marveljt
JF-Expert Member
- Jan 11, 2017
- 1,503
- 1,479
Tatizo ninaloona pale ITV na redio one ni kuwa na majina makubwa ya vipindi lakini contents za ovyo.
Mfano kile kipindi cha dakika 45 kila kipindi kuanzishwa kwake ni kunasibu japo kidogo kipindi cha hard talk(BBC) au kile cha Riz Khan lakini cha kushangaza badala ya kuwabana waalikwa kwa maswali na hoja nzito wao wanatoa platform ya waalikwa kutamba na kujisifu watakavyo na ndio maana waziri/mkurugenzi/mbunge akialikwa akatai tena nasikia wengine wanaomba kualikwa. Hii yote ni udhaifu wa mhariri na mtangazaji.
Wanaoendesha hivyo vipindi ni wasoma habari na si wanahabari.msoma habari hawezi kubwa na Mawazo ya maswali magumu yenye kumfikirisha mwalikwa.hivyo vipindi wanatakiwa wanataaluma haswa siyo wenye PhD za kwakiembe