GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,646
- 10,860
Sidhani kama kuna Mtanganyika yeyote aliyeukataa uwekezaji! Kinachopigiwa kelele ni mapungufu yaliyopo kwenye huo mkataba. Kama mapungufu yatarekebishwa, mwekezaji anakaribishwa kwa mikono miwili. Kinyume na hapo, bora tubaki na bandari yetu.Serikali haipaswi kuacha mipango ya kuleta mwekezaji bandarini , suala la mapungufu ya mkataba yaangaliwe.
Hoja kwamba nchi yenye watu milion 60 kushindwa kuendesha Bandari NI hoja mufilisi kabisa na ni hoja ya mtu asiye na uelewa kuhusu Bandari.
Bandari si stand ya Magufuli au Nyegezi kwamba inahudumia Zaid mabasi ya mkoani.
Bandari inaangaliwa kuhudumia Dunia au mataifa kadhaa.
Nani au kampuni gani ya Kitanzania utaipa iendeshe Bandari Kwa ufanisi wa kushindana kidunia?
Hakuna Mtanzania au kampuni yoyote ina msuli wa kuweza kuisimamia Bandari ikaweza kuleta ushindani Duniani.
Hatuna Mtanzania yeyote anayeweza kuingia top 1000 ya matajiri Duniani ,, iweje tuwe na kampuni yenye uwezo huo?