Watanzania mnajionaje?

Watanzania mnajionaje?

Sasa dunia hii ina vichaa wangapi wanaotaka kufanya ukichaa wao wenyewe?

Na mimi nitafuatilia wangapi?

Miezi michache nilimpigia simu binamu yangu mmoja yupo Geneva, Switzerland. Baba yake mtu mkubwa sana serikalini. Na alikuwa katoa habari fulani kuhusu mkutano wa Davos. Sasa mimi mara nyingine nikitaka kufuatilia hizi habari sisomi magazeti wala kusikiliza kauli rasmi, napiga simu kuongea na watu wenye access na hizi habari kama wanafamilia, wanafunguka vizuri sana.

Nikamuuliza binamu yangu, mbona baba yako hajaenda Ulaya kutuwakilisha? Mbona Tanzania tunajifungia sana watu hawatembei kwingine duniani kutafuta biashara?

Akaniambia, binamu yangu, wewe si uko Marekani huko? Nikamwambia ndiyo. Ushajipatia makaratasi yote ya kuishi kama raia poa tu? Nikamwambia ndiyo. Akasema safi sana. Sahau hawa Watanzania na siasa zao. Wewe hakikisha familia yako iko fresh na watu wako wa karibu wako poa. Hao Watanzania siasa zao waachie wenyewe wanazijua wenyewe. Zitakuumiza kichwa tu.

Nikaona duh. Mimi huwa nakuwa na kisirani cha kufunga vioo, lakini huyu zaidi.

Lakini alinipa somo kubwa.

Mara nyingine tunahangaikia mambo ya "Watanzania" wakati hata tukiulizwa "Mtanzania" ni nani hatuwezi kumtaja.

Sitaweza kuacha kufuatilia siasa za Tanzania kama alivyoshauri yeye. Lakini pia sitakesha kufuatilia habari za "Watanzania wakoje?" bila msingi maalum.

Sorry if I come off snobbish or uppity. That is just how I feel.
 
Kiranga Michango yako huwa naiheshimu sana bro....

Heshima kwako....
Asante sana.

Na mimi ningekuja hapa kutaka kila Mtanzania awe kama mimi ninavyotaka pangetosha?

Mara nyingine inabidi tuweze kuchukuliana na kufurahia tofauti zetu.

Ndiyo maana kuna siku asubuhi naweza kuingia Jamii Intelligence nikajadili Poincare's conjecture and the shape of spacetime as described by Roger Penrose in "The Road To Reality: A Complete Guide To The Laws of The Universe" na jioni nikawa chit chat nasoma habari za Bongo Celebrity wanavyofukuzana. Na hata nikajimix kuchombeza kuchangia watu wakashangaa Kiranga unafika mpaka huku kona kona za "Uwanja wa Fisi"?

Sasa mimi napenda kuwa mtu wa watu. Kujichanganya full blast.

Sasa kama mtu hajui nondo zako za Jamii Intelligence anakukuta chit chat anaweza kuona jamaa liko shallow sana limejichanganya huku hili.
 
Najiona tofauti kidogo na Watanzania wengi.. Kama yupo Mtz makini kama me ataungana na mimi kuuliza, mnajionaje??
Mkuu acha dharau kwa sisi watz,huku ndiko kwenye asili yako.
Unamdharau hata baba na mama yako kisa tu unaishi nje? Andika wosia mapema ukifa uzikwe/uchomwe moto huku huku nje.
Endapo utatambulika pindi utakapo kufa,kwa jeuri na nyodo zako ukiletwa Tz bakora ni halali yako.

Utadhani unaishi peponi!!?)) 😡 😎
 
Vizuri kama umeelewa, nachotaka kusema ukweli hauvishwi nguo otherwise tunachelewa sana kwa kudhan ukweli usipova nguo ni udharilishaji. Ni mtazamo wako juu ya uwasilishaji.
Ukweli una vazi lake mkuu na vazi jenyewe ni busara, endapo ukweli ukiunyima hilo vazi basi ujumbe au huo ukweli hautafika moja kwa moja kwa mlengwa zaidi utampa mtihani wa kuanza kukuchambua wewe zaidi badala ya unachokiwasilisha......
 
Ukweli una vazi lake mkuu na vazi jenyewe ni busara, endapo ukweli ukiunyima hilo vazi basi ujumbe au huo ukweli hautafika moja kwa moja kwa mlengwa zaidi utampa mtihani wa kuanza kukuchambua wewe zaidi badala ya unachokiwasilisha......
You are misusing that term.

I thought it was a simple msg to understand .. beta end this discussion
 
Niliwahi kufanya kazi Wall St. na dada mmoja Mkorea, Korean American.

Yule dada mtu poa sana. Anapiga kazi kama hana akili nzuri, yuko serious vizuri (usinywe naye pombe tu happy hour, anaweza kukuparamia maana akili zote zinamtoka).

Basi yule dada by all accounts nilikuwa namuona mtu well balanced. Isipokuwa kitu kimoja tu.

Anawachukia Wakorea wenzake kichizi.

Yani ukitaka kumchafua aanze kupaka mtajie habari za Wakorea. Si Wakorea wa Marekani si Wakorea wa North Korea, si Wakorea wa South Korea.

Anawapaka vibaya sana. Uzuri wake sijawahi kumsikia akibagua Waafrika au watu wengine wowote.

Yeye ni Wakorea tu.

Granted kuna Wakorea wanastahili maneno yake, lakini obviously alivuka mpaka.

Kuna kitu katika psychiology kinaitwa "self hate". Unaweza kujichukia wewe mwenyewe au ukachukia watu wa taifa lako. Inawezekana kabisa ukajiaminisha unawapenda ndiyo maana unachukia mambo yao fulani.

There is a whole Wiki about Self hating Jews for example.

It is here Self-hating Jew - Wikipedia

Mind you, I don't have any problem with being self critical. In fact I have been self critical of myself and Tanzanians in many occassions. But when the negativity is unchecked, this self critical nature turns into self hate.

Tanzanians are too diverse and numerous to be categorized in an overly monolithic way.
 
Mtanzania ndie kaja na wazo la kuanzisha jukwaa hili ambalo wewe umepata nafasi ya kulitumia kuandika ' uharo' wako huu hapa, twambie labda ni lipi sasa la maana ambalo wewe umelifanya ktk jamii. Huwezi kukejeli wana Jf na watanzania kwa ujumla pasi na ssb ya msingi. Acha ulimbukeni kijana!
 
Nisikitike sana SANA! Mambo ninayoyaona kwa Watanzania wengi hapa Nchini na hata nje ya TZ .. Dah! ni ASANTE. Tabia zenu HAZIELEZEKI, hazieleweki! Yaani ikitokea nimeishi na Mtz ama kufanyakazi na MTz hua ni changamoto kwelikweli!

Binafsi si mchangiaji sana hapa JF cuz most of your posts sio maisha ya ulimwengu huu kidogo twitter ina reflect life lkn hapa JF .. bla bla bla nothing serious. Huwa nafurahia sana ku- socialise na watu wa nje kuliko watu hapa Tz. Kama nakosea samahani sana ila nayasema tu kwa nia nzuri. Zungumzia U - Great thinker utabaki kwa MAX na crew yake, kidogo Biashara uchumi na ujasiriamali alikuepo Ontario wengine wooote, ni ASANTE kwa kweli. HAMNA KITU

Nikifikiria kuhusa hapa nyumbani styl ya maisha mlionayo kwa ujumla hua nachoka, wakati mwingine nakosa usingizi kabisaa .. tujivunie nini TZ? Yan ni aibu (kitu sipendi maisha yangu yote). Entertainment hakuna, Siasa safi hakuna, Uadilifu zero, Uchapakazi hakuna, Time management zero! Yani ni changamoto!! You are not existing in reality, You are not existing in this world life.

Franky, nmeishi na kufanya kazi na Nigerians, Rwandese huko nje, And am not sorry to say I envy these Ppl.

Et kwani Watz mnajionaje?
Jifunze kuandika kwanza
 
Back
Top Bottom