa chama badala ya kiongozi.

Usitake kunchekesha kuhusu chadema, hata mwenda'zimu anajuwa kuwa kile ni chama cha wachagga.
 
Back
Top Bottom